Jumapili, 11 Oktoba 2020

MAJIRA YA KULISIMAMISHA JUA. Ni semu ya Hiki kitabu

 Na Mwl Oscar Samba, 

Lengo: Kukujengea Kiu ya KuhakikihaMiujiza na Ishara na Matendo ya Mungu ya Ajabu Yanatendeka kwenye Huduma yajo kama Ilivyokuwa Kipindi ca Baba, na Mababu Zetu Kiimani.

Utangulizi

Mungu wa ma Mtendo ya Mitume ndie Mungu wetu! Wala hajawahi kubadilika, na jambo hili halitarajiwi wala kutazamiwa kuwa ipo siku itakuwa vivi, maana imenenwa hivi; Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele. Waebrania 13:8.

Ile ishara za Mungu hazijawa halisi kwako haina maana kwamba Mungu amebadilika, kaishiwa nguvu, ama amebadili utendaji na hata kufikiri kwamba ilikuwa ni kwa kipindi kile tu na kwa sasa haiwezekani, au inaonekana kwama Mungu hajaamua kufanya au kutenda kama hapo kale pia ni makosa tena mazito!

Ni kwambie ukweli ni kwamba tatizo lipo kwetu! Yeye ni Yeye Yule, jana leo hata milele, habadiliki, fahamu sana kuwa kama mvua ina nyesha na wewe hujaloana usijaribu kugombana na mvua, ila utupe mwamvuli uliojifunikia, toka chini ya paa la nyumba linalokuzuilia, na kama upo chini ya mti wewe toka hapo maana unyeshewaji wako utakuwa tofauti n ambaye hajafunikwa na matawi au majani ya mti!

 

Wala usijaribu kufikiri kugombana na mti, au kung’o mti, ama kuezua paa la nyumba, ila wewe tafuta mlango ulipo na utoke! Usigombane na dini yako, wala dhehebu lako au Mchungaji wako ambaye haamini katika Roho Mtakatifu, dini au dehebu ama huduma ambayo inasema kwamba Roho alikujaga na hataka aje tena, ama waliojazwa na kutumiwa na Roho ni wale tu wa kansia la kwanza, ama wale wasemao kuwa utendaji wa Mungu wa kipindi kile sio kama wa leo! Hao usifanye nao vita, bali wewe jitenge kati yao na utafute kundi sahihi kwako, huu sio wa kati wa kukumbatia dini na kuacahana na wingu la utendaji wa kazi za Mungu.

 

Ninakwambia hivi kwa maana kwamba kitabu hiki hakijaja kwa bahati mbaya, na japo na hakijaja ili kukutenga na dini yako, ila kimekuja ili kukusaidia  kufuatana na wingu hili, Kifu Barthomayo, na yule wa Yohana 9, wote hawa walikuwa na dini zao, alikuwa dini ya Mafarisayo na yamkni pia Masaduayo, ila alipo au walipomuona Yesu anapita moja kwa moja walipaza sauti zao! Walitambua kuwa kuna wingu linapita ambalo lina mujiza wangu hawakukubali kamba ya dini iwazuilie, waliruka ukuta wa dini! Ninaamini hata mlangoni hawakutokea, yaani hawakwenda kuaga ka wakuu wao wa dini bali walichomoka! Unaju ukitaka kuwa huru, hutatafuta pa kutokea, maana ukigundua au hata hapa dirishani ninaweza kuchomaka, basi utachomoka! Maana hata Daudi aipokuwa akiwindwa na Sauli, mkewe Mika, alimtolea au alimuwezesha kutoroka kwa kuptia dirisha!

 

Yule wa Yohaa 9, Mafarisayo walinuka kweli kweli ili kupinga jambo hilo, ila hakukubali kukwamishwa nao, ndio maana alidiriki kufika mahali na kusema kuwa mimi sijui kama ni mwenye dhambi yaani Yesu, ila ninachojua ni kwamba nilikuwa sioni na sasa ninaona, ni kwa nini ninakujuza haya? Jambo la kutaka kuziona ishara za Mungu zinakuwa dhairi kwako ni vita! Na kama ni vita inakupasa ujue namna ya kukubaliana navyo, na uwe tayari! Dini isikuzuilie kumjua Mungu zaidi! Hata wakina Petro na wengine walikuwa na dini zao, ila walihakikisha wanalifuatilia au wanafuta wingu sahihi!

 

Kwani Yesu alimwambiaje Nathanaeli! Nathanaeli akamjibu, Rabi, wewe u Mwana wa Mungu, ndiwe Mfalme wa Israeli. Yesu akajibu, akamwambia, Kwa sababu nilikuambia, Nilikuona chini ya mtini, waamini? Utaona mambo makubwa kuliko haya. Ni Yhana 1:49-50.

 

Unaonaje kama angegoma kumfuata au angezembea, ama angeendelea kusema kama wengine wanavyosema leo kuwa nina dini yangu, hata huku kwetu tunamuamini Mungu! Hakika ambayo alikuja kuyashuhudia isingaliwezekana kwake!

Kumbe kuna vitu ambavyo huweza kutuzuilia kutenda ishara na miujiza! Ni kweli kabisa Mwalimu Oscar, natumai kuwa hilo ndilo jibu lako!

 

 

Unajua Paulo Mtume angeweza kuendelea kusema kuwa Yesu wewe unajua kuwa mimi nina dini yangu, na kuongezea kuwa hii dini ndiyo ile tuliyoachiwa na Musa, sisi ni watu wa Torati, kwa hiyo hata huku ninaweza kumtumikia Mungu, na kadhalika! Uwe na hakika yale aliyoyatend asingeweza kuyateda kabisa!

            Wala mimi sina lengo au nia ya kukutoa humo kwenye dini au kusanyiko lako kama nilivyokujuza hapo awali, ila nataka kukufikirisha kiupana zaidi kama dini, au kusanyiko lako ni kizuizi cha Mungu kutembea na wewe uwe na hakika kuwa ile kiu, na shahuku iliyo ndani yako haiwezi kamwe kutimia, Gideoni alikuwa na maswali kama yako, kuwa yupo wapi Mungu wa Baba zao, Yule ambaye amesikia matendo yake, na yamkini alipita kule ambako wana wa Reubeni, na Nusu ya Kabila ya Manase na wagadi walipoweka alama, madhabahu ambayo ilikua na nia ya kuja kuonyesha watoto au wajukuu au vizazi vijavyo kuwa yupo Mungu aliyewatoa utumwani na kuwafikisha hapo, kama Yoshua 22 isemavyo, lakini pia Yoshua aliweka alama ya mawe au nguzo ikiwa na maana kwamba uzao ujao ukiyaona au kuona wajue kuwa yupo Mungu, na maswali hayo yalikuwa magumu sana kwake!  Lakini fahamus sana kuwa, katika hali hiyo utendaji wa Mungu haukuwa umeisha nguvu zake!

 

 

 Na kuna mambo huyu Gideoni litatikana kuyatenda na alipoyatenda Mungu yule yule wa Baba zake ndipo alipokuja na kujidhiirisha, na wewe kuna mambo muhimu unatatikana kuyatenda ili kunufaika na utendaji wake kwenye huduma yako! Fahamu sana umuhimu wa kumfuata Yesu kama Nathanaeli! Ukikwama hapa, hakika utakwama na kwenye miujiza na ishara, haijalsihi dini yako inamtajaje Yesu, maana hata Torati ya Pauo ilimtaja, maana Yesu alitabiriwa katika Torati, Zaburi na Manabii ila haikumuwezesha Paulo kunufaia na alichobeba Yesu, na wewe maamuzi haya ni kwa ajili yako leo na huduma yako!

Tafathali kitabu kiitoka kitafut, pia tumeanza kuuza kwa njia ya

‘Soft Copy’ bathi ya vitabu vyetu.

 

Hongera kwa kusoma ujumbe huu, nakutia moyo kuzidi kumtazama Mungu, na pia uwenda hujaokoka, yaani Yesu sio Bwana na mwokozi wa maisha yako! Nakutia moyo tena kuokoka sasa! Yamkini ni uchumi, fedha, hazipatikani, unazingirwa na nuksi na mikosi, kila unalofanya haliendi, unakabwa na mapepo, ! Wewe njoo kwa Yesu na hayo yote yatapita kabisa ! Sasa natumi u tayari!

 

Sema; MUNGU BABA, NINAKUPENDA, ASANTE KWA KUNIPENDA KWANZA, LEO NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NA NIPO TAYARI KUOKOKA, TAFADHALI INGIA NDANI YANGU, SAMEHE DHAMBI ZANGU, NA FUTA JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKU, NA ULIANDIKE SASA KATIKA KITABU CHA UZIMA WA MILELE, Ameni.

 

Kwa kufanya hiyo umekwisha kuokoka sasa, na tafadhali tafuta kanisa la watu waliokoka lililopo karibu nawe ukasali, hapo, waambie kuwa umeokoa hivi karibuni, ili wakulee vyema kiroho.

 

Mawasiliano yetu, kwa M-Pesa au Simu: +255 759 859 287, barua pepe: ukombozigospel@gmail.com

pia temnbelea: www.ukombozigospel.blogspot.com . AU www.mwalimuoscarvitabu.blogspot.com

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni