Alhamisi, 5 Machi 2020

MREJELEE YESU.


Na Mwalimu Oscar Samba
Waimbaji wakaimba; “Kale nilitembea Nikilemewa dhambi
Nilikosa msaada, kuniponya mateso.
Usifiwe Msalaba! Lisifiwe kaburi!
Linalozidi yote, Asifiwe Mwokozi!

Shalom Mwana wa Mungu, kwa moyo mkunjufu ninakukaribisha katika Makala hii murwa, yenye nia ya kukufanya umrejelee Yesu, ujumbe huu nimeupata usiku wa kuamkia leo nilipokuwa nimelala, ulinijia kama maomo nami nalisikia sauti hii, “mrejelee Yesu,” kisha na andiko hili kunijia; “Tangu wakati wa baba zenu mmegeukia mbali na amri zangu nanyi hamkuzishika. Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi,” asema BWANA Mwenye Nguvu.   ‘‘Lakini mnauliza, ‘Tutarudi  kwa namna gani?” Mlaki 3:7.

Sijui ni jambo gani lililokutatiza kiasi cha kuiamcha Imani, kiasi cha kuamua kurudi nyuma kiroho, kiasi cha kukataa kabisa au kukata tamaa moja kwa moja na safari hii ya wokovu ?

Yamkini unasema mimi sijarudi nyuma kabisa mtumishi, Yesu bado na mpenda, ila nimeishiwa nguvu za kiroho, nimejikuta sina tena kiu wala hamu ya maombi, nimejikuta nimekuwa mzito kusoma neno, na kuudhuria ibada ! Na hali hii ilianza tu pale mama yangu, mume aa muke alipofariki, ama mtoto, na mwingine labla ni baada ya kuugua, au biashara yake kufa ama kufukuzwa kazi, kusema vibaya na wapendwa, kuacha au kukosa msadaa, mwingine yamkini anasema ni mwaka wa sita sasa Mungu hajanijibu, amekaa kimya, hanisiki: kwa hiyo mtumishi hizo ndizo au ndiyo sababu kuu.


Nami nakwambia kuwa wewe uliyeamua kabisa kuacha Imani, na wewe uliyelega kiroho kutokana na ugumu fulani, umrejelee sasa,  japo wengine ni toka wamebarikiwa na Mungu ndipo ilipokuwa mwisho wa ushirika wao, wamesahau maagizo ya Kumbukumbu la Torati, saba na nane, kuwa ukiingia katika hiyo nchi usimuache Mungu, wala usiseme ni akili, au uwezo wako ndio uliokutajirisha.

Wote ninyi, ujumbe huu ni wako, Bwana anasema mrejee Yeye, mrudie leo, naye atakurudia, sijui upo katika hali gani leo, au majira haya, ila hata wewe mwenyewe moyoni mwako u wajua kuwa ujumbe hu ni wako.

Fanya hima leo kumrejelea Mungu, kumbuka alikokutoa, wengine walikuwa wagonjwa Bwana akawajibu, wengine walikuwa hawana kazi au ndoa, ama walikuwa na adha fulani na Mungu kuwatokea, kisha leo mambo yamekuwa mazuri wamemsahau, ni kama vile Mungu alikosea kuwabariki au uwapa majibu yao, sikiliza, siku inakuja, na hicho unachokitumainia hautakiona tena, hakitakwepo tena, utakuta siku moja kimetoweka. Mujiza huo uliokufanya kumwamini Yesu utageuka kuwa “shubiri.”

Inasikitiksha sana mtu alikuwa hana kazi, alikuwa masikini, kabla ya ndoa alikuwa muimbaji na shemasi mzuri kanisani, kipindi cha taabu yake alikuwa haachi kuudhuria kanisani, kila wakati na hata majira ya maombi ya mkesha huwezi kumkosa kwenye kusanyiko, ila sasa toka amejibiwa, anatoa visingizio vingi, “ubize” sasa sijui Mungu amnyanganye kazi ili awe na nidhamu?

Mtu mmoja alikuwa hana mtoto, na alikuwa muudhuriaji mzuri sana wa ibada, ila alipompata, kisingizio ni mtoto! Sasa mujiza wa mtoto umekuwa kikwazo, mchungaji wake akamwambia vipi tuombe Mungu amchukuwe huyo mtoto ili upate muda sasa wa kuja kanissani ?

Uhusiano wako na Mungu usijengwe na vitu, au kitu, maana kama umerudi nyuma kwa sababu Mungu hajakujibu ombi lako la kuolewa au kuoa, ama la uponyaji wa ndoa yako, au kwa kuwa hajakuponya au kumponya ndugu yako, mkeo ama wewe mwenyewe, ama kwa kuwa tu huduma haikui, ama uliomba ndugu ama mtu wako wa karibu asife na akafa, alafu kwa jambo hilo umerudi nyuma, umekaukiwa kabisa nguvu za maombi, huwezi hata kuomba dakika moja, huwezi tena kusoma neno, kwa sababu tu ya ugumu wa maisha, hakika umejenga msingi wako juu ya udongo, tope au mchanga.

Leo nakusii umrejelee Mungu, naye anasema kuwa atakurejelea, wewe, ni muhimu na lazima kujua na kufahamu kuwa Mungu atabaki kuwa Mungu hata kama hajajibu maombi yako, hata kama hajafaya kama ulivyohitaji, hata kama hajakupatia haja ya moyo wako, kukujibu au kutokujibu, hakumbadilishi, Yeye husalia kuwa Mungu.

Hili ni jambo muhimu sana, Daudi alifunga na kuomba, ila bado mtoto alifariki, na jambo ile halikubadlisha Uungu wa Mungu, Ayubu alipitia mahali pa gumu na alikuwa mwenye haki, na jambo hilo halikuondoa Uungu wa Mungu !

Uliomba apone, na amefariki, bado Mungu ni Mungu, uliomba uolewe nabo milango ni migumu, Mungu ni Mungu, habadiliki, atasalia kuwa Mungu, na uhusiano wako na Mungu usijengwe kwemye vitu, maana hata Ayubu anatufundisha hili jambo, kwani ungejengwa kwenye vitu ni lazima angekwama, ndio maana akatuambia haya maneno;

“Kwani msiba utokao kwa Mungu ulikuwa na kitisho kwangu, na kwa sababu ya ukuu wake sikuweza kufanya neno.  ‘Kama nimeweka tumaini langu kwenye    dhahabu,  au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe    salama yangu,’ kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu,  ustawi ambao mikono yangu ilikuwa    imepata, …” Ayubu 31:23-25.

Ukuu wa Mungu sio wa kuhojiwa, Mungu ni Mungu, amekujibu, hajakujibu, asaliye kuwa Mungu kwako, wala usiinuwe kinywa chako kwa maneno ya ukaidi kama ya yu wapi Mungu mbona hajanijibu, mbona hataki kunijibu, mbona hajibu maombi, huyu Mungu sio sahihi, na kadhalika, kama una mwaswali iwe ni katika kuhojiana naye katika heshima kuu, katika unyenyekevu, katika sala na sio katika manung’uniko, maana kitu kikubwa kilichowaponza wana wa Israeli ilikuwa ni manung’uniko, sasa wewe epuka hili ili uwe salama.

Mkuu wangu wa chuo, Mwalimu Mkuboba aliwahi kusema hivi, kuwa kipindi akiwa anasoma kuliwahi kutokea msiba wa mwanafunzi mwenzao waliompenda sana, na alikufa akiwa katika kutumwa na chuo, “na kama unavyojua ni mwanafunzi wa chuo cha Biblia” sasa hili liliwaumiza naye aliumia, sasa alijipanga kwenda kwenye ukumbi wa maombi au ibada ili kumuhoji Mungu, akiwa njiani anasema, alikutana na maswali magumu sana ya Mungu, “Wewe ni nani hata uhoji ukuu wangu, ulikwepo wapi wakati na muumba, mkataba wangu na wewe unakuhusu nini?”

Anasema baada ya hapo alijikuta akimtukuza Mungu, na kumshukuru, na kumsifu, ama kumuadhimisha, katika hili jaribu kujiuliza kama Ayubu angalitazama aliyoyapitia katika jicho la namna hii ? hakika ni kwamba angekwama tu !

Jifunze sana kumfanya Mungu kuwa ni Mungu hata kama hajakujibu kama ulivyotaka au kuhita, jicho lako lizidi kumtazama Yeye daima, naye sio dhalimu atakutokea na kukujibu tu, ila fahamu kuwa ni kwa muda wake, ni katika majira yake, sio yako, hufanya kama apendavyo Yeye, usimlazimishe kama upedavyo wewe, maaana sasa hapo unataka kumfanya Yeye awe wewe na wewe uwe Yeye, haya hayawezekani.

Natumai sasa upo tayari kumrejelea ! maana nje ya hapo jehanam ya moto inakusubiri, usifikirie utaenda mbinguni kwa kuzingatia historia la ! Mtu mmoja akaniambia kuwa mimi nilimjengea Mungu ubavu mmoja wa jengo la kanisa nikausimamisha unafikiria Mungu ataniacha ?

Huu nao ni ujinga ule wa kwanza, maana bora wa mwisho maana yake ni mwenye kiwango kidgo cha ujinga, ila wa kwanza kazidi wengi kwa huo ulumbukeni!

Mwingine anadhani kuwa ataenda mbinguni au kuhesabiwa haki kwa kuwa tu anatoa sana sadaka kanisani, au anawategemeza sana watumishi, ni kweli mbele ya mchungaji wako unaweza kuwa na kibali, ila sio mbele za Mungu !

MUGU wetu ni mwenye haki, utakatifu ndio sifa pekee ikuwezeshayo kufika mbinguni au kuhesabiwa haki, na sio vinginevyo, kuwa mtoto wa mchungaji, mama mchungaji au mchungaji ama mwinjilisti au nabii mstaafu sio tiketi ya wokovu, au kuhesabiwa haki !

Geuka leo, ni kwli tunakuona u mtumishi mzuri ila kwa kweli umeoza, unazini kwa siri, unalewa kwa kificho, umejaa masengenyo na uchonganishi, Mungu anakutaka kurejea kwake leo, umemuacha na kumuasi vya kutosha, leo rudi, leo rejea kwake, na fanya hima maana mlango bado haujafungwa, kumbuka enzi za Nuhu,w atu waliendelea kunywa, na kulewa na kuzini, ila muda wa mwisho ulipofika, walijikuta wakitafuta msaada na kuukosa, rejea leo, ile watu wanakuona u mtumishi, sio kigezo cha kuhesabiwa haki, kumbuka hili daima.

Sasa kama u, tayari kurudi, imizo langu kwako ni hili, tubu sasa, omba msamaha sasa, nyeyenyekea sasa, na ukaache ule uovu wako wote, 2 Nyakati 7:14, hapo kuna na uponyaji na kuondolewa misiba, kama tu utamaanisha, na urejesho wa mali, ndoa, uchumi, na maisha kama tu utamaanisha kiukweli.

Sasa yamkini unataka kuokoka, mara baada ya kuguswa na Mungu katika ujumbe huu, au ulikuwa umeokoka na kurudi nyuma, au ulilega katika uhusiano, tafadhali fanya sala hii ya toba pamoja nami kwa Imani;

Sema, MUNGU BABA, NINAKUJA MBELE ZAKO, NINATAMBUA YA KUWA MIMI NI MWENYE DAHAMBI, NINAKUOMBA UNISAMEHE, NA ULIONDOWE JINA LANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, NA TAFADHALI ULIANDIKE KWENYE KITABU CHA UZIMA WA MILELE, NA NIPE KUMAANISHA KWENYE WOKOVU, NISHINDIE VISHAWISHI NA KILA DHAMBI INIZANGAYO KWA HARAKA, NINAKUAMINI NA KUKUPOKEA MOYONI MWANGU KAMA BWANA  NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, Amen.

Hongera kwa kukoka, na sasa tafuta kanisa la watu walioka, ukasali hapo sasa, wambie umeokoka hivi karibuni, ili wakulee vyema, na kama ulishaokoka ukarudi nyuma, tafadhali eleza udhaifu wako wa awali kwa mchungaji ili aombe pamoja nawe, na usitende dhambi tena, pi usikubali kujihukumu nafsini mwako kwa makosa yoyote yale ya awali maaana Damu ya Yesu imeshakuondolea hatia zote.

Kwa mawasiliano tafadahli wasiliana nasi, Simu 0759859287, baruapepe: ukombozigospel@gmail.com.
Asante, ujumbe huu nimeuombea na hakika utasalia moyoni mwako daima, na kukupa nguvu wewe uliyeko katika hali ya kuzimia, au kuchoka kiroho, Isaya 40:28-31.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni