Jumanne, 29 Aprili 2025

Pasaka ya Kweli: UKOMBOZI SAHIHI KATIKA MSAMAHA WA DHAMBI.

 Ujumbe huu ni Sehemu ya Kitabu Chetu Kipya cha MOTO WA UAMSHO KATIKA BIBLIA. Ni kitabu kinachochambua kila Tukio la KiUamsho Ndani ya Biblia nzima.

Na Mwl Oscar Samba 

 Kitabu cha Kutoka. Sura ya 12 ...

Somo la...... UKOMBOZI KWA NJIA YA DAMU: Kristo Yesu Ndiye Pasaka.

1 Wakorintho 5:7 Basi, jisafisheni, mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa donge jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa chachu. Kwa maana Pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani, Kristo;

8 basi na tuifanye karamu, si kwa chachu ya kale, wala kwa chachu ya uovu na ubaya, bali kwa yasiyochachika, ndio weupe wa moyo na kweli. 

Tunajulishwa ya kuwa Kristo ndiye Pasaka wetu, na ili kumuenzi au kuyaishi maisha yake basi tunapaswa kuwa na mwenendo au moyo safi ama weupe wa moyo. Tuifanye karamu hii katika hali au kusudio lililokusudiwa pale msalabani ambalo ni la ukombozi wa kutoka dhambini. Tumaanishe katika wokovu, kwa lugha nyingine Ukristo sio dini tu, bali kunabeba maana pana ya kuyaishi yale aliyoyaishi Yesu Kristo. 

Kuyaacha mambo ya kale, maisha ya Misri yako, maisha yenye michanganyiko na chachu za dhambi, uzinzi, masengenyo, biashara za magendo na kadhalika. Ukristo ni Kuokoka, hakuna utofauti kati ya wokovu na Ukristo. Anayejiita Mkristo na hajaokoka huyo ni mpagani mwenye dini. Lazima uiondoe chachu inayokufanya kuwa donge lisilofaa, uwe na maisha safi, maisha bila chachu.

Miongoni mwa imizo kubwa la Mungu katika siku hii ya Pasaka kule Misri ilikuwa ni kula mikate isiyotiwa chachu kwa muda uliopangwa. Lengo lilikuwa ni mkazo wa kiroho katika picha ya maisha ya wokovu, ambapo ni maisha bila mawaa. Sijui unakisoma kitabu hiki ukiwa wapi, na ni lipi dhehebu lako; na inawezekana linasherekea na Pasaka, na yamkini huamini kuhusu wokovu! Pole ni nyingi kwako, maana karamu hiyo unaifanya kwa hasara. Paulo anatutaka kuifanya kwa faida. Bila chachu ndani yake; 1 Wakorintho 5:8 basi na tuifanye karamu, si kwa chachu ya kale, wala kwa chachu ya uovu na ubaya, bali kwa yasiyochachika, ndio weupe wa moyo na kweli. 

Jumatatu, 28 Aprili 2025

Pambano la Nguvu, Ni Vita Dhidi ya Ufalme wa Giza, Mawakala na Wajumbe wa Kuzimu "Maajenti."

Ujumbe huu ni Sehemu ya Kitabu Chetu Kipya cha MOTO WA UAMSHO KATIKA BIBLIA. Katika Pointi ya Pambano la Nguvu (Ni kitabu kinachogusa Matukio na Mambo Muhimu Katika, Biblia Nzuma.)

Na Mwl Oscar Samba 

Kitabu cha Kutoka. Sura ya 7:..

Somo la .... : PAMBANO LA NGUVU; Pigano la Ushindi Dhidi ya Wakala au Mwakilishi ama Mjumbe wa Ibilisi yaani mfalme wa Ufalme wa Giza.

Ni wasaa mwingine mzuri, tunaendelea kujifunza kuhusu Moto wa Uamsho Ndani ya Biblia. Kama nilivyokujuza hapo awali kuhusu pambano la nguvu dhidi ya ufalme wa giza kwa Musa, basi sasa nawiwa kukupanulia swala hili kiupana zaidi. Hapa tutatazama hadi tukio la namna hii la Paulo mtume dhidi ya yule mchawi, pamoja na Daudi na Goliathi. Karibu:

Musa na Fimbo ya Haruni kwa Farao

Mungu alimpatia Musa ishara ya fimbo yenye kugeuka nyoka. Fimbo huwakilisha mamlaka, utawala, uchungaji, pigo na hata heshima kwa mtu wa aina fulani. Mfano, kuna makabila ambayo kijana akifikia umri fulani hukabidhiwa fimbo, au huruhusiwa kutembea na fimbo. Rungu na fimbo, huwa na muktadha unaofanana sana kwa baadhi ya jamii. Kumbuka pia fimbo ni silaha ya ulinzi, makabila yenye utamaduni wa ufugaji, au kuishi porini hili wanalifahamu sana. Pia fimbo, ni ishara ya kuwa nipo tayari kwa safari. Jamii za kale zililijua sana hili; ndiposa katika Kutoka 12 wana wa Israeli walipaswa kula nyama ya Pasaka wakiwa na fimbo mikononi mwao. Ili nini? Ilikuwa ni sehemu ya ishara kwao ya kuwa, wamekaa mkao wa kisafari. Viatu miguuni, mshipi kiunoni, viliwakilisha pia. 

Inapogeuka na kuwa nyoka, ni swala la ishara yenye miujiza ndani yake. (Ishara ni kiwakilishi, maana yake ni kwamba, ukiona alama au jambo hili, fahamu kuna hiki nyuma yake. Kuna alama mtu akiionyesha maana yake ni kwaheri au anakuaga. Nyingine ni anakuita, au anakwambia subiri. Alikadhalika, kuna vitu kama ishara vikitokea, hukujulisha kuwa Mungu yupo hapa. Ama ni MUNGU mkuu ndiye aliyelifa ya hili, na kadhalika.)

Ijumaa, 25 Aprili 2025

Ishara na Miujiza Kwa Mkono wa Musa: MIUJIZA HUITAMBULISHA HUDUMA.

 Ujumbe huu ni Sehemu ya Kitabu Chetu Kipya cha MOTO WA UAMSHO KATIKA BIBLIA (Tunachambua kila Kila Tukio Lenye Uamsho ktk Biblia Nzima).

Na Mwl Oscar Samba 

Kitabu cha Kutoka ... na Yoshua Sura ya 3 na 4, pia Yohana 2:7-11.

Somo la ....: Ishara na Miujiza Kwa Mkono wa Musa: MIUJIZA HUITAMBULISHA HUDUMA.

Shalom mtu wa Mungu, tumekutana tena katika somo jingine. Hapa kwa pamoja tunaangazia nafasi ya ishara na miujiza katika kuitambulisha huduma au mtumishi husika. 

Tukiwa tungali katika wito wa Musa kwenye kitabu hiki cha Kutoka; Musa alipoitwa, na kukabidhiwa majukumu kadhaa, alionyesha hali ya kutokukubalika. Alikuwa na mashaka au wasiwasi kama atapata kibali kutoka kwa watu. Jibu la Mungu lilikuwa ni jepesi tu kwake, Mungu alimpatia ishara kadha wa kadha. Na kumwambia ya kuwa, watamuamini kwa kupitia hizo.

Jumatatu, 7 Aprili 2025

Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba, Uhuru wa Maoni na Kukosoa. Quote of Teacher Oscar Samba, Freedom of Option and Criticizing

If I Don't Have the Freedom of Criticizing; I will Bury My Chance of Praising 

Kama Sina Uhuru Wakukosoa; Nitazika Nafasi  Yangu Ya Kusifia.

By Mwalimu Oscar Samba

Kwa hiyo, Uhuru Wangu Wakusifia, Umefungwa Kwenye Uhuru wa Kukosoa. "Kukosoana ni Afya na Sio Fedheha."

Alhamisi, 3 Aprili 2025

Moto wa Uamsho Katika Biblia

 

Ujumbe huu ni Sehemu ya Kitabu Chetu Kipya cha; MOTO WA UAMSHO KATIKA BIBLIA
(Mwanzo Hadi Ufunuo.)
Na Mwalimu Oscar Samba 
Utangulizi:
1.Kitabu hiki kimenuia kukusaidia kuona mbinu, kanuni, au matukio na matendo ya Kiungu ya kiuamsho katika Biblia.

2. Kina muwezesha Mkristo kwa muhubiri, kuisoma Biblia yote kwa sura ya kiuamsho.

3. Kinanuia kuibuisha tena kusudio la Kiungu lakuleta uamsho, au kuturejesha katika viwango vya kiroho.

4. Kinanuia kuunga mkono na kivitendo ajenda ya kanisa la nchi ya Tanzania na Afrika na baadhi ya makanisa ya nchi nyinginezo: inayohusu uamsho.

5. Ni muongozo wa Kibiblia wa kujifunza uamsho.