Tusipoishi Tunayo Yahubiri; Kuna Siku Tutaishi Tunayo Yatenda.
Zaidi Endelea Kutembelea www.ukombozigospel.blogspot.com
Zaidi Endelea Kutembelea www.ukombozigospel.blogspot.com
"Ubarikiwe sana mwalim Oscar Samba, kwa kitabu hiki, kimenitia moyo sana kwa hali ninayopitia saiv chuoni, Siku sita nyuma nimekuwa mtu wa kuchoka, kuwa na mawazo mengi na kuhuzunika sana na kukata tamaa, nimekosa amani kulingana na Nafsi niliyonayo katika huduma ya Yesu kristo. Ila jana usiku roho inalisii na kunisisitiza kusoma kitabu hiki, nimekisoma hadi sa nane usk asubuhi nimekimaliza, kweli Mungu akubariki kwa huduma hii, niliwaza hadi kuachia nafasi niliyonayo ya huduma ili nipambane na masomo, ila najikuta nina nguvu za kusimama kuwaongoza tena watu ambao Mungu amenipa kuwaongoza, nimengi sana ya kusema Ahsante sana Mungu kwa neema ya kunikutanisha na Mwalimu Oscar Samba, Mungu akubariki na kukuinua kwa kazi hii.
Tuzidi kuombeana
Kesho yangu ni bora kuliko leo yangu, sitakubari kuzimia Moyo, Licha ya changamoto ninazopitia"
Ukikihitaji Kitabu Niandikie Ujumbe huu Wasapu +255759859287
Haijalishi Unapitia Mahali Pagumu Kiasi Gani, Huna Budi Kuhakikisha ya Kwamba Unaamua Kuokoka
Wokovu Utampa Yesu Nafasi ya Kuyapigania Maisha yako...Anasema Hata Kutupa Kamwe....Hili Ni Andiko la Ajabu Kabisa Katika Biblia.
Ujumbe huu ni Sehemu ya Toleo la Pili la Kitabu Chetu cha NAFASI YA MAMA MCHUNGAJI; KATIKA HUDUMA YA MUMEWE.
Kwenye Pointi ya . Ishinde Hofu ya Kesho Kimkakati, (Maisha Baada ya Huduma au Uwepo wa Mume Wako). Kuna maisha baada au nje ya wito ama Utumishi. Umri ni kigezo muhimu cha kuweza kuwaondoa katika utumishi wa madhabahuni. Kifo pia ni njia ya jambo hili.
Ni kweli kabisa kumekwepo na maisha magumu, na hata manyanyaso mara baada ya mchungaji kufariki, kuondoshwa katika utumishi ama kustaafu. Mke na watoto au familia hujikuta wakiwa katika maisha yasiyo mepesi. Machozi ya uchungu na huzuni uwaandama. Malalmo na majeraha huwa sehemu ya maisha yao.
Hali hii imepelekea hofu kubwa katika nyumba nyingi za kitumishi. Watoto kwa mama wachungaji wamejikuta wakizungukwa na tatizo hili. Na hii
Follow the Mwalimu Oscar Samba Mafundisho Ya Neno La Mungu channel on WhatsApp: https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h
Na Mwalimu Oscar Samba
Katika hii pointi ya Chunga Mnasema Nini Mbele ya Familia, Uzao Wako, Washirika au Kanisa Kuhusu Dhehebu, Viongozi Wako wa Kiroho Dhidi ya Wito Wenu au Utumishi.
Unachopanda Kinaota. Linda Sana Unapanda nini katika fikra na mioyo yao. Watoto ndio kanisa la sasa na kesho. Washirika ndio watumishi wanaoandaliwa. Unaandaa watumishi wa aina gani?
Kumbuka, Upandacho Ndicho Uvunacho. Au Upandacho, Ndicho Tuvunacho!
Iwe ni wewe au mmeo, ama mtumishi mwingine katika madhabahu mliyopewa na Bwana, huna budi kuhakikisha udhaifu huo unaondoka miongoni mwenu. Mbegu nyingi za uasi zinapandwa mioyoni mwa washirika, au watoto kama sehemu ya manung'uniko kutoka kwa wazazi au watumishi wao. Wataponda dhehebu lao, watachambua kila madhaifu, lakini wao hawatoki; wanakuja kushangaa baadae wana watoto au washirika wasiopenda dhehbu la wazazi wao! Wanaanza kutafuta na kujaribu kuwarudisha bila mafanikio!
Hakuna sehemu isiyokuwa na madhaifu, hakuna viongozi waliokamilika. Sema tu, unafanya nini kukabiliana na hayo madhaifu ya wengine hapo ndipo swali lilipo. Malalamiko ya kwamba katika dini hii mchungaji binafsi huwezi kuendelea, michango ni mingi, mara mimi mchungaji nikifa leo mke wangu hatathaminiwa, ni miongoni mwa mambo ya kulinda sana. Mioyo ya watoto huumia wanaposhirikishwa maumivu ya wazazi, na tena huumia zaidi. Wanaanza kukua na "mentality" ya kwamba dini hii inawanyanyasa wazazi wangu. Fikra hizi zinakuja kuamia kwenye mioyo yao.
Machozi unayolizwa na viongozi yalilie bafuni, ili ukimaliza kulia maji unayoogea yaweze kuyasafirisha machozi yote; na lisisalie hata moja. Daudi hakuruhusu ubaya wa Sauli mfalme kuendelea kwenye moyo wa Sulemani mwanaye. Lazima hekima ya namna hii tuwe nayo. Ni hatari tukampa adui Shetani nafasi ya kutufanya kuandaa kizazi chenye "elements" au chembechembe za uasi ndani yake. Na uasi unaotokana na maumivu ni mbaya sana. Magumu unayoyapitia mengine umeandikiwa na Mungu ili baadae ukijakuwa kiongozi uweze kuja kuwa mtu sahihi kwa watu wako.
Nimeshuhudia mtoto wa mchungaji mmoja toka akiwa shule ya msingi na kisha sekondari akijisemea ya kuwa: siku nikiwa mkubwa sitafungua kanisa TAG, Kisa maneno ya malalamiko kutoka kwa wazazi wake. Wenzangu niliokuwa nao wengi walihama dini, kisa mbegu kama hizi. Baadae wanakuja kugundua ya kuwa walifanya maamuzi yasiyo sahihi!
Chunga sana, unalalamika nini kuhusu dhehebu, viongozi wako wa kidini, au utumishi ulio nao mbele ya watoto, uzao wako, mwenza wako na hata kanisa kwa ujumla! Kile unachokifanya kinapandwa ndani yao kama mbegu. Kuotesha mchongoma ni kazi ndogo sana, ila kuung'oa ni kubwa mno.
Baya zaidi, wengine wanachambua madhaifu kama haya, hata mbele ya watumishi ambao wapo chini yao, au ambao tayari anawaanda kabisa kuwa watumishi. Hili ni tatizo kubwa sana. Ni sawa na kubandua vipande vya boti vilivyowekwa kwenye nyufa au maungio ya mbao ya boti mliyoipanda.
Muungwana hutafuta na gundi ili kuziba vizuri kwa nia ya kupaimarisha zaidi. Ni lazima fikra zetu zifikie mahali pa kukua na kukomaa vizuri kabisa katika hili.
Kitabu Kikitoka Kitafute:
Mawasiliano:
Tutembele ama Wasiliana Nasi
http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Tumeunda Channel ya WhatApp, Tufolo;
https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287, Email: ukombozigospel@gmail.com
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook:
https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbW
KwL
Tuandikie pia Maoni Yako; mwalimuoscarvitabu@gmail.com
Usiongeze, Wala Kupunguza Wino Kwenye Kalamu ya Historia ya Maisha Yako. Uliopo Unatosha.
By Mwalimu Oscar Samba
https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h
Tunza Hili Daima...sio Kila Tatizo Lazima Liondoke...Mengine Yakwepe.
By Mwalimu Oscar Samba
Habakuki 3:19 YEHOVA, aliye BWANA, ni nguvu zangu, Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, Naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka .
Visti www.ukombozigospel.blogspot.com
Kalamu ya Kuandika Historia, Ina Wino Mwingi Sana. Kwa Hiyo, Usigonge Kichwa cha Kalamu.
By Mwalimu Oscar Samba
Unapaswa Kuvumilia Hadi Wino Uishe. .. _Ukigonga Kichwa Itagoma Kuandika na Utajidanganya Wino Umeisha_ ....
For More Keep In Visiting
www.ukombozigospel.blogspot.com
B Mwl Oscar Samba
Ni sehemu ya Kitabu chetu cha NAFASI YA MAMA MCHUNGAJI; KATIKA HUDUMA YA MUMEWE. Kitabu kipo katika hatua ya mwisho.
10. Mungu Amekupa Kiwango Fulani cha Busara au Hekima ama Akili. Nachelea kusema kuliko mwanaume: maana hili pia utaliona kwa wenza wakiume ambao wake zao ni wachungaji. Na wao (wachungaji wa kike) wanapaswa kujifunza sana kuwaheshimu, kwa kutanguliwa na utambuzi wa nafasi za waume zao katika hili eneo la utumishi wao. Unatakiwa uijue hiyo nafasi ya umakamo kuwa huwa inaambatana na hekima au busara au akili za namna hii; ili uzitumie kutatua migogoro.
Mama mchungaji epuka sana kuwa mtu wa kukoleza chumvi inapofika swala la tatizo au mzozo fulani. Epuka pia tabia ya kutaka kuwa upande wa mumeo ili tu kupata kibali kwake, angali unajua yeye ana makosa, au uamuzi wake sio sahihi.
Msuluishaji yeyote yule lazima awe na tabia na maarifa ya kuwa katika mizani ya haki na usawa. Usitafute kupata kibali, tafuta kutatua mgogoro. Mke wa Hamani inaonekana alijua ukweli, alifahamu mumewe hayupo sahihi, lakini hakumuonya. Hadi mambo yalipoelekea mrama au kwenda kombo, ndipo alipomueleza wazi wazi; ya kwamba huyu Modekai uliyeanza kuanguka mbele yake....., hili ni kosa.
Mke wa Hamani laiti kama angejua mapema ya kuwa, anguko la Hamani mumewe, ni anguko lake; basi angalichukuwa taadhari mapema. Hamani alipotundikwa, na mkewe na watoto nao waliuawa, wakapokonywa na nyumba yao.
Una neema ya ajabu sana, itambue na uitumie vizuri (msisitizo upo katika kuitambua na kuitumia vizuri). Mama mchungaji wangu aliyenilea Arusha, siku moja alichungulia dafutari la mchungaji la matangazo, akaona tangazo la kuivunja kwaya. Alitumia hekima kuinusuru, alimuomba kuwa atazungumza nao. Na kweli alifanikisha jambo lile. Unaonaje kama angekoleza chumvi?
By Mwl Oscar Samba
Ni sehemu ya Ujumbe katika Kitabu cha #NAFASI YA MAMA MCHUNGAJI KATIKA HUDUMA YA MUMEWE
Kitabu kipo katika hatua za Mwisho. Na hapa ni katika pointi ya Beba Udhaifu wa Mumeo; Mfichie Aibu. Jukumu kubwa la nguo ni kuusitiri mwili. Hili ni jukumu la mwanzo na muhimu kuliko yote. Ni kweli nguo ina kazi nyingine kama vile ya urembo au kufanyika pambo, ila la kwanza kabisa ni kuufunika utupu. Aliyevaa nguo na ikaonyesha utupu, ni anajaribu kutuambia ya kuwa hajavaa nguo. Anapaswa kurudi katika Mwanzo sura ile ya tatu, ambapo Adamu na mkewe walipogundu waa uchi walilazimika kutafuta sitara.
Ambapo sitara hiyo ya vazi la majani haikuweza kukidhi hitaji, Mungu akawapatia vazi la ngozi. Sasa kama Mungu aliliondoa vazi ambalo bado lingeonyesha utupu na kuwapatia zuri zaidi. Uwe na hakika anayekataa zuri zaidi na kuvaa lenye kuonyesha utupu kuna shida kichwani; na shida hii itakuwa imeanzia moyoni. Huwa nasema hivi; nguo haina dhambi, ila nguo huwakilisha moyo wa dhambi au moyo mbovu.