Jumatano, 3 Mei 2017

Nukuu iliyopo kwenye Kitabu cha Sadaka Kama Mbegu cha Mwalimu Oscar Samba

 "Ni jambo la hatari sana kufikia hatua ya kula Sadaka ambayo Mungu amekupa kama Mbegu na umejua fika kabisa alikupa kuitoa ila kwa sababu una hitaji fulani ukalazimika kuitumia. Nisikilize kwa ukaribu na utulivu: Maana hitaji na uhiitaji wa mwadamu hauishi, na Mungu anapotaka umtolee Sadaka kama Mbegu haimaanishi kuwa haioni shida yako, laa! Asha! Anaiona na amepanga kuitatua kwa kukupa njia ya upandaji.
Hivi kama una uhitaji wa mahindi kilogramu 30 na una mbegu ya mahindi kilo mbili. Itakufaidia nini kula mbegu hizo leo na kubakiwa na uhitaji wa kilogramu 28? Ni ya heri kuzifukia mbegu mchangani kama Yesu alivyosema kwenye Mariko 4:26-29. Na hatimaye kukupatia mavuno yatakayokidhi mahitaji yako.
Masikini wegi ni masikini kwa sababu walikwepa garama za kutoka katika umasikini. Na matajiri wengi ni matajiri kwa sababu walikuwa majasiri wa kuzikabili gharama za kutoka katika umasikini huku wakiwa wanajua faida za kuwa tajiri.
"

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni