Jumanne, 23 Mei 2017

USILIYE.

Mwalimu Oscar Samba wa huduma ya Ukombozi Gosple
Najua umekuwa na wakati mgumu sana maishani mwako, na umelia vyakutosha, ila sasa ninakwambia usiliye tena maana Yesu amekusikia na kukuhurumia.
Kitabu kile cha Luka 7:11-17, Kinaeleza kisa cha mwanamke mjane aliyefiwa na kijana wake wa pekee, na Yesu alipoukaribia huo mji wa Naini alimuona na kisha kumuhurumia na hakuishia kumuhurumia tu, bali alimwambia; “USILIYE.”
Mara baada ya maneno hayo alitenda mujiza wa kumfufua mwanaye. Bila iyana nakufunulia maandiko hayo ili ujidhibitishiye mwenyewe.

13 Bwana alipomuona alimuonea huruma, akamwambia, “Usiliye.” 14 Akakaribia, akaligusa jeneza; wale waliokuwa wakilichukuwa wakasimama. Akasema, “Kijana nakuamuru: Inuka.” 15 Yule maiti akainuka, akaketi, akaana kusema. Akampa mama yake.


MAOMBI:  Mpendwa na kwa upako niliopewa na YESU KRISTO kama mtumishi wake ninakiamuru hicho kitu kilichokufa maishani mwako kiinuke sasa na kwa kinywa hiki ninaligusa jeneza kwa JINA LA YESU KRISTO MNAZARETI.

Amini sasa ya kwamba muujiza wako umekwisha kupatikana. Langu jina ni Mwalimu Oscar Samba mtumishi wa Huyu Mwanaume wa ajabu aitwaye YESU KRISTO.  Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com, ama ukurasa wetu wa facebook na kundi: Ug Ukombozi Gosple. #Like hiyo page na #Share ujumbe huu.
Kama hujaokoka na unataka kuokoa ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KAUMINI KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Kwa Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni