Ijumaa, 26 Mei 2017

NYAMAZENI NI VUKE.

Na Mwalimu Oscar Samba #Ug Ministry
Ayubu 13:13a Nyamazeni, niacheni, ili nipate kunena.) Hayo ni maneno ya Shujaa Ayubu aliyoyanena mbele ya adui zake. Na wewe leo ujumbe huu ni wa kwako kwani ninakutaka kutokutishwa ama kubabaishwa na maneno au mtazamo mbovu wa adui dhidi yako bali wewe mtazame Yesu aliyebingwa wakuwafunga vinywa kwa Utukufu atakao kutendea.

Adui zako walinena kila lilobaya vinywani mwao, huku wakimtuhumu ya kwamba ametenda dhambi.Ndio maana mabaya yanampata, tutizame sehemu ya maneno ya Elifazi.
Ayubu  4: 7 “Kumbuka, tafadhali: ni nani aliyeangamia akiwa hana hatia? Au hao waelekevu, walikatiliwa mbali wapi? 8Kama mimi nilivyoona, hao walimao maovu, na kupanda mathara, huvuna yayo hayo. 9 Kwa pumzi ya Mungu huangamia, na kwa kuvuma kwa hasira yake humalizika. ”

Ona tena kebei hii katika mstari wa 11; “Simba mzee huangamia kwa kukosa mawindo, nao watoto wa simba mke wametawanyika mbalimbali.”

Rafiki na ndugu yangu katika Bwana huenda upo katika majira ama nyakati au wakati kama huu ila yangu kauli ni hii; “Usitishwe na manongono hayo bali wewe waambiye ama watake wafumbe vinywa ili uvuke.”

Wakigoma wewe waache maana hata kwa Ayubu alifanya hivyo ila walikataa. Ukiweza kujitetea ni sawa ila usitumie muda mwingi kufanya hivyo bali wewe muache Bwana ajitukuze ndani yako na Falisafa yako iwe ni kuwataka wanyamaze ili uvuke. Ikiwa na maana ya kwamba majibu kamili watayapata mara baada ya wewe kuvuka na hapo ndipo watakapojua ya kwamba ulitenda dhambi ama ilikuwa ni Mungu anajivunia wewe.

Na hata kama umetenda dhambi kazi yao sio kukushutumu ama kukuteta bali ni kukuombea rehema kwani wanatakiwa kukumbuka ya kwamba mwenye haki wa Mungu huanguka mara saba na kuinuka tena.
Njia yakujisafisha sio njema kama ile ya kusafishwa na Mungu, Jionee jitiada za Ayubu zakujitakasa mbele yao;
Ayubu 21:7 “Mbona waovu wanaishi, na kuwa na wazee, naam, nakuongezeka kuwa na nguvu?  8 Kizazi chao kinadhibitika nao machani pao, na wazao wao mbele ya macho yao”

Hapo Ayubu anajaribu kujibu hoja zinazomshutumu kuwa ametenda dhambi ndio maana anapatwa na mabaya ila yeye anadhirisha kwamba wapo wasiomjua Mungu na bado mabaya hayawapati hapa ulimwenguni, na ukiendelea kusoma hiyo mistari utapata taswira halisia.

Lakini ashukuriwe na atukuwe Mungu Baba juu mbinguni na Duniani atendaye mambo makubwa kuliko hata yale tuyawazayo kwani ilifika majira ya Mungu yakuwafumba vinywa hawa adui zake. Tena kwa kitisho na kuwataka wakamuombe msamaha ama kupiga magoti mbele yake.

Ayubu 42:7.. Bwana akamwambia huyo Elifazi Mtemani, “Hasira yangu inawaka juu yangu, na hao rafiki zako wawili, kwa kuwa ninyi hamkunena yaliyo katika habari zangu, kama alivyo nena mtumishi wangu Ayubu.”

Hivyo ndivyo Bwana alivyo jidhiirisha kwa hao waliopaswa kunyamaza kimya ili Ayubu avuke salama. Na wewe yakupasa kuishika hii Falisafa ili kuwataka wanyamaze kimya na wakigoma wewe endelea kuwa mpole kwani majira ya wakina Elifazi yanakuja na Mungu atawataka kurejea kwako kama hao na hayo utayaona zaidi katika misitari inayoendelea.

Bwana wangu akupiganiye salama nami sina la ziada hadi wasaa huu ila ninakukumbusha kuwa somo la kesho linaitwa, BONDE LA KUKATA MANENO. Tafadhali usilikose kwani limesheheni ujumbe marithawa kuhusu mathara ya maneno na namna ya kupambana nayo. Mie ni Mwalimu wako Oscar Samba wa UG Ministry.

Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundila Fb, ili kuupta habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                       PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                              





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni