Jumatano, 28 Januari 2026

Karibu katika Mfululizo Wetu wa 1, wa Kitabu Chetu Hiki Kipya cha #KUJARIBIWA KWA IMANI katika Mada ya Cha Kufanya #Unapotupwa Kwenye Shimo, Pointi ya 1.

Na Mwl Oscar Samba

1. Cha Kufanya Unapotupwa Kwenye Shimo

1. Uwe Utayari na Ufahamu ama Akili ya Kukubali Kuishi Katika Shimo. Lugha ya kutupwa katika shimo ina maana ya kushushwa au adui kunuia kukuua. Ni aina ya pigo la kukung'oa au kukuangamiza kabisa kabisa. Mfano vijana wale wa tatu wa Yuda alipotupwa katika tanuru la moto; Meshack, Shedraka na Aberinego. Danieli katika shimo lenye simba wakali. Alikadhalika Yusufu gerezani, maana alitolewa katika maisha ya utukufu, na kisha kushushwa chini ghafla. Alikadhalika pia alipotupwa katika shimo na nduguze, na kisha kuuzwa utumwani. Maisha ya utumwa kwake bado yalikuwa ni kama shimo, maana anatolewa katika familia ya

Jumatatu, 26 Januari 2026

Karibu Katika Mfululizo Wetu wa 10, katika Kitabu Chetu Hiki cha CHA #KUFANYA UNAPOKUWA NJIA PANDA. Pointi ya 8-10

Mwl. Oscar Samba

8. #Uwe na Utulivu Moyoni. Nimekujuza kuwa kama hujui cha
Kufanya usifanye chochote, ila na hapa nakutaka pa kuhakikisha ya
kuwa unakuwa na utulivu moyoni. Ukapata kibali cha kusoma kitabu
chetu kinacho uelezea nafasi ya mwili wa mwandamu au viungo vyake katika kumtumikia Mungu; kuna jambo muhimu sana utalipata
pale.

Jambo hilo lipo katika tukio la Nuhu akiwa katika Safina. Alimtuma
kunguru na kugundua kuwa muda bado wa kutoka safinani. Mara
baada ya muda kadhaa kupita, akamtuma njiwa: mara ya kwanza na
alirudi na jani la mti bichi. Napo kuna kitu aligundua ya kwamba bado
hakujakauka. Mara ya mwisho akamtuma na hakurudi tena; ndipo
alipogundua ya kuwa nchi imekauka!

Hakuwa na haraka, hakuchukua maamuzi hadi alipojiridhisha; sio

Jumatano, 21 Januari 2026

Karibu katika Mfululizo wa 9 wa Kitabu Chetu cha CHA KUFANYA UKIWA NJIA PANDA . Katika Pointi ya 7. Na Mwl Oscar Samba 7. Kama Hujui cha Kufanya Usifanye Chochote

 Watu wengi wamejikuta wakiwa katika njia isiyo sahihi mara baada ya kupitia 

kipindi cha ukimya wa Mungu. Kuna kipindi Mungu huwa kimya kama 

sehemu ya jaribu kwetu. Ikiwa imani yetu kwake inapimwa, jambo la 

sabra na hata nidhamu, utii na hofu kwake; ni kwamba ni kweli 

tunamtegema na kumtumaini Yeye! 

Japo wakati mwingine anaongea lakini hatuelewi, na pia kuna muda 

anaona hata akiongea hatutamuelewa. Usisau pia ukimya wake, huweza 

kuwa ni matoke ya hasira yake juu yetu. Maana hata mfalme Sauli kuna 

wakati Mungu hakusema naye; baada ya kukorofishana naye, na 

kujikuta akigeukia msaada kwa mganga wa kienyeji. Na alilalamika 

kuwa Mungu hasemi naye hata kwa ndoto.

Sasa, Nisikilize; Mungu anapokua kimya, au unapofikia katika hatua 

Jumamosi, 17 Januari 2026

Usiogope Na Uwe Mwaminifu Hadi Kifo

Uwe Mwaminifu hadi kifo maana yake uwe na msimamo ambao utakuwa tayari kulipa gharama yoyote ile.

Pia tunaambiwa ya kuwa, ukishinda kuna madhara utaepukana nayo; hii inatupa kufahamu bayana ya kuwa, zipo faida za ushindi.

 Tazama Andiko : Ufunuo wa Yohana 2:10 Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima. 

11 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatapatikana na madhara ya mauti ya pili. 

Ninalowiwa kukupatia Majira haya ni kukutia moyo ya kwamba USIOGOPE na nikutake kuwa Mwaminifu huku ukijua mwisho wake kuna ushindi tele.

Maumivu nyakati kama hizi ni muhimu, ila mwisho wake umejaa mafanikio tele...kuna majira unalazimika kuingia gharama kwa ajili ya kulinda kile ulichokibeba ....

Jumatano, 14 Januari 2026

Karibu Katika Mfululizo wa 8 wa Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UKIWA NJIA PANDA, Pointi ya 5.

 Na Mwl. Oscar Samba

 5. Omba Mpenzi ya Mungu Yatimie.* Unajua maana yake ni nini?

Ni kwamba, umefikia mahali ambapo kwa akili na fahamu zako, 

hujui mpango wa Mungu, ama unajua lakini huna ujasiri na uwezo 

wakuukukabili! Sasa mwambie Mungu sio kama mimi nitakavyo bali 

mapenzi au mpango wako, ama njia yako ndiyo niiendee, sio njia 

nyingine. Yaombe haya kwa mzigo mkubwa sana, na kwa kumaanisha 

kwa viwango vikubwa mno.

22:41 Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba, 

42 akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; 

walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke. 

Jumanne, 13 Januari 2026

Jifunze Kubariki na Kubarikiwa Katika Swala la Uzao, na Kuoa au Kuolewa

Watu wengi hawaijui hii siri...ndio maana sio wepesi wa kuzidai baraka hizi iwe ni kutoka Madhabahuni, (kwa watumishi wa Mungu) Wazazi na Kadhalika...

Hata wao wanaopaswa kuzitoa wengi wao hawana weledi wa kutosha kuwahusu au kuzihusu....

Nikiwa katika mkoa ambao hivi sasa nipo, nimejikuta nashangaa kuona sherehe za SendOff hata za watu walio okoka zisizokuwa na ibada ndani yake.

Sherehe hizo unakuta nyingine zinaudhuriwa hata na wachungaji na zinafanyikia kanisani ama mazingira hayo...lakini hata muda wa neno la Mungu haupo...(Hawajui kilichotokea kwa Rebeka saa anaagwa).

Jumapili, 11 Januari 2026

#Muamshe Yesu Kwenye Maisha Yako*

Sikatai ya Kwamba Yesu Unaye, Nakubali Kabisa...

Ila Umemfanya Kukosa Chakukufanyia Kiasi cha Yeye Kutulia au Kunyamaza Kimya...

Ni sawa na wewe kualikwa ugenini alafu mwenyeji wako akawa anafanya kila kitu...hali hiyo inakufanya kukosa jambo la kufanya...

Na unajikuta umekaa mkao wa kusubiri kuambiwa walau nisaidia kukatakata mboga ama kufagia hapo nje...hii ikupe kuhakikisha unamfanya Yesu Kutokutulia katika Maisha Yako...

Siku moja wanafunzi wa Yesu wakapaswa kuvuka  kutoka ng'ambo moja na kuelekea Gerasi...katika boti Yesu hakupewa chakufanya...akalazimika kulala....walipokutwa na Dharuba Majini Ndipo Walijikuta Wakimuamsha....hapo ndipo alipoingia kazini na kuwasaidia....jifunze kitu hapo..

Jumamosi, 10 Januari 2026

Mfululizo wa 7, Katika Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UKIWA NJIA PANDA, Pointi ya 4.

Na _Mwl. Oscar Samba_ 

 4. Tafuta Ushauri Sahihi.

Hapo juu nimekupa mfano wa huyu baba ambaye alifikia mahali

pagumu sana kimaamuzi, ila mkewe alimshauri asimwache Mungu.

Badala yake waombe, nukuu moja wapo inamtaja au inamkariri huyu

baba akiwa anasema kuwa, Mungu amempa mke mzuri sana maana

alimshauri vyema!


Katika nyakati kama hizi ni muhim kujua umhimu wa namna ya

kukabiliana na shauri mbalimbali, maana wapo marafiki wataabishaji

ambao hawataacha kuja kwa nia ya kukuyumbisha kiushauri.

Kwenye fikra zako ni alzima kuwa na akiba ya hekima na maraifa ya

namna ya kukabilina na mamabo au amsuari au hali amahizi;

Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na