Jumapili, 11 Januari 2026

#Muamshe Yesu Kwenye Maisha Yako*

Sikatai ya Kwamba Yesu Unaye, Nakubali Kabisa...

Ila Umemfanya Kukosa Chakukufanyia Kiasi cha Yeye Kutulia au Kunyamaza Kimya...

Ni sawa na wewe kualikwa ugenini alafu mwenyeji wako akawa anafanya kila kitu...hali hiyo inakufanya kukosa jambo la kufanya...

Na unajikuta umekaa mkao wa kusubiri kuambiwa walau nisaidia kukatakata mboga ama kufagia hapo nje...hii ikupe kuhakikisha unamfanya Yesu Kutokutulia katika Maisha Yako...

Siku moja wanafunzi wa Yesu wakapaswa kuvuka  kutoka ng'ambo moja na kuelekea Gerasi...katika boti Yesu hakupewa chakufanya...akalazimika kulala....walipokutwa na Dharuba Majini Ndipo Walijikuta Wakimuamsha....hapo ndipo alipoingia kazini na kuwasaidia....jifunze kitu hapo..

Jumamosi, 10 Januari 2026

Mfululizo wa 7, Katika Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UKIWA NJIA PANDA, Pointi ya 4.

Na _Mwl. Oscar Samba_ 

 4. Tafuta Ushauri Sahihi.

Hapo juu nimekupa mfano wa huyu baba ambaye alifikia mahali

pagumu sana kimaamuzi, ila mkewe alimshauri asimwache Mungu.

Badala yake waombe, nukuu moja wapo inamtaja au inamkariri huyu

baba akiwa anasema kuwa, Mungu amempa mke mzuri sana maana

alimshauri vyema!


Katika nyakati kama hizi ni muhim kujua umhimu wa namna ya

kukabiliana na shauri mbalimbali, maana wapo marafiki wataabishaji

ambao hawataacha kuja kwa nia ya kukuyumbisha kiushauri.

Kwenye fikra zako ni alzima kuwa na akiba ya hekima na maraifa ya

namna ya kukabilina na mamabo au amsuari au hali amahizi;

Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na

Jumanne, 23 Desemba 2025

Mfululizo wa 6 Katika Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UKIWA NJIA PANDA.

Mada ya 2 ya Mambo Mengine ya Kufanya au Kuepuka Ukiwa Njia Panda.

Na _Mwl. Oscar_ Samba 

Pointi  ya 3. Ingia kwenye Maombi ya Muda Mrefu. Yanaweza pia yasiwe 

ya muda mrefu, ila yakawa ya kina na mazito au yenye mzigo mzito. 

Lakini imizo la maombi ya muda mrefu sio la kupuuza, ni muhimu sana 

kulizingatia. Yanaweza kuwa ya siku tatu kavu, masaa 24, au ya wiki 

moja. Huweza kuwa katika mfumo wa masaa 12 au 24 kwa 24 ama 

masaa 36 na kadhalika. Ni kadri Roho wa Bwana atakavyo kuongoza.

Kuna baba mmoja alikuwa akipitia mahali pa gumu sana, aliingia ubia 

wa kibiashara na mtu ambapo ilimbidi aweke dhamana mali zake 

muhimu. Na Yule mtu baadae akajakukimbia na ile fedha; alifikia hatua 

ya kutaka kujiua. Maana ilikuwa ni fedha nyingi, mkewe alimshauri 

asijidhuru badala yake wa mgeukiye Bwana.

Jumatatu, 22 Desemba 2025

3⃣ SERA YA UFALME WA MBINGUNI KUHUSU UJENZI WA NYUMBA YA KUISHI KWA “RAIA” WAKE WALIOKO DUNIANI πŸ–Š Mwl.CHRISTOPHER MWAKASEGE.

Bwana Yesu asifiwe sana!

Masomo ya wiki mbili mfululizo zilizopita, juu ya Sera ya ufalme wa Mungu kuhusu ujenzi wa nyumba za kuishi, yamezaa maswali kadha kutoka kwa wasomaji.


Maswali hayo yalihusu kupata ufahamu zaidi, juu ya sera hii ya ufalme wa Mungu. Tumeyapokea hayo maswali, ingawa si rahisi tukayajibu yote, kwa sababu ya “ufinyu” wa nafasi ya kufanya hivyo.

Lakini kwa leo tunataka tujibu swali moja, kati ya maswali mengi yaliyoulizwa, – na tunaamini majibu hayo yataongeza ufahamu zaidi juu ya utekelezaji wa sera hii.

Swali lenyewe lenyewe liliulizwa hivi: “Je, unatushauri kuweka wakfu au kuitakasa ardhi kabla ya sijajenga?”

Majibu yake ni haya:

Kuna tofauti kati ya kutakasa kitu,

Alhamisi, 18 Desemba 2025

Mfululizo wa 1 wa Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UNAOOKUWA NJIA PANDA

Tunaanza na Utangulizi (kinapatikana Google Bure)

 Na Mwl. Oscar Samba

 Utangulizi

Kitabu hiki kimenuia kumsaidia mtu ambaye yupo katika mazingira

magumu ya kimaamuzi, na mbele yake kuna aina zaidi ya moja ya

maamuzi ambayo anahatarishwa kuyachukuwa au yanayomkabili,

inawezekana lililo hatari ni moja, au salama ni moja ila kuna zaidi ya

aina mbili au moja na kadhalika.

Kitabu hiki ni matokeo ya sehemu ninayopitia sasa kuhusu ndoa yangu.

Ikumbukwe sasa ni mwaka unaokaribia wa nane toka mwenzangu

tuoane na kujikuta ananiacha kwa talaka mahakamani hali inayonipa au

kunipelekea kuwa njia panda. Njia panda yangu inaweza isiwe na tija

sana kwako ila la muhimu ni wewe kufahamu mazingira ya kitabu

hiki ili kikusaidia. (Wakati nakitoa, imetimia miaka 10/11, “2015-

2015”.)

Unaweza usione umuhimu wake kwa leo ila nikuhakikishie kuwa

chakula hiki ni kama akiba, kuna muda tunakula leo lakini chakula

hicho kinatusaidia kesho; sio kwamba tuliingia kwenye mfungo la! Bali

homa ya ghafula imetukuta na kutunyima hamu au uwezo wa kula. Ila

kwa akiba ya jana ambayo hatukuwa hata na wazo la kula tumevuka leo

salama!

….Nikikuongezea ni kwamba, mara baada ya kuandika

utangulizi huu, na nikiwa tayari nimeshaanza kukiandika hiki

kitabu, njia panda nyingine ilijitokeza kama sio moja basi ni

zaidi, licha ya swala la ndoa, lakini pia limeibuka swala la

kusimamishwa masomo chuoni. Kumbuka nipo katika chuo cha

Biblia Dodoma cha CBC; mara baada ya kutofautiana na

kiongozi wangu mmoja wapo katika swala fulani, nilijikuta

nikipewa adhabu ya kusimamishwa masomo mwaka mmoja.

Nikiwa tu nimetoka kuchukuwa barua zangu, (ikiwa moja yangu na ya

mchungaji wangu kingozi,) ndipo nilipokutana na mchungaji mmoja wa

dhehebu jingine akiniambia kuwa nihamie kwake. Maana huku

kumekuwa kugumu kwangu na katoa sababu kadhaa: zingeweza

kuonekana ni zenye mashiko maana nyuma ya pazia jambo langu

limeonekana ni matokeo ya mimi kuwa na tabia ya kutetea na kudai haki. Pamoja na kusema ukweli pale ambapo ninapoona mambo

hayajaka sawa.

Wazo hili halikwepo kabisa kichwani mwangu, maana nilishapitia

mahali kama hapa mara baada ya uongozi wangu wa sehemu huko

Arusha kutofautina nami na kunichukulia mamuzi ambayo sikuyapenda

maana sikusikilizwa kimapana!

Jumanne, 11 Novemba 2025

Jifunze Kuidharau Aibu #mwalimuoscarsamba


 Kuna Mafanikio ili Uyafikie; Lazima Ujifunze Kuidharau Aibu.

By Mwalimu Oscar Samba

#nukuuyamwalimuoscarsamba MVUVI na Mvua

 


#nukuuyamwalimuoscarsamba KUMUA MAREHEMU



 

Ufunuo Dhidi ya UTAWALA

Mimina Kitasa yaani Pigo Juu ya Utawala, au Ufalme Usioutaka yaani Uliodhalimu...

Ufunuo wa Yohana 16:1 Nikasikia sauti kuu kutoka hekaluni, ikiwaambia wale malaika saba, Enendeni, mkavimimine vile vitasa saba vya ghadhabu ya Mungu juu ya nchi. 

10 Na huyo wa tano akakimimina kitasa chake juu ya kiti cha enzi cha yule mnyama; ufalme wake ukatiwa giza; wakatafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu.

Waombaji Wana nafasi Kubwa Sana ya Kuleta Mabadiliko Ktk Mifumo ya Uongozi Kwenye Maeneo Mbalimbali.

Heri Alitunzaye Vazi Lake

Uwokovu ni Vazi. Je, Unautunza Wokovu wako?

Nikuite Moyo hivi Leo kutokuendelea kucheza na Dhambi. Tunza wokovu, linda vazi lako. Yesu yu karibu kuja. Anakuja kulinyakuwa kanisa lake..

Ufunuo wa Yohana 22:13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho. 

14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake. 

15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya. 

Jumamosi, 18 Oktoba 2025

Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba, Ubaya na Uzuri Hautajwi kwa Wema wa Muda Fulani Daima wala Ubaya Wake.


 Kuna Kitu Kimoja Watu Wengi Wanakisahau; Sii Lazima Aliyekufanyia Wema: Awe Mwema kwa Kila Mtu. Alikadhalika Aliyekufanyia Ubaya Wewe Awe Mbaya kwa Kila Mtu. Na Aliyekutendea Wema Huo Awali, Sii Hakikisho la Yeye Kudumu Kuwa Mwema Kwako kila Wakati. 

(Tuepuke Kuwatetea Watu, Kwa Kuwa Kwetu Ni Wema, Nakuziba Masikio Pale Wanaoonewa Wakilia.) Tuepuke Pia Kulazimisha Wanaokuonea Kuonekana Wabaya Kwa kila Mtu. By Mwalimu Oscar Samba

Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba, Ushindi Dhidi ya Geteza la Ndoto Zetu


 Gereza Halikuzuia Mpango wa Mungu kwa Yusuphu, Badala Yake Liliurahisha.

Said Mwalimu Oscar Samba

Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba USHINDI DHIDI YA KABURI LA NDOTO


 

Jumanne, 29 Julai 2025

AKILI ZILIZO MACHO KATIKA UFALME WA MBINGUNI Mathayo 24:45

Ujumbee huu ni Sehemu ya Kitabu Chetu Kipya Cha: KILI ZILIZO MACHO KATIKA UFALME WA MBINGUNI

Mathayo 24:45

Na Mwalimu Oscar Samba 

Utangulizi
Kulala Usingizi, Kupoa kiroho, au Kifo cha Kiroho = Ni sawa sawa na:- (Hufananishwa na Hali ya Mtu Asiye na Akili ama Mwenye Tatizo hilo Katika Ulimwengu wa roho. 

Hiyo ni picha muhimu unayopaswa kuwa nayo, wakati huu unapoelekea kukisoma kitabu hiki. Ni muhimu sana kufahamu ya kuwa maana moja wapo ya Yesu ya kututaka tusilale usingizi yaani tuwe macho; ama tukeshe ililenga eneo la akili zetu.

Tazama mfano ule wa Wana Wali watano wenye Busara na watano Wapumbavu. Ndipo utakapotambua ya kuwa upumbavu unaotajwa pale, ni unaotokana na hali ya kutokujua ni nini cha kufanya katika nyakati kama hizi.

Malengo ya Kitabu:

1. Kuyafumbua Macho ya Aliyefumbwa, Kuziamsha Akili za Asinziaye ili Aweze Kuwa na Utayari wa Kutumika Kiusahihi (kama impasavyo), Katika Kulielekea Kusudi Aliloitiwa Kinyakati.

2. Kumpatia Ufahamu, Utakaotumika Vyema na Akili Zake, ili Kujua Ni Nini Kimpasacho Kukifanya Katika Majira Husika.

1 Mambo ya Nyakati 12:32 Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.

3. Kumjengea Fikra za Kumuwezesha Kuzitambua Hila za Adui Shetani; Katika Mpango wa Kumnyamazisha au Kutaka Kumpoozesha Kiroho na Kiutumishi, (au Kiutumishi/Kiroho.) 2 Wakorintho 2:11 Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikra zake.

4....


Lengo Kuu: Kukujengea Fikra za Kiuamsho, Ili Kuibua Hari na Kuamsha .... Kukuumbia Nia ya Kiuamsho Ndani Yako. (Penye Nia, Pana Utayari).

.....,....

1. Maonevu na Migogoro Katika Kanisa, Ama Baina ya Watumishi, au Washirika: Ni Ishara ya Kujisahau Kiroho. Watu waliopoteza kusudi, au kulisahau ama walioshindwa kujitambua ndio pekee huweza kuanza kuumana. Unapoona

Jumamosi, 19 Julai 2025

ROHO MTAKATIFU KAMA MSAADA, KATIKA GHARAMA ZA KULIPA ILI KULETA UAMSHO

 Na Mwl Oscar Samba

Matendo ya Mitume 1:8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi. 

 Lengo la Somo: 

Kukuwezesha, au Kukujengea Fikra za Kuhitaji Msaada Wa Roho Mtakatifu; Ili Awe Mwezeshaji Wako Mkuu, Katika Kulipa Gharama kwa Ajili ya Uamsho.

Taswira ya Ujumbe: Imejikita katika kufahamu umuhimu wa kumpata Roho Mtakatifu kipindi cha maandalizi ya kiroho kwa ajili ya uamsho. Hapa nilipo nalenga aina ya upako unao hitajika, ili kulipa gharama ya kuleta Uamsho. Ni sawa na kipindi kile cha mwanafunzi kusoma kabla ya kazi. Uamsho ni kipindi cha kazi, lakini kabla ya kazi kilipita kipindi aidha cha chuo au shule. 

Askari kabla ya kuingia vitani, au kuwa askari kuna kipindi cha mafunzo au cha maandalizi ya vita. Sasa kipindi hiki katika swala la Uamsho, ndicho hukiita kipindi cha kulipa gharama kwa ajili ya Uamsho. 

Kati ya eneo kubwa na muhimu watu wengi hawalijui wala kulizingatia, ni lile la maandalizi au la kulipa gharama. Mfano, Uamsho wa huduma ya Yesu, ulilipwa gharama na watu wengi. Akiwemo Yohana Mbatizaji, aliyekaa nyikani akila asali ya mwitu na nzige. Akivaa mavazi kama ya Elia, yaliyo ya ngozi na kadhalika. Maana huyu alikuwa ni mtangulizi.

Jumamosi, 5 Julai 2025

Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba, Kuishi na Watu Kwa Akili ili kumshinda Shetani

 


Shetani Hutumia Watu Ili Kufanya Vita na Wewe; Kwa Hiyo Ukifanikiwa Kuishi na Watu Kwa Akili: Ni Umemshinda Shetani Kwa Viwango Vikubwa.


By Mwalimu Oscar Samba