Jumatatu, 29 Mei 2017

WANAFUNZI MLIOKOKA NISIKILIZENI.

Na Mwalimu Oscar Samba #Ug Ministry
Nina wasalimu katika jina lenye Uweza na Furaha ya hali ya juu la Bwana wetu Yesu Kisto, Leo nimeandaa ujumbe mahususi kwa ajili ya wanafunzi waliokoka katika ngazi zote za Elimu hususani vyuoni ila wazazi walimu, walezi na watumishi pia ni wahusika wa ujumbe huu ili kutimiza adhima hii.

Kusudi kuu la ujumbe huu, Ni kuwataka wanafunzi kutokuacha utayari wao wakumtumikia Mungu pindi waendapo ama wamalizapo vyuo.

Kuna tatizo kubwa sana linawakumba wanafunzi hawa nalo ni hili, Kabla ya kwenda vyuoni katika makanisa walipotokea walikuwa ni watumishi wa zuri sana ila baada ya kwenda wanaacha kumtumikia MUNGU.

Wengine wanajitaidi pindi wa wapo chuoni ila wakimaliza na kupata kazi huacha kabisa kufanya utumishi na baya zaidi wengine wana WITO na kusudi la Mungu kuwapeleka vyuoni ni ili wamtumikiye.

Kama watafanya utumishi baada ya kuhitimu, wengi ni wakati wanasubiria majibu aidha ya chuo, vyeti ama yale ya Kazi.
Inamsikitisha sana Mungu kuona jambo hili linatokea, kwani Utumishi wake haukusudiwi kufanywa tu na watu ambao hawajafika kiwango hicho cha Elimu bali hata wasomi wana Nafasi kubwa kwake kwani Paulo Mtume alikuwa Msomi na aliifanya kazi yake kwa umakini na weledi mkubwa .

Kinachotokea ni hiki, Wanapokuwapo chuoni uwanapoteza utayari wakumtumikia MUNGU, ambao huwakilishwa na viatu kwenye ulimwengu wa roho.
Tuone kwenye kitabu kile cha Wefeso;  WAEFESO 6: 15 NA KUFUNGIWA MIGUU UTAYARI TUUPATAO KWA INJILI YA AMANI.
Na sababu inayopelekea hayo ni kuweka kando Fikra za kutumia elimu yao ili kuujenga ufalume wa mbinguni badala yake huzijaza nafsi zao na fikra za kufanikiwa kimwili kwa elimu yao.
Jambo hili maandiko yamelizungumzia kwenye mfano wa Mpanzi na yanalifananisha na mbegu iliyodondoka kwenye miiba na kusongwa nayo, ambapo tafsiri yake ni mtu aliyesongwa na shuhuli nyingi na udanganyifu wa mali. Kwenye shuhuli nyingi ni hizo fikra na udanganyifu wa mali ni huo udanganyifu wa mafanikio ya kielimu.

Ukiwahitaji kumtumikia MUNGU huwa na kisingizio cha “ubize” ama ratiba ni nyingi, kumbuka jibu la huo mfano wa Mpanzi linasadifu majibu yao. Tuhakiki hilo jambo.
Mathayo 13:22 Naye aliyepandwa penye miiba, huyo ndiye alisikiaye lile neno; na shuhuli za dunia na udanganyifu wa mali hulisonga hilo neno, likawa halizai.

Rai yangu kwao ni kuwakumbusha jinsi MUNGU alivyowatoa mbali kipindi ambacho ada ilikuwa ikisumbua walivyomlilia kwa magoti, walipofukuzwa shule kwa kukosa karo za shule walivyoombolezana kuwaendea watumishi ila wakati huu imefika hatua ya kuwakwepa na wakipigiwa simu kuhusu changizo za huduma huzima hata simu ama huona wanasumbuliwa.
   Kumbuka ulipokosa msaada YESU alikupigania, kabla hujasoma ulivyokuwa na nia ya kuifanya kazi ya MUNGU tena kwa mzigo. Kumbuka siku ile ulipokuwa kwenye taabu kubwa kimaisha ulivyomuaidia Mungu kama atakutoa hapo kwa kumuwekea nadhiri ya jambo utakalolifanya kwenye utumishi wake.

Fanya hima sasa kumrejea yeye.
Ni kweli sio kila mtu ameitwa kuwa Mchungaji ama Mwalimu ila wapo walio waimbaji, wapiga vyombo, wanaodeki kanisani na cha ajabu wanaofanya usafi siku hizi sio wale wasomi wa chuo tena bali wasomi wameweka Elimu yao mpaka kwa MUNGU. Paulo alisoma ila alijishusha na Mungu kumuinua.

Mshahara wako utumiye kuifanya kazi yake, masomo ama kazi ikichukuwa muda mwingi ama kukupa ubize epeleke msalabani kwa maombi na sadaka maalumu ukimsihi MUNGU akupe hekima ya namna ya kumtumikia pia kukupa muda katika hiyo shuhuli.

Rudia enzi zile za maombi yako ya kufunga na kuomba, usiombe tu siku ukiwa na jaribu ama uliyokosa amani. Mungu akutiye nguvu pia #Share ujumbe huu na uweneze kwa wengine ikiwemo kwenye vikundi vya wanafunzi ili waliokoka wapone kiroho.

Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPLE, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigosple@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigosple.blogspot.com   #UkomboziGosple  #MwalimuOscarSamba
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundi la Fb, ili kupata habari hizi kwa haraka, zaidi. Ug Ukombozi Gosple,                                                                                       PAGE: https://www.facebook.com/Ug-Ukombozi-Gosple                                              
Pia kwenye mtando Mpya wakitanzania wa                                                                       2 DAY SKY: https://www.2daysky.com/home





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni