Jumanne, 23 Mei 2017

NGAMBO YA YORIDANI, Sehemu 2.

Na Mwalimu Oscar Samba  Ug Ministry 
Yesu akawambia wanafunzi wake, “Natuvuke mapaka ng’ambo ya ziwa” Luka 8:22. Kisha mbele yake kukatoke dhoruba kali iliyolenga kuwazuia wateule hawa wa Mungu kulifikia kusudi la Mungu lilopo ng’ambo ya Ziwa.

Mariko 4:37Ikatokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi yakakipiga chombo hata kikaanza kujaa maji. 38 Naye mwenyewe alikuwapo katika Shetri, amelala juu ya mto; wakamwamsha, wakamwambia, Mwalimu sii kitu kwako kuwa tunaangamia?” 39 Akaamka, akaukeme upepo, akaiambia bahari, “Nyamaza utuliye!” Upepo ukakoma, kukawa shwari kuu.

Wanafunzi wa Yesu walitambua fika ya kwamba inawapasa kufika ng’ambo ya Ziwa ili kukutana na kusudi la kimungu huko kama Yesu alivyowataka wavuke, ila jaribu ama kikwazo kilitokea, na walifahau hawapaswi kupiga mbio kurudi nyuma bali ni lazima wasonge mbele. Na katika kusonga mbele upinzani upo, nawe usikubali kukata tamaa badala yake yakupasa uvuke ng’ambo nyingine ili kukutana na mujiza wako hapo.
Wana wa Iziraeli walipokuwa katika nchi ya mateso, Mungu aliwapa ahadi ya kuwapa maisha ya Mziwa na Asali lakini mambo hayo hayakutokea kirahisi hadi walipopambana na ugumu wa jangwa ama nyika.

Jangwani kulikwepo na vikwazo vingi sana ikiwemo njaa, kiu, nyoka wa moto, hali iliyosabisha vifo kwa wengi wao waliopopungukiwa na Imani. Na wewe ahadi uliyopewa na Mungu ni lazima ipitiye katika jangwa ndiposa ufike katika ng’ambo yako.
Ninakuta kuwa mwepesi wa kumkimbilia Mungu kama ilivyokuwa kwa Musa na kama nilivyokujuza kwenye sehemu ya kwanza ya makala hii.
Mungu akubariki na endelea na wokovu ila Kesho usikose kwani nimeakuandalia makala nzuri inayomtaja YESU kama mtuliza mawimbi ama dhoruba baharini.
Langu jina ni Mwalimu Oscar Samba, ninakupenda na endelea kuifwatilia mafundisho  haya pamoja na kuchota Baraka kwa kuiwezesha huduma hii kwa sadaka yako.

Kama hujaokoka na unataka kuokoa tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KAUMINI KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundila Fb, ili kuupta habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                       PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                              

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni