Ijumaa, 26 Mei 2017

SHINDA VIKWAZO TUKUTANE NG’AMBO YA YORIDANI.

  Na Mwalimu Oscar Samba #UgMinistry  
Maziwa na Asali, hayapatikani Misiri wala jangwani hakuna malisho yawezeshayo ng’ombe kutoa Maziwa ama maua ya mimea ili nyuki wazalishe Asali. Bali ukiyataka yakupasa Kufika Kanani kwani ndiko kwenye mizabibu na tini na zaituni zenye maua mazuri ya wezeshayo nyuki kutanda hapo na kisha kufwonza na hatimaye kuunda Asali.

Maziwa ama majani yatoayo maziwa hustawi kando ya mito na karibu na chemichemi za maji, na vitu hivyo hupatika kanani ambapo ndipo paitwapo; “NG’AMBO YA YORIDANI.”
Huku hawaingi, Waoga, Wasioamini ahadi za Mungu, yaani wasiochanganya ahadi za Mungu na imani, Wanung’unikaji, kwani hao hufa kwa nyama za kware kuwatokea puani; Hesabu 11. Ama kwa nyoka wa Moto; Hesabu 21.


Bali Mashujaa kama wakina Yoshua na Kalebu hao ndio waingiao, katika jiji hili la maraha. Hata leo ndivyo ilivyo kwetu siye kwani kama unataka kutimiza maono yako yakupaa kushinda vikwazo kama Yusufu ili kuishi maisha ya raha na mustarehe katika Kanani yako. Usifuraiye tu ahadi ya Maziwa na Asali bali tazama pia vikwazo ambavyo huna budi kuvishinda.

Embu tuangaliye walionshindwa na walioshinda katika safari hii ya kufika ng’ambo ya Yoridani. Manung,uniko yalifanyika kikwazo kikubwa sana kwa wana wa Waebrania. Na sababu ikiwa ni Chakula, chunga na wewe kulala njaa ama kula mlo mmoja mwaka mzima kusifanyike kikwazo kama hawa ndugu.
Hesabu, 11:5 Twakumbuka samaki tuliokula huko misiri bure,na yale matango, na matikiti, na mboga, na vitunguu,  na vitunguu saumu 6 Lakini sasa roho zetu zimekauka; hapana kitu chochote, hatuna kitu cha kutumaini isipokuwa hii mana tu.
Hesabu 11: 1-35, 33 Kisha hiyo nyama ilipokuwa ingali kati ya meno yao, hawajaitafuna bado, hasira za Bwana ziliwaka juu ya watu, Bwana akawapiga watu kwa pigo kuu mno.  Umeona hicho kikwazo kilivyo waangamiza?
Tutizame mfano mwingine, Hesabu 21: -4 Wakasafiri kutoka mlima wa Hori kwa njia ya Bahari ya Shamu, ili kuizunguka nchi ya Edomu ;watu wakafa Moyo kwa sababu ya ile Njia.  5 Watu wakamnung’unkia Mungu na Musa, “Mbona mmetupandisha huku kutoka nchi ya Misiri? Maana hapa hapana chakula wala hapana maji, na roho zetu zinakinai chakula hiki dhaifu.

Tuone matokeo yake, Mstari wa 6 Bwana akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma, watu wengi wakafa.

Lakini katikati ya hayo matatizo bado Mungu alitoa Rehema zake ambazo zilimuitaji aliye Hodari wa kushinda vikwazo ili aweze kupona. Ona tukio hili lililo na uajabu wenye ajabu.
Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti: hata ikiwa nyoka amemuuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya sahaba, akishi.Hesabu 21:9.
Ni walioshinda kikwazo hicho pekee ndio waliokutana na Bwana katika ng’ambo ya Mto Yordani. Na tuangaziwe mfano wa wakina Yoshua na Kelebu walivyo shinda kikwazo cha hofu dhidi ya majitu na kisha kufika ng’ambo ya Yordani salama.

Kumbuka hiki ni kisa cha wale wapelelezi kumi na wawili walioleta habari za nchi waliotumwa kuipeleleza ila kumi walileta mbaya huku wawili wakileta njema. Kwa kuwa watu wengi walikuwa waoga wakushinda vikwazo; walilazimika kuzipokea zile mbaya na hatimaye kukwama ila wajanja wanao ujua uzuri wa Ng’ambo ya Yordani ya kwamba ndimo mlimo Maziwa na Asali, walihakikisha wanashinda kikwazo hicho. Bila kukupotezea muda, pata Stori kamili kimaandiko.

Hesabu 13:31 Bali wale watu waliopanda naye wakasema,Hatuwezi kupanda tupigane na watu hawa, kwa maana wana nguvu kuliko sisi. 32Wakawaletea wana wa Iziraei habari mbaya za ile nchi waliyoipeleleza,  wakasema, “Ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi  inayowala watu wanayoikaa;  na watu wote tuliowaona ndani yake ni watu warefu mno 33 Kisha humo tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili;  tukajiona nafsi zetu kama mapanzi , nao ndivyo walivyo tuona sisi”

Kilichofwata ni hiki: Hesabu 14:4 "Na tuweke mtu mmoja awe akida , aturudishe Misiri.
Mbele yake katika sura ya 14 wanataka kuwapiga kwa mawe wakina Musa. Na Bwana anagadhabika na kuwaangamiza kwa hasira yake. Kuwa makini na tatizo kama hili la hofu lisikukwamishe kufika hatua ya kutaka kuacha wokovu. Kwani kutamani kurudi Misiri ni kutaka kuacha Wokovu, pia Usitake kumpiga Musa wako na mawe, kwani huku ni kulisengenya kanisa ama kumsema vibaya Mchungaji wako au wazee wa kanisa.Ukitenda hayo utakwama.
 (“Hesabu 14:10 Lakini Mkutano wote wakaamuru watu wote wapigwe kwa mawe”)

Tuwaangaliye walioshinda kikwazo hiki kama nilivyokujuza hapo awali:  Kelebu pasina hofu wala woga alinena haya:
Hesabu 13:30. Natupande mara, tukaitamalaki ;maana twaweza kushinda bila shaka” 
Wakati walioshindwa kuvuka vikwazo wanaona ni nchi ilayo watu walioshinda wanatamani kuiendea kwa haraka ili kuitamalaki.
Kwani ndani yao hawakuona majitu bali waliliona kusudi la Bwana likiwa hapo ng’ambo ya Yordani.
Hesabu 14:7 “Ni nchi njema mno ya ajabu.. 8 Ikiwa Bwana anatufuraia,atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali. ” ( Ona maziwa na Asali katika ng’ambo ya Yordani Mpendwa usione majitu)

Hayo ni maneno Mubashara yeye kutia moyo kutoka katika vinywa vya mashujaa Yoshua mwana wa Nuni na Kalebu mtoto wa Mzee Yefune.

Kwa Ujasiri Yoshua alisimama na kusema hili.
14:9 “Lakini msimwasi Bwana, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi,maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, Naye Bwana yu pamoja nasi;msiwaogope”

Kumbe Yoshua hapa anatufundisha jambo ya kwamba mtazamo ndio kikwazo, kwani walioshindwa walijiona kama mapanzi, na mithali husema aonavyo mtu nafsi mwake ndivyo alivyo. Ila hawa walioshinda kikazo waliwaona ni chakula wala wao sio kitoweo chao kwani hawakuwa na taswira ya kuliwa kama walivyonena walioshndwa ya kwamba ni nchi ilayo watu. Na walioshindwa wanaiona kama ni nchi watakayoila. Kisha mtazamo huo unapata nguvu kiimani kwa kubainisha kwamba MUNGU YU PAMOJA NAO. Kumbe anayeshindwa  huona kama Mungu hayupo pamoja naye. Ndio maana anakuwa mwepesi wa kulaumu mara michango mingi kanisani, Sadaka zimezidi, Mchungaji hana upako, mara Oh! Sikuizi hata uwepo haupo.

Yamkini Mpendwa mwenzangu kikwazo kikubwa ulicho nacho ni huyo mume/mkeo kugeuka teso kwako, tafadhali usiikimbiye ndoa kwani kufanya hivyo ni kuyaogopa majitu bali wewe Muombe Mungu naye atakuongoza chakufanya au kubadilisha kabisa na jambo hilo kubakia kuwa historia iliyosaulika.


Usikubali kuchelewa kwako kuolewa ama kupata mwenzi kufanyike kikwazo, badala yake mngoje Bwana kwa Saburi naye atakujibu, huyu Mungu aliyempa Ibrahimu Isaka akiwa na miaka mia moja na kumpa Hana mwana Samweli aliyedharauliwa na Penina atakukumbuka na wewe.

Haijalishi ugumu wa mazingira uliyo nayo, yamkini unaupata ujumbe huu ukiwa jela, mahabusu, ama wewe ni mfanyakazi wa ndani au maisha uliyo nayo ni magumu kiasi cha kukosa chakula ama kukosa kodi ya nyumba. Watoto huenda wamerudishwa ada, umesoma lakini huna kazi, au umefukuzwa kazi na uwenda biashara imekudodea; Kwani kila ukiuzacho hakitoki ama unauza ila hela au faida hauioni.

Skia Neno la Bwana: Mungu wetu hashindwe na jambo, wala mazingira hayo yasifanyike kikwazo kwako, aliyemtoa Yusufu gerezani na kumpa mujiza wa ajabu na wewe inawezekana hii leo. Hakika Mungu wetu sio mwanadamu hata ashindwe kufanya jambo ama aseme yaliyo ya uongo. Wewe hakikisha unasonga mbele na kuyatazama majitu kama chakula yaaani hizo changamoto kama mtaji wako huku ukiamini bila hizo hakuna kuinuliwa.

Ngoja ni kupe kisa hiki, Kijana mmoja aitwaye Daudi kijana wa mbari ya Mzee Yese alikuwa akienda siku moja kutembelea nduguze mjini na alikutana na kikwazo kikubwa sana maishani mwake ila hakukitazama hicho.

Unataka kukijua? Alikuwa ni mtu mkubwa na mzoefu kivita, Shujaa na pande la mtu, kwa kiluga cha leo tungali mwita; “Jitu la miraba minne.” Ila alilitazama kama ngazi ya kuinuliwa ama daraja la kufika ng’ambo ya Yoridani kwani bila Goliati Asingali pata alichokipata.

Alijitoa sadaka kama Shujaa asiyejulikana anayetafuta kujulikana, alipambana na kuhakikisha anampiga tena kwa jiwe la mkono, mara baada ya hapo kijana alipata ushindi mkubwa na kuuvuka mto Yordani huku akiiacha ng’ambo ya kunuka kinyesi cha Mbuzi ama kondoo, ya kupambana na simba na dubu na kunukia pafyumu ama marashi ya mazizini.

Unaonaje kama kijana huyu angemuogopa Goliati? Hakika asingefika ng’ambo hiyo ya heshima. Muhubiri mmoj akasema kuwa, “Usimuogope Goliati wako kwani ni Promosheni ya kuinuliwa.”
 Bila shaka wala takshishi ninakubaliana naye kwani mara baada ya ushindi huo wa mama walipita mji mzima wakimuimbia ya kwamba ameua makumi elufu huku aliyeogopa kuvuka ng’ambo hiyo akipewa elufu zake.


( Ona maziwa na Asali katika ng’ambo ya Yordani Mpendwa usione majitu yaani Wanefili na wana wa Anaki.)

Hongera kwa kuanza kuchukua hatua ya kukutana na Bwana katika ng’ambo ya Yordani kwani ni yangu imani kwamba hutatazama tena vikwazo kama vizuizi  bali vitafanyika kuwa daraja kwako.

Kama hujaokoka na unataka kuokoa ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundila Fb, ili kuupta habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                       PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                               




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni