https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h
Jumatatu, 13 Januari 2025
Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba CHANGAMOTO DHIDI YA MTAZAMO WA ADUI NA MUHUSIKA
Nukuu ya Mwl Oscar Samba: Hekima Katika Majaribu au Changamoto za Kimaisha
Kuna Mlima wa Kuing'oa na Kuutupa Baharini, na Kuna Mlima wa Kuuzunguka Upite.
Tunza Hili Daima...sio Kila Tatizo Lazima Liondoke...Mengine Yakwepe.
By Mwalimu Oscar Samba
Alhamisi, 2 Januari 2025
Neno la Leo
Habakuki 3:19 YEHOVA, aliye BWANA, ni nguvu zangu, Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, Naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka .
Visti www.ukombozigospel.blogspot.com
Jumatano, 1 Januari 2025
Kalamu ya Historia na Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba
Kalamu ya Kuandika Historia, Ina Wino Mwingi Sana. Kwa Hiyo, Usigonge Kichwa cha Kalamu.
By Mwalimu Oscar Samba
Unapaswa Kuvumilia Hadi Wino Uishe. .. _Ukigonga Kichwa Itagoma Kuandika na Utajidanganya Wino Umeisha_ ....
For More Keep In Visiting
www.ukombozigospel.blogspot.com
Jumanne, 31 Desemba 2024
Mama Mchungaji: MUNGU AMEKUPA KIWANGO FULANI CHA BUSARA AU HEKIMA AMA AKILI.
B Mwl Oscar Samba
Ni sehemu ya Kitabu chetu cha NAFASI YA MAMA MCHUNGAJI; KATIKA HUDUMA YA MUMEWE. Kitabu kipo katika hatua ya mwisho.
10. Mungu Amekupa Kiwango Fulani cha Busara au Hekima ama Akili. Nachelea kusema kuliko mwanaume: maana hili pia utaliona kwa wenza wakiume ambao wake zao ni wachungaji. Na wao (wachungaji wa kike) wanapaswa kujifunza sana kuwaheshimu, kwa kutanguliwa na utambuzi wa nafasi za waume zao katika hili eneo la utumishi wao. Unatakiwa uijue hiyo nafasi ya umakamo kuwa huwa inaambatana na hekima au busara au akili za namna hii; ili uzitumie kutatua migogoro.
Mama mchungaji epuka sana kuwa mtu wa kukoleza chumvi inapofika swala la tatizo au mzozo fulani. Epuka pia tabia ya kutaka kuwa upande wa mumeo ili tu kupata kibali kwake, angali unajua yeye ana makosa, au uamuzi wake sio sahihi.
Msuluishaji yeyote yule lazima awe na tabia na maarifa ya kuwa katika mizani ya haki na usawa. Usitafute kupata kibali, tafuta kutatua mgogoro. Mke wa Hamani inaonekana alijua ukweli, alifahamu mumewe hayupo sahihi, lakini hakumuonya. Hadi mambo yalipoelekea mrama au kwenda kombo, ndipo alipomueleza wazi wazi; ya kwamba huyu Modekai uliyeanza kuanguka mbele yake....., hili ni kosa.
Mke wa Hamani laiti kama angejua mapema ya kuwa, anguko la Hamani mumewe, ni anguko lake; basi angalichukuwa taadhari mapema. Hamani alipotundikwa, na mkewe na watoto nao waliuawa, wakapokonywa na nyumba yao.
Una neema ya ajabu sana, itambue na uitumie vizuri (msisitizo upo katika kuitambua na kuitumia vizuri). Mama mchungaji wangu aliyenilea Arusha, siku moja alichungulia dafutari la mchungaji la matangazo, akaona tangazo la kuivunja kwaya. Alitumia hekima kuinusuru, alimuomba kuwa atazungumza nao. Na kweli alifanikisha jambo lile. Unaonaje kama angekoleza chumvi?
Jumatatu, 30 Desemba 2024
#BEBA MADHAIFU YA MUMEO; MFICHIE AIBU.
By Mwl Oscar Samba
Ni sehemu ya Ujumbe katika Kitabu cha #NAFASI YA MAMA MCHUNGAJI KATIKA HUDUMA YA MUMEWE
Kitabu kipo katika hatua za Mwisho. Na hapa ni katika pointi ya Beba Udhaifu wa Mumeo; Mfichie Aibu. Jukumu kubwa la nguo ni kuusitiri mwili. Hili ni jukumu la mwanzo na muhimu kuliko yote. Ni kweli nguo ina kazi nyingine kama vile ya urembo au kufanyika pambo, ila la kwanza kabisa ni kuufunika utupu. Aliyevaa nguo na ikaonyesha utupu, ni anajaribu kutuambia ya kuwa hajavaa nguo. Anapaswa kurudi katika Mwanzo sura ile ya tatu, ambapo Adamu na mkewe walipogundu waa uchi walilazimika kutafuta sitara.
Ambapo sitara hiyo ya vazi la majani haikuweza kukidhi hitaji, Mungu akawapatia vazi la ngozi. Sasa kama Mungu aliliondoa vazi ambalo bado lingeonyesha utupu na kuwapatia zuri zaidi. Uwe na hakika anayekataa zuri zaidi na kuvaa lenye kuonyesha utupu kuna shida kichwani; na shida hii itakuwa imeanzia moyoni. Huwa nasema hivi; nguo haina dhambi, ila nguo huwakilisha moyo wa dhambi au moyo mbovu.
Ijumaa, 20 Desemba 2024
Jumamosi, 30 Novemba 2024
Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba, Adui Wanaokuzunguka
Kuwa Makini, Unapozungukwa na Watu Waliobeba Tochi Inayomulika Ulipokanyaga (Wakitafuta Makosa); Na Sio Wakumulikie Ili Usikosee Kukanyaga.
By Mwalimu Oscar Samba
Jumatano, 13 Novemba 2024
Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba, Taa
Sii Kila Wakati Unahitaji Taa; Kuna Nyakati Unahitaji Macho Yenye Taa.
Jifunze kwa Wanyama Waonao Usiku!
Mwenye Taa, Akikimbia Nayo; Unabaki na Macho Yako: Usiku na Mchana Utaweza Kutembea.
UTOFAUTI KATI YA MSAADA NA SADAKA, na hata Mchango
*UTOFAUTI KATI YA MSAADA NA SADAKA*
Nimejibu swali la Mpendwa aliyetaka kujua huo utofauti
1.Msaada unatoa chochote....Sadaka Unatoa Ulichoguswa moyoni
2. Sadaka Unatoa ukiwa na Imani Kuna kitu nitapata kutoka kwa Mungu...Msaada unatoa ili kukidhi tu hitajio
3. Sadaka Unatoa kama kwa Bwana,....Msaada Unatoa kwa kumlenga muhusika
4. Sadaka Ukiitoa kwa Mazoea ina Adhabu kwa Mungu, Kuna kukataliwa kama Kaini au watu wa Kitabu cha Malaki moja na mbili...ila Msaada Sivyo
5. Baraka za Sadaka ni Kubwa kuliko Msaada.
6. Utoaji wa Sadaka Hukukutanisha na Mungu...Mfano Kornerio ktk Mtd. 10, na Mfalme Sulemani; 1 Wafalme 3. .....ila msaada utakutana tu na shukurani za wapokeaji...
NB: (a). Unaweza Kugeuza Msaada Kuwa Sadaka kwa Kuliombea jambo hili ili utoaji wako uwe na mguso wa Kiungu.
(b). Pia Kusikia Moyoni Mwako Roho Anakusukuma Kutoa nini?
(c) Toa Kwa Imani...yaani tarajia kitu kutoka kwa Mungu.
Muhimu : Kama ndivyo basi, likija changizo lolote, ikiwemo la harusi au kanisani...usiwe mwepesi kutoa kiwango kile kile kilichoainishwa au kuombwa kwenye kadi au kile cha desturi.
Badala yake tenga muda wa kutaka mapenzi ya Kiungu hapo. Sii vibaya ukavuka lengo lao au mazoea, kusikia kutoka moyoni na kutii ndiko kutakakobadili utoaji huo kutoka kwenye mchango au changizo la kawaida na kuwa Sadaka.
Maana Warumi 10:17 hutuambia imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huko huja kutokana na Neno la Kristo na neno ni Kristo Mwenyewe...na utoaji wa kiimani ndiyo huitwa Sadaka.
Ukichunguza kwa umakini ujumbe huu...utagundua ya kuwa hata makanisani muda ule wa sadaka wengi wetu hatutoi Sadaka bali ni kama msaada.
Tunatoa kwa sababu bila hivyo mchungaji ataishiwa chakula, tunatoa kwa sababu jirani yangu hapa atanionaje nimekuja kanisani bila Sadaka! Ama ninaona aibu wenzangu wote wamesimama kutoa na mimi sijatoa!
Tunachangia kwa sababu bila hivyo kengo halitajengwa...! Ni kweli ni wajibu...lakini badili wajibu kuwa Imani..
Ndiyo maana watu wengi ni wagumu kutoa kwenye ujenzi wa kanisa jingine, tena kama ni dhehebu tofauti basi ndipo huwa wagumu zaidi.
Sababu kubwa ni imani kukosekana katika hili. Moyo wowote wa utoaji, lazima daraja lake liwe ni imani. Licha ya imani kutarajia kutoka kwa Mungu...lakini kitu kimoja wapo kikubwa inafanya ni kuyataka mapenzi ya Mungu katika hilo jambo...Kumsikia Yeye na Kumtii.
Maandiko yanaposema kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, hunuia kutusaidia katika kusudio lililozaliwa na imani. Ndiposa anatukumbusha kuwa akitoa haba au kidogo atapata kidogo, na baraka zipo kwa anayetoa kwa moyo wa ukarimu...huu sio ukarimu wa kawaida ni ukarimu ambao ndani yake una nasaba za Kiungu....
Note : Kilio kikubwa cha kutoa sana na kutokuziona baraka...kinatokana na imani kutokuwa daraja la utoaji....utoaji ukiunganishwa na daraja la mazoea, msaada, changizo na hata lile la ninaona aibu wenzangu wanatoa mimi sijatoa; uwe na hakika baraka zake ni haba au hafifu.
Mungu anaposema atoaye haba atapata haba, ni makosa kulitazama hili andiko kwa kuangalia kiwango cha utoaji tu...Mungu hakuwa analenga tu kiwango cha utoaji...maana yule mwanamke alitoa kidogo kwa jinsi ya kipimo, ila kwa Mungu hakikuwa haba.
Imani ni kitu muhimu sana kinachopimwa hapo...utaiona kwa yule mwanamke wa kipindi cha Yesu, imani ilimsukuma kutoa vyote!
Huwezi kutoa vyote kama huna tarajio na humuamini aliyekutaka kutoa ya kwamba hatima ya maisha yako yote anayo yeye!
Ni rahisi kutoa ziada, au kumi ya 100 kati ya vile ulivyo navyo, maana una uhakika jioni asilimia 90 iliyosalia itakulisha, italipa yamkini na ada pia na hata rejesho la VICOBA!
Ila kutoa vyote, yaani asilimia 100 yote, ni imani kubwa sana maana umemuachia Mungu chakula cha jioni, ada na rejesho.
Sikuimizi kufanya hivyo!
Maana pia kama hujasikia kutoka moyoni bado itakuwa sio imani ni msisimko!
Na hapa ndipo wengi wanakwama...wanatoa kwa msisimko na wanashangaa hawajapokea hadi leo!
Imani lazima izaliwe katika kusikia ndani!
Tatizo wengine ni viziwi wa kiroho, masikio yao kwenye utoaji yamezibwa...hata Roho Mtakatifu akisema hawasikii....unapaswa kutatua hili tatizo...
Jumamosi, 2 Novemba 2024
Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba, Wokovu, Maisha, Usikate Tamaa, Usivunjike Moyo, Jipe Moyo
Maisha ya Wokovu: Kuna Wakati Hata Kama Huoni mbele; Muamini Aliyekutangulia, yaani Kristo. Kwa hiyo usitumie Nguvu Nyingi Sana Kutazama Mbele, Bali Tazama Alipokanyaga ili Na Wewe Ukanyage.
By Mwalimu Oscar Samba
Ijumaa, 18 Oktoba 2024
Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba Kuhusu Kipimo na Ubora wa Kiakili au Kufikiri kwa Watu au Vijana Wengi.
Kuna Watu Ukiwaambia "Mimi ni Big Brain," Watakuuliza "Do You Have Any Article?" Na Wengine Watakutazama Umevaaje!
#Vijana Wengi Wameamua Kuwa Kundi la Pili.
By Mwalimu Oscar Samba
Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba, Maono, Uongozi, Ushindi, Kushindwa
Tatizo Kubwa la Viongozi wa Kiafrika Sio Kukosa Maono; Ni Kushindwa Kupandikiza Maono Kwa Watu Wanaowaongoza. Hawajui Hakuna Mkuu wa Jeshi Anayeshinda Vita Kutokana na Uwezo Wake Binafsi tu; Bali ni Kwa Sababu Amefanikiwa Kuandaa Jeshi Zuri. Ubora wa Kocha Unapimwa Kutokana na Uwezo Wake wa Kuandaa Timu Nzuri.
Ukifeli Kuwafanya Wafikiri Kama Wewe, Uwe na Hakika Watafikiri Kama Wao; Na Watatenda Kiholela.
By Mwalimu Oscar Samba
Ukishindwa Kulea, Ni Umeshindwa Kurithisha; Kwa Hiyo Jiandae Kusahaulika."
Gharama Moja Wapo ya Kulea Ni Kuvumilia, Kujifunza Kumchukulia na Kuchukuliana Huku Ukisalia Katika Lengo na Kusudi la Kutaka Chombo Unachokitaka.
Ni Hatari Kuhitaji Mtu Unayemtaka Awe Unayemtaka Kwa Dakika Moja. Jifunze kwa Fundi Muwashi au Mfinyazi wa Vyungu, Tazama Inavyochukuwa Muda Kukipata Anachokitaka!
Ghrama Kubwa ya Kulea Ipo Kwako Wewe na Sio kwa Anayelelewa; Ustaimilivu na Hekima Vitakusaidia.
Paulo Mtume Hakaanguka Juu ya Mti, Hakujilea...Alilelewa...Wakati Hanania Anasema ni Muuaji, Mungu Alimuona Kuwa Chombo Kiteule..
Unahitaji Jicho la Tatu ili Uweze Kuondokana na la Pili Linalomuona Sauli Muuaji; La Tatu Litamuona Chombo Kiteule.
John Marko Alionekana Hafai, Barnaba Alimuona Anafaa Katika Kipindi Ambacho Alikuwa Hafai.
Ni Muhimu Pia Kuwaheshimu Waliokuona Unafaa Katika Majira ya Ulipokuwa Hufai; Maana Sasa Kila Mtu Anakuona Unafaa kwa Saabu Unawafa; Fahamu Yupo Aliyelipa Gharama.
Ni Kweli Utukufu ni kwa Mungu. Lakini Kumbuka Alimtumia Barnaba Kumuandaa Sauli Aliye Paulo na John Marko.
NB: Tatizo la Sasa sio Wakina John Marko na Wakina Paulo Wanaotufaa Katika Utumishi; Ila Tatizo ni Kukosekana kwa Walezi Wenye Fikra za Ukocha...Walezi Wengi Wana Fikra za Ushindi, Yaani Wamtumie Nani ili Wafanikiwe na Sio Wamuandae Nani ili Wafanikishe Malengo yao. Asante:
"Ukishindwa Kulea, Ni Umeshindwa Kurithisha; Kwa Hiyo Jiandae Kusahaulika."
By Mwalimu Oscar Samba
www.ukombozigospel.blogspot.com
Alhamisi, 18 Julai 2024
MAFANIKIO KWA KANISA LA KWANZA
Nina *Mshukuru Mungu* kwa Kufanikiwa Kukamilisha Kitabu Changu Kipya cha Uchambuzi wa Kitabu cha Matendo ya Mitume. Kitabu kinaitwa SIRI YA *MAFANIKIO KWA KANISA LA KWANZA* ( *kanisa la Mitendo ya Mitume) By Mwl Oscar Prospa Samba mwana wa Flora Samba
Kipakiwe Bure Kitabu hiki Free Download Pdf
Bonyeza Hapa Mwalimu Oscar Samba SIRI YA MAFANIKIO KWA KANISA LA KWANZA (Kanisa la Matendo ya Mitume)
Jumatatu, 12 Februari 2024
Ni Sehemu ya Kitabu Chetu Tarajiwa cha IMANI SAHIHI, Katika Mada ya Misingi na Tabia za Imani Sahihi.
Mwalimu Oscar:Mwl OSCAR SAMBA ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu: #Usiogope
Lengo la kitabu hiki ni kukuwezesha kuijua au kuitambua imani ya kweli, na kuzifahamu hila za adui Shetani katika imani potofu; ikiwemo namna ya kuzitofautisha na ile ya kweli na jinsi ya kuzishinda.
Misingi na Tabia za Imani Sahihi
Maana ya Imani. Katika Biblia na hata maisha yetu ya kawaida, neno imani limegawanyika katika maana zaidi ya moja, na huweza kuwa na maana kuu mbili. Mosi ni ile imani kama kuwa na hakika ya jambo unalolitarajia ambalo bado hujalipata ama kuliona ila unamatumaini nalo. Waebrania 11:1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.
Unganisha na hili andiko; Warumi 8:24 Kwa maana tuliokolewa kwa taraja; lakini kitu kilichotarajiwa kikionekana, hakuna taraja tena. Kwa maana ni nani anayekitarajia kile akionacho?
Maana ya Pili ya Neno Imani: Ni mfumo au "settings" ya mambo muhimu yenye kunuia kuunda aina fulani ya njia ya mtu; kimtazamo, fikra na hatimaye kimatendo, (kiimani "faith:") yenye kufuma namna ya kuabudu kwake, kusali, miiko fulani na maadili muhimu ya kuishi hapa














