Ijumaa, 30 Julai 2021

UPENDO WA MUNGU KWAKO NI WA MILELE, HAUFUNGWI NA MSIMU WALA MUDA

Na Mwalimu Oscar Samba

Ujumbe hu ni Sehemu ya Kitabu chetu cha MUNGU ANAKUPENDA. Kitabu kinachonuia kukusaidia kuliona pendo lake hata kama upo wakati mgumu, ukifahamu kuwa haupitii kwa sababu Mungu amekuacha, hakupendi ama amekukatataa.

Yeremia 31:3-7

Bwana alinitokea zamani, akisema, Naam nimekupenda kwa upendo wa milele, ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu.
 Mara ya pili nitakujenga, nawe utajengwa, Ee bikira wa Israeli mara ya pili utapambwa kwa matari yako, nawe utatokea katika michezo yao wanaofurahi. Mara ya pili utapanda mizabibu juu ya milima ya Samaria; wapanzi watapanda, nao watayafurahia matunda yake.
Maana kutakuwa siku moja, ambayo walinzi watalia juu ya vilima vya Efraimu, Inukeni, tukaende Sayuni, kwa Bwana, Mungu wetu.
Maana Bwana asema hivi, Mwimbieni Yakobo kwa furaha, mkampigie kelele mkuu wa mataifa, tangazeni, sifuni, mkaseme, Ee Bwana, uwaokoe watu wako, mabaki ya Israeli.

 

Jumatano, 21 Julai 2021

KAWIA UFIKE

 Na Mwalimu Oscar Samba

Ni kweli ngoja ngoja huumiza matumbo, au fahamu pia simba mwendapole ndie mla nyama! Maana mtaka yote kwapupa hukosa yote! Hawakuwahi kukosea waliosema kuwa subra yavuta heri!

 Ni hakika haraka haraka haina baraka! Maana hata waingereza ama wenye kingereza chao husema kuwa, njia ya kato siku zote ni njia isiyo sahihi.

 Kuna watu wengi wamjejikuta wakiingia hasara maishani mara baada ya kutaka mafanikio kwa haraka! Wamejikuta wakipoteza ama wakiharibikiwa kimaisha, ni kweli ni tajiri ila kapoteza mke na woto kwa sababu ya mashariti ya mganga! Ni kweli ana fedha sawa na elimu sawa ila ni muadhirika wa UKIMWI! Kapenda chipsi hatimae ni mjamzito na ndoto za kusoma zimakomea hapo!

 Ni heri ukawie lakini ufike uendako, kuliko kukimbia ukajikuta unakimbia hadi unasahau nyumbani ama unashindwa kuangalia taadhari ya alama za barabarani na hatimae ukaingia katika kusababisha ama kujisababishia ajali!

Narudia tena na tena kuwa kawia ufike, pole pole ndio mwendo! Unaonaje mkulima akapanda mbegu leo na kutaka kuvuna siku hiyo hiyo! Kama kwa mkulima haiwezekani uwe na uwakika kuwa na katika safari ya mafanikio ndivyo ilivyo.   

Embu tujionee jinsi maandiko mtakatifu ya Biblia yanavyotufunza katika kitabu kile cha Yakobo: 5:5 Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho.

8 Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia.9 Ndugu, msinung'unikiane, msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.

 

Jumamosi, 3 Julai 2021

Mwalimu Oscar Samba KUMFANANIA KRISTO Mkimbizi Iringa Ibada ya 1

Mwalimu Oscar Samba THAMANI YA KUMKABITHI MUNGU MAISHA YAKO YA BAADAE na...

Nilipata nafasi ya Kuwafundisha wanafunzi wahitimu wa Chuo Kikuu cha Mipango Dodoma CASFETA
Ujumbe huu utakusaidia uliye mwanafunzi na usie mwanafunzi kujua umuhimu wa kumshirikisha Mungu katika kila hatua muhimu ya maisha yako ikiwemo ile ya mawazo ama upangaji wa mipango

Jumatano, 24 Machi 2021

Ujumbe huu ni sehemu ya #kitabu chetu cha MTUMIKIE MUNGU, UKubali #Wito, #Kuna Faida katika Kumtumikia Mungu, na Kuna Hasara za Kukaidi Wito.

Na Mwalimu Oscar Samba

Usipoelewa jambo hili, huwezi elewa ni kwa nini Mungu aliamua kumfuata Yona baharini! Angeweza kuamuacha na kuinua mtu mwingine!

Anayefahamu swala hili kwa kina sio mwepesiwa kuimba ule wimbo wa “usifaye mchezo na Yesu na watu wengi! Wengine wanapanda na wengine anshuka!”
Japo ni kweli kabisa, ila kuna wakati mukutadha wake unagoma!
Hivi unajua ilimgharimu Mungu miaka mingapi kumuinu mbadala wa mfalme Sauli!
Ni rahisi sana kushangilia Mungu kumkataa Sauli! Ila fahamu iligharimu muda mrefu sana hadi kuja kutawala kwa mfalme Dudi!
Daudi hawezi kutawala kama muda hajaimarika, hajamaliza darasa la uongozi, hajafikia vigezo vya ufalme wa mbinguni.
Ndio maana hata baada ya Sauli mfalme kukataliwa na Mungu aliendelea kutawala hadi wakati ulipofika, na hata alipofariki bado Dauli hakuruhusiwa kutawala Israeli yote! Kwa hiyo bado kuna maeneo tena eneo kuba sana lilikuwa halina utawa ambao Mungu anautaka.

Jumamosi, 6 Machi 2021

Muombee Elia ama Yusufu wako, Ni Msaada wa kutoka kwenye Majanga kama ya Corona. #Corona #Covd19

 nA mWALIMU oSCAR sAMBA

Ujumbe huu ni sehemu ya #kitabu chetu cha MAMBO MUHIMU YA KUFANYA AU KUZINGATIA KUNAPOKUWA NA ADHABU YA KIUNGU INYOIJUMUISHA ENEO ULILOPO AU JAMII

18. Muombee Elia ama Yusufu wako; Kuna mtu MUNGU amemuweka ili kukuvusha ama kulivusha taifa na hata dunia kwa ujumla! shida kubwa ya wapendwa ni kwamba katika mambo kama haya kuomba kwa maarifa kumekuwa ni tatizo kubwa sana kwao! Wamisri walivushwa kutokana na akili, na hekima, pamoja na Roho wa Bwana ndani ya Yusufu kama Farao anavyokiri kwenye ile Mwanzo 41, kuwa hapana mtu mwenye akili, hekima na Roho wa Bwana ndani yake kama Yusufu! Ina maana gani! Kama Misri na dunia ya kipindi kile ilivushwa katika janga la njaa kutokana na sifa hizo zilizopelekea uwekaji wa akiba, basi na wewe muombee mtu ambaye mbingu zimemuandaa au kumtazamia kama sehemu ya majibu ya janga husika, kama ni la njaa, sawa, kama la kijografia pia sawa. Mfano kama ni la ugonjwa, ambao tena hauna dawa au kinga, waweza muombea Mungu ampe maarifa zaidi, na uwezo zaidi ama kuwaombea wanasayansi wapate maarifa zaidi ya kuwawezesha kugundua chanjo sahihi, na yenye uwezo stahiki, na isiyo na madhara katika mwili wa mwanadamu. Pili wagunduwe dawa, au tiba, huku ukiombea na viwanda vunavyotengeneza au vitakavyotengeneza dawa hizo, na vifa ambazo pia hutumika kipindi kama hiki, pamoja na kuwaombea madakitari na wauguzi ulinzi maalumu, maana nini kitatokea kama ukienda hosipitalini na kukuta madakitari na wauguzi wote hawapo ama wamaelemewa na wagonjwa kuiasi cha kushindwa kukusaidi na sababu ni baadhi yao kufariki!
Waombee pia wafadhili wataojitoa kwa fedha zao ili kuwezesha upatikana wa dawa hizo na vifaa pamoja na kuchangia gharama ili watu wengine wazipate, na huku sio kupungukiwa na imani bali ni kiroho kabisa. Kuweka akiba kwa Yusufu ni jambo la mwilini, na dawa pia ndivyo ilivyo, sayansi ni kiroho kabisa. Sasa tumekuwa na injili ambayo huiita injili makorokocho, kuwa hata chanjo ni pepo, hususani za ambao unaendeleao sasa, kuwani njama za watu wa mataifa fulani wanaotaka kutuua! Unafikiria mwenye fikra kama hizi ataombea sayansi isaidie kupembana na tatizo kweli! Maelekezo ya Paulo mtume kwa Timotheo kutumia mvinyo ilikuwa ni sayansi, maana kuna tiba hapo! (Sasa sina maana na kwako ufanye hivyo la!) Ila ninataka uione nafasi ya sayansi katika mambo kama haya! Tunajua kwa Yesu kumpaka mtu tope na kumtaka akanawe na Isaya kutumia makate wa tini ilikuwa ni ufuno sawa, ila sayansi nayo ni kiroho, waombee wafunuliwe dawa!

Jumamosi, 27 Februari 2021

Kitabu chetu cha: MAMBO MUHIMU YA KUFANYA AU KUZINGATIA KUNAPOKUWA NA ADHABU YA KIUNGU INYOIJUMUISHA ENEO ULILOPO AU JAMII.

Na Mwalimu Oscar Samba 

Neno Kiungu huwakilisha kutoka kwa Mungu au Shetani, ujumbe huu ni sehemu ya hiki kitabu chenye mada na pwenti kadhaa, ila hapa nimezicha,bua mbili tu; #Corona #Covd19 #Tsunam #Majanga  #Kimbunga #magonjwayamlipuko  #tanzania

1. Lifanye Eneo Unloishi kuwa Ghosheni yako. 2. Ijue na Uitumie Damu ya Yesu ya Pasaka; 3. Mulize Mungu kama Daudi; 4. Litengenezee Kusudi la Mungu Kisafina kama Musa, ama Nuhu; 5. Jifunze Jambo kwa Mke wa Lutu;

6. Sadaka kama Ulinzi; 7. Sadaka kama Sehemu ya Rehema, Mfano ile ya Daudi kipindi cha adhabu ya Tauni, 8. Taka Kujua pigo Hilo au Adhabu hiyo Inataka nini ili Ujisalimishe kwa Bwana, Mfano Rahabu, na Epuka kosa la Farao.

 9. Yajue na Uyaombe Maombi ya Musa ya Kulitengeneza Boma, 10. Mtafute na Umuondoe Akani, 11. Jitenge na Kusanyiko, au Kiunganishi cha Kusanyiko ama Waadhibiwa, ondoa jina lako kwenye watu wanaotakiwa kupewa hiyo Adhabu kwa Damu ya Yesu.

 

12. Tafuta Maelekezo Maalumu ya Mungu juu yako, kama Isaka dhidi ya Janga la Njaa na Wazazi wa Yesu. 13. Unapoisikia Hofu Usiipuzie, Taaka Kujua ni Aina gani ya Hofu ala Uikabili..

 

14. Tafuta Kukumbuka kama Mungu Aliwahi Kukujuza hapo Awali na Hukumsikia Vyema au Hukumbuki. (Amosi 3:7 Hakika Bwana MUNGU hatafanya neno lolote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.) Sijui sana ni kwa nini kanisa la leo lina uzito kwenye hili,  nijualo ni kwamba uwezo wa kusoma alama za nyakati, au majira umekuwa ni adimu sana kwa kizazi cha leo! Nafahamu kuwa hali ya kupuzia ndoto, kutokutambua jinsi Mungu anavyoongea, na mafundisho manyonge kuhusu uhusiano wetu na Roho Mtakatifu ni miongoni mwa sababu ambatanishi.

 

Kama kuna mahali Shetani amefanikiwa leo ni kuondoa, ama kuzimisha kama sio kufifisha karama ya unabii, na huduma ya nabii, pamoja na neno la maarifa!

 

Na anatumia njia kuu kama mbili hivi, moja ni kuhakikisha kanisa linapoteza imani na manabii au wanaotumiwa na karama hizi, kwa kujiwekekea manabii wa uongo, ili kuwakatisha watu tamaa na kuwafanya wa waone hata wale wa Mungu nao ni kama hao wengine!

Pili analitumia kanisa lenyewe, kwa kufikia hatua ya kupinga, na kukataa, na kuzimisha huduma na karama hizi, na sababu zao ni nyingi ila hazina hoja timilifu kibiblia, maana kama kuna wimbi la mafundisho na huduma potofu, suluhu bado sio kuzima na kukataa ile ya kweli, bali wafunze watu namna ya kutambua kweli na uongo. Mchele ukiwa na chuya, dawa sio kukataza nyumbani wasipike tena mchele bali ni kuwafunza kuzitoa, na kama ni mcahanga basi watake kuwa makini kuchambua maana mawe mengine ni yale meupe, kwa hiyo yanafanana kwa karibu na mchele, lakini pia kama ni vigumu, wafunze kupembua au kuuchambua wakati wanauosha na maji, njia ambayo ni salama zaidi.

 

Maharage yakiwa na mchanga au mawe, hayamwagwi, bali huchambuliwa! Na wewe ukiona dosari katika hudumka na karama hizi, hakikisha unazikabili!

 

Maandiki yako wazi kabisa katika biblia kuwa tunatakiwa kujifunza na kuhakikisha kuwa tunasoma alama za nyakati, au tunajua mabadiliko kwa kuzitambua dalili zake, mkulima asipojua kusoma uso wa nchi, hakika atakuwa akipitwa na maamuzi dhabiti katika majira husika, wakati wengine wanandaa mashamba yeye atashindwa kufanya hivyo, ama atajikuta akiwacheka wengine, maana kwa wengine ili walime ni hadi waone mvua imenyesha bila kujua kwa kufanya hivyo ni gharama zaidi maana aridhi husumbua kwani kulima kwenye tope ni kugumu zaidi! Pia ipo hatari ya kushindwa kufanya vyema maana kuna uwezekano wa kunyeshewa! Kuna kuchelewa pia kupanda, maana wakati wa kuotesha wewe ndo kwanza unakwatua udongo.

 Hosea hufananisha jambo la kuukwatua udongo sawa na kuomba, maana husema tumtafute Mungu, akitangulia na kututaka kuukwatua udongo wa mashamba yetu! Kiroho kuna vipindi kama hivi! Kuna kipindi cha kumtafuta Mungu kabla ya adahabu haijaja! Ukichelewa gharama yake ni kubwa sana! Unaweza kujikuta umeshapoteza ndugu wengi, ama hasara kubwa imeshatokea!

 Mama yangu wakati ugonjwa huu unaingia au umeanza kushamiri, ndipo aliponitaarifu kuhusu ndoto aliyowahi kuiota! Japo hakuwa ameielewa kipindi hicho! Ila nataka ufahamu kuwa Mungu alikuwa ameshaongea naye!

 Elimu na ufahamu wa kuzijua nyakati ni muhimu sana, na ni kiroho kabisa, jihakikishie kwa watu hawa, ambapo hata leo makanisani wapo, na kama hawajafungwa

Jumapili, 17 Januari 2021

kitabu cha UKULIE WOKOVU

#Habari-Njem ni kwamba, tumefanikiwa kutoa kitabu cha UKULIE WOKOVU, Kimetoka kwa njia ya PDF, tayari kwa ajili ya kusomwa kwenye simu na kompta, bei ni shilingi 5,000 za kitanzania; ukikihitaji wasilaina nasi kwa simu +255759859287, barua pepe: ukombozigospel@gmail.com pia zidi kutembelea: www.ukombozigospel.blogspot.com

 

Jumapili, 1 Novemba 2020

MATESO, MAPITO SIO ISHARA YA KUPUNGUA, KUFIFIA AU KUTOKUWEPO KWA PENDO LA KRITO PAMOJA NAWE.

Na Mwalimu Oscar Samba.

Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu chetu cha MUNGU ANAKUPENDA, chenye mukutadha wa kukujulisha hata katika taabu yako pendo lake lingali lipo hapo!

Wiki hii, (wakati mada hii inaandikwa) nilimuliza Mwalimu anayetufundisha kitabu cha Matendo ya Mitume swali gumu sana, ambalo lilisadifu ujumbe huu ambao ninauleta mbele yako siku ya leo!

Nilimuliza ama nalitaka kujua kuwa kweli ni Mungu huyu huyu liyejifunua kwa Stefano wakati anapiga mawe! Stefano anasema anamuona mwana wa Adamu au wa Mungu katika mkono wa kuume, tena tunaambiwa alikuwa amejaa Roho, kwa hiyo utatu mtakatifu ulikwepo ukimtazama au uwepo wake ulikwepo pamoja naye!

 

Jumapili, 11 Oktoba 2020

MAJIRA YA KULISIMAMISHA JUA. Ni semu ya Hiki kitabu

 Na Mwl Oscar Samba, 

Lengo: Kukujengea Kiu ya KuhakikihaMiujiza na Ishara na Matendo ya Mungu ya Ajabu Yanatendeka kwenye Huduma yajo kama Ilivyokuwa Kipindi ca Baba, na Mababu Zetu Kiimani.

Utangulizi

Mungu wa ma Mtendo ya Mitume ndie Mungu wetu! Wala hajawahi kubadilika, na jambo hili halitarajiwi wala kutazamiwa kuwa ipo siku itakuwa vivi, maana imenenwa hivi; Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele. Waebrania 13:8.

Ile ishara za Mungu hazijawa halisi kwako haina maana kwamba Mungu amebadilika, kaishiwa nguvu, ama amebadili utendaji na hata kufikiri kwamba ilikuwa ni kwa kipindi kile tu na kwa sasa haiwezekani, au inaonekana kwama Mungu hajaamua kufanya au kutenda kama hapo kale pia ni makosa tena mazito!

Jumapili, 27 Septemba 2020

MUNGU ANAKUPENDA KWA SABABU AMEANDAA MPANGO WA KUKUTOA KWENYE HILO JARIBU AU PITO.

Basi, Bwana ajua kuwaokoa watauwa na majaribu, na kuwaweka wasio haki katika hali ya adhabu hata siku ya hukumu. 2 Petro 2:9.

Wakati wana wa Israeli wanalia, wanalalamika, wanaumia ama wanaonyesha hisia zao kutokana na ugumu wa mateso yale ya nchi ya utumwa wa Misri, Mungu kwa upande mwingine alikuwa akitekeleza mipango ya kuwaokoa kwenye ile nchi!

Hakuna mtu aliyekuwa akiona, kutambua, au kufahamu kuwa upande wa pili Mungu alikuwa akimpatia Musa maelekezo ya namna ya kuwatoa kwenye ile ncchi!

Na hata kabla ya hapo, Mungu alikuwa akimuandaa Musa kwa ajili ya swala hilo, sio kwamba tu alilifanya hilo wakati Musa akiwa Midiani, bali hata kabla ya Musa kukimbilia huko Mungu alishamuandaa, ndio maana yale mahubiri yake kwenye kitabu kile cha Matendo ya Mitume yanaelelezea vyema kuwa Mungu alimuandaa huyu, ila hakumuelewa mapema, na wana wa Isreali hawakulielewa lile ndio maana walimkataa kwa wakati ule!

 

Jumamosi, 19 Septemba 2020

Kitabu cha USIFIE JANGWANI Mwalimu Oscar Samba Pdf

#Tangazo, Tunamshukuru Mungu kwa kufanikiwa kutoa kitabu hiki kwa njia ya Pdf, kwa hiyo kinaweza kusomwa kwenye Simu yako au Komputa, ukikihitaji utakipata kwa shilingi 50,000/ths. Tumia namba zifuatazo kufanya mawasiliano na malipo kwa M-Pesa, +255 (0) 756293767, jina ni Oscar Samba. Mwalimu Oscar Samba Tunajianda pia kukipeleka Amazon

 

Ijumaa, 28 Agosti 2020

Utangulizi wa Kitabu chetu cha UTUMISHI NA MTUMISHI

Mwalimu Oscar Samba

Luka 10:20 Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.
Ni kweli kabisa maandiko yanasema kuwa mtawatambua kwa matunda yao! Na mti mbaya au mwovu hauwezi kuzaa matunda mema, kwani tini huzaa tini wala zabibu haiwezi kuzaa michongoma, au kwa lugha nyingine huwezi kuchuma embe kwenye mti wa mchongoma au mchicha katika mbigili!
Lakini ukweli na uhalisia ni kwamba andiko hilo lina mukutadha wake na undani wake! Wengi wamekuwa wakiyatumia ili kuficha uhalisia wao bila kujua kuwa hawamdanganyi Mungu bali ni wanadamu wenzao, na hawa ni wale wasiojali sana hatima zao, yaani kwao maisha baada ya kufa sio kipaumbele chao kikuuu!
Kitabu hiki mpendwa kimebeba nia na kusudi la kuwasaidia watumishi, ili wasije kubweteka na utumishi walio nao, au wakifikiria kuwa utumishi ni tiketi au kibali cha kuwapeleka mbinguni, ni vyema kufahamu kuwa pasipo huo utakatifu haiwezekani kumuona Mungu!
Utumishi na Mtumishi maana yake ni kwamba hakuna uhusiano kati ya utumishi ulionao na wewe kumuona Mungu! Kuingia mbinguni kigezo kikubwa ni utakatifu au wokovu na sio jinsi gani unatumiwa na Mungu! Na kitabu hiki pia kitawasaidia wale watu ambao wanateseka na kuumia na kujiuliza maswali yasiyo na majibu kuwa inakuaje mtu anatumiwa na Mungu kwa ishara na miujuza, au kwa neno ambalo linawasaidia wengine na wengi kuokoka ama kufunguliwa lakini maisha yake mwenyewe binafsi ni machafu!
Sikatai kuwa kuna mapungufu, ambayo mtu huzidi kukamilishwa, au kuna kuanguka au kukosea kama Daudi alipolala na mke wa mtu, na kumua mumewe, au jinsi Musa na Haruni walivyokorofishana na Mungu, ama mapungufu kadha wa kadha ambayo pia tunayona kwa Petro!
Hapa ninanena habari za watu walioharibika mioyo kabisa, au ambao wapo katika kuharibika lakini kwa kuwa Mungu anajithiirisha kwao au kwa kuwa bado wamejaa Roho basi wanabweteka na hali hiyo, na kudhania kuwa Mungu hachukizwi na kosa au mwenendo wao!
Kuna muda utakatifu unaenda pamoja na utumishi! Ila kuna muda utumishi au mapenzi (kusudi maalumu) ya Mungu hutimizwa hata na chombo ambacho sio kisafi! Tutajionea kwa Balaamu, mtu mchawi aliyetumiwa kiunabii na kukamilisha makusudi ya Mungu, ila alikuwa mchawi na utumishi haukubadili maisha yake, lakini pia tutajionea kwa watu kama yule mganga wa kienyeji alivyo mpandisha Samweli nabii kutoka Ahera au kifuani mwa Ibrahimu, (Paradiso) lakini alikuwa ni mpunga pepe!
Nakutaka sana kuhakikisha kama kweli unataka kwenda mbingunbi basi unjitahidi kuulinda utakatifu! Na hii ilikuwa ni shabaha kubwa sana ya Paulo mtume, kuwa alilinda asije akawa wa kuwahubiria wengine na kisha yeye kuachwa! Nawe uwe makini, pepo kutoka sio kigezo cha wewe kuiona mbingu!
Ndio maaana furaha ya wanafunzi wa Yesu kuhusu ishara na ambao yaliyotokea haikuwa kipimo au kigezo chawao kuiona mbingu, bali furaha yao iliyopaswa kupimwa ni kwa kuwa majina yao yameandikwa mbinguni! Kuupata ulimwengu wote, kujaaa karama na kutenda miujiza hakuna faida kwako kama utapata hasara ya nafsi yako! Mathayo 16: Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake? 27 Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
Kilio chako kikubwa, na haja yako kubwa isiwe ni huduma yenye miujiza, ishara na umaarufu wa kiutumishi, bali utakatifu kwanza! Tafuta kumpendezesha Mungu kwanza!
Nayanena haya maana tumekuwa na watumishi ambao wapo tayari hata kutumia ushirikina ili tu wahakikishe wanapata nafasi fulani kwenye dini au dhehebu lake! Wapo ambao hutumia rushwa, na hata kampeni chafu ili tu kupata vyeo, wapo ambao hutumia hila wakifanya miujiza bandia ili tu wapate umaarufu na kadhalika!
Utakatifu kwanza, kisha vingine baadae! Tumekuwa na watumishi ambao hukandamiza vipawa au huduma za wengine kwa hofu ya kupinduliwa kiutumishi, na hata kuwatengenezea tuhuma au hila mabaya ili tu kuwachafua wengine kwa nia ya kulinda mkate!
Wapo ambao huhakikisha wanawaaribia wengine kwa lengo la kuchua nafasi walizo nazo! Wengine hutimia vibaya mahusioano yao na waangalizi, maaskofu au watu wenye dhamana husika ili kuwataka wamuondoshe ama wampe uhamisho mtumishi fulani kwa lengo la wao kukaa kwenye hiyo nafasi! Hii ni dhambi kama nyingine! Fahamu sana kuwa haki ni tabia ya Mungu, kutenda haki ni sehemu ya utakatifi!
Wapo viongozi ambao huonea wengine, wakikosewa au wakiona hawajatendewa sawa hata kama muhusika yupo sahihi basi kinachofuata ni wao kumuadhibu kwa kumuamisha au kumuondoa kwenbye vyeo fulani fulani! Huyu naye hatambua kwamba anapaswa kuhakikisha jina lake li mbinguni kwa kuwa mtu wa haki!
Mshirika! Kitabu hiki ni muhimu kwako pia! Maana unapaswa kuhakikisha kuwa unazingatia mambo ya adili au maadili ya kiroho kwanza na sio vinginevyo! Maana Yesu alisema kuwa napenda adili kwanza! Na katika Agano la Kale akasema anataka rehema kwanza! Kwa maana kwamba kuna vitu vya msingi ambavyo Mungu anavitazama, ili kukuhesabia haki!
Epuka sana mambo fulani fulani yakaonekana mema ila wewe ukakataliwa! Mungu alimkubali Habili, na sadaka yake, kwa hiyo angeweza kuikubali sadaka ya Habili, ila asimkubali Habili! Kwa Korinerio aliikubali sadaka yake/zake na kumkataa Korinerio! Kisha akahakikisha anamtuma Petro ili sasa sio sadaka tu zikubalike bali na kiroho cha Korinerio kikamilishwe! Sasa kwa Kornerio ilikuwa ni kesi tofauti! Kwako wewe uliyeijua kweli yote, ukiteleza/haribika hakika utakuwa kama Kaini, ambaye sadaka yake ilikuwa mbovu, ikakataliwa, na maisha yake yalikuwa mabaya pia nayo yakakataliwa! Sasa wewe usiishilie tu kuwa na sadaka njema, kuwa mfanya usafi mzuri kanisani, kumjali mchungaji wako na kusahau roho yako ! Ambapo hayo yatakubalika! Bali hakikisha na kiroho chako kipo vyema! Kwa hiyo kwa moyo mkunjufu ninakukaribisha humu kitabuni!
Kitabu kikitoka kitafute!
Hongera kwa kusoma ujumbe huu, nakutia moyo kuzidi kumtazama Mungu, na pia uwenda hujaokoka, yaani Yesu sio Bwana na mwokozi wa maisha yako! Nakutia moyo pia kuokoka sasa! Yamkini ni uchumi, fedha, hazipatikani, unazingirwa na nuksi na mikosi, kila unalofanya haliendi, unakabwa na mapepo, ! Wewe njoo kwa Yesu na hayo yote yatapita kabisa ! Sasa natumi u tayari!
Sema; MUNGU BABA, NINAKUPENDA, ASANTE KWA KUNIPENDA KWANZA, LEO NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NA NIPO TAYARI KUOKOOKA, TAFADHALI INGIA NDANI YANGU, SAMEHE DHAMBI ZANGU, NA FUTA JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKU, NA ULIANDIKE SASA KATIKA KITABU CHA UZIMA WA MILELE, Ameni.
Kwa kufanya hiyo umekwisha kuokoka sasa, na tafadhali tafuta kanisa la watu waliokoka lililopo karibu nawe ukasali, hapo, waambie kuwa umeokoa hivi karibuni, ili wakulee vyema kiroho.
Mawasiliano yetu, kwa M-Pesa au Simu: +255 759 859 287, barua pepe: ukombozigospel@gmail.com