Jumanne, 23 Mei 2017

HAYUPO KABURINI AMEFUFUKA.

Mwalimu Oscar Samba
Tatizo lako halipo tena kaburini bali limefufuka na Bwana YESU, Wakati watu wakikuona wanakuona kama mtu aliyepoteza matumaini ama wengine wakikumbuka jinsi ulivyokuwa mfanikiwa ila kwa sasa maisha ni kama yamekupiga wewe tambua ya kwamba matatizo hayo ni kweli yalikwepo  ila kwa sasa yamekwisha kufufuka na YESU WALA HAYUPO TENA KABURINI. 
Mtazamo wa wengine usikutishe kwani hadi leo huko Uyaudi zipo dini zinazongonja masiya wakiamini kuwa hajaja na wapo wachache wanaoamini ya kwamba YESU hakufufuka kama viongozi wa mafarisayo na wakuu wa makuhani walivyowahonga wale walinzi na kuwataka kusema ya kwamba watangaze eti wanafunzi wamemuiba na haja fufuka.  Hakiki hilo jambo hapa, Matahyo 28:11-15.
Naguswa kukudokezea walau kidogo, 13 wakisema, “Semeni, ya kwamba wanafunzi wake walikuja usiku, wakamuiba, sisi tulipokuwa tumelala.” 15….Na neno hilo likaenea kati ya Wayahudi hadi leo.

Kwa hiyo wapo watu ambao hawataamini mujiza wako ulikwisha kuumbika rohoni milele na wengine ni wakina Tomaso hadi wa guse, pia usisahau kundi jingine lile la wale watu waliokuwa wakielekea Emau, walikuwa na Yesu ila hawakumtambua maana macho yao yalipofushwa kwa hiyo wengine wamepofushwa na subira punde Yesu akiumega mkate watafumbuliwa macho wala usiwabaguwe.
Na wewe achana na hiyo mitazamo bali amini hicho kilichokuwa kimekufa hivi sasa kimefufuka na Yesu kristo. Na wakikugasi wewe waambie ya kwamba wasimtafute aliye hai miongoni mwa wafu kwani amefufuka kama alivyosema.

Tumsikilize Malaika alivyotangaza Ushindi huu bila kipaza sauti wala spika ama chombo cha habari ila ulienea ulimwenguni mwote.
Mathayo 28:5 Malaika akajibu, akawaambia wale wanawake, “Msiogope ninyi! Kwa maana ninajua mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa. 6 Hayupo hapa: Kwani amefufuka kama alivyosema,  njooni mpatazame mahali alipolazwa.

Na kusihi endelea kusoma makala nyingine na hongera kwa Imani iliyokwisha jengeka ndani yako na kwa kupokea mujiza wako, Tafadhali utunze vyema.
    
  Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundila Fb, ili kuupta habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                       PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                              



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni