Jumatano, 24 Novemba 2021

NI JUKUMU LAKO KUITUMIA MAMLAKA Mathayo 28:18










Mathayo 28:18 Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.

Ni wajibu na jukumu lako, na jitihada zako kuhakikisha ya kwamba unaweka imani na unaipa matendo tena kwa kujiamini ili mamlaka hiyo iweze kuwa halisi kwako.

Wewe ni sawa na askari mwenye bunduki, aspojua kuitumia bado hataweza kumdhuru adui. Na adui akijua muhuska hajui kuitumia basi naye hatamuogopa.

Tumia mamlaka uliyonayo vilivyo.

*Kumbuka* : Sio Jukumu la Yesu kuitumia. Ni lako. Yesu yupo kuiwezesha ifanaye kazi.

Ni muhimu kulielewa hili maana kuna wakati tunamlaumu Yesu na kumuona hajatusaidia kanakwamba Yeye ndie aliyepaswa kuitumia..hapana..alipokabithiwa yote ama vyote, alitukabithi sisi.

Nikikupa bunduki, usipofwetua risasi ni makosa kuilaumu bunduki ama aliyekukabithi... www.ukombozigospel.blogspot.com

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni