Jumanne, 23 Desemba 2025

Mfululizo wa 6 Katika Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UKIWA NJIA PANDA.

Mada ya 2 ya Mambo Mengine ya Kufanya au Kuepuka Ukiwa Njia Panda.

Na _Mwl. Oscar_ Samba 

Pointi  ya 3. Ingia kwenye Maombi ya Muda Mrefu. Yanaweza pia yasiwe 

ya muda mrefu, ila yakawa ya kina na mazito au yenye mzigo mzito. 

Lakini imizo la maombi ya muda mrefu sio la kupuuza, ni muhimu sana 

kulizingatia. Yanaweza kuwa ya siku tatu kavu, masaa 24, au ya wiki 

moja. Huweza kuwa katika mfumo wa masaa 12 au 24 kwa 24 ama 

masaa 36 na kadhalika. Ni kadri Roho wa Bwana atakavyo kuongoza.

Kuna baba mmoja alikuwa akipitia mahali pa gumu sana, aliingia ubia 

wa kibiashara na mtu ambapo ilimbidi aweke dhamana mali zake 

muhimu. Na Yule mtu baadae akajakukimbia na ile fedha; alifikia hatua 

ya kutaka kujiua. Maana ilikuwa ni fedha nyingi, mkewe alimshauri 

asijidhuru badala yake wa mgeukiye Bwana.

Jumatatu, 22 Desemba 2025

3⃣ SERA YA UFALME WA MBINGUNI KUHUSU UJENZI WA NYUMBA YA KUISHI KWA “RAIA” WAKE WALIOKO DUNIANI πŸ–Š Mwl.CHRISTOPHER MWAKASEGE.

Bwana Yesu asifiwe sana!

Masomo ya wiki mbili mfululizo zilizopita, juu ya Sera ya ufalme wa Mungu kuhusu ujenzi wa nyumba za kuishi, yamezaa maswali kadha kutoka kwa wasomaji.


Maswali hayo yalihusu kupata ufahamu zaidi, juu ya sera hii ya ufalme wa Mungu. Tumeyapokea hayo maswali, ingawa si rahisi tukayajibu yote, kwa sababu ya “ufinyu” wa nafasi ya kufanya hivyo.

Lakini kwa leo tunataka tujibu swali moja, kati ya maswali mengi yaliyoulizwa, – na tunaamini majibu hayo yataongeza ufahamu zaidi juu ya utekelezaji wa sera hii.

Swali lenyewe lenyewe liliulizwa hivi: “Je, unatushauri kuweka wakfu au kuitakasa ardhi kabla ya sijajenga?”

Majibu yake ni haya:

Kuna tofauti kati ya kutakasa kitu,

Alhamisi, 18 Desemba 2025

Mfululizo wa 1 wa Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UNAOOKUWA NJIA PANDA

Tunaanza na Utangulizi (kinapatikana Google Bure)

 Na Mwl. Oscar Samba

 Utangulizi

Kitabu hiki kimenuia kumsaidia mtu ambaye yupo katika mazingira

magumu ya kimaamuzi, na mbele yake kuna aina zaidi ya moja ya

maamuzi ambayo anahatarishwa kuyachukuwa au yanayomkabili,

inawezekana lililo hatari ni moja, au salama ni moja ila kuna zaidi ya

aina mbili au moja na kadhalika.

Kitabu hiki ni matokeo ya sehemu ninayopitia sasa kuhusu ndoa yangu.

Ikumbukwe sasa ni mwaka unaokaribia wa nane toka mwenzangu

tuoane na kujikuta ananiacha kwa talaka mahakamani hali inayonipa au

kunipelekea kuwa njia panda. Njia panda yangu inaweza isiwe na tija

sana kwako ila la muhimu ni wewe kufahamu mazingira ya kitabu

hiki ili kikusaidia. (Wakati nakitoa, imetimia miaka 10/11, “2015-

2015”.)

Unaweza usione umuhimu wake kwa leo ila nikuhakikishie kuwa

chakula hiki ni kama akiba, kuna muda tunakula leo lakini chakula

hicho kinatusaidia kesho; sio kwamba tuliingia kwenye mfungo la! Bali

homa ya ghafula imetukuta na kutunyima hamu au uwezo wa kula. Ila

kwa akiba ya jana ambayo hatukuwa hata na wazo la kula tumevuka leo

salama!

….Nikikuongezea ni kwamba, mara baada ya kuandika

utangulizi huu, na nikiwa tayari nimeshaanza kukiandika hiki

kitabu, njia panda nyingine ilijitokeza kama sio moja basi ni

zaidi, licha ya swala la ndoa, lakini pia limeibuka swala la

kusimamishwa masomo chuoni. Kumbuka nipo katika chuo cha

Biblia Dodoma cha CBC; mara baada ya kutofautiana na

kiongozi wangu mmoja wapo katika swala fulani, nilijikuta

nikipewa adhabu ya kusimamishwa masomo mwaka mmoja.

Nikiwa tu nimetoka kuchukuwa barua zangu, (ikiwa moja yangu na ya

mchungaji wangu kingozi,) ndipo nilipokutana na mchungaji mmoja wa

dhehebu jingine akiniambia kuwa nihamie kwake. Maana huku

kumekuwa kugumu kwangu na katoa sababu kadhaa: zingeweza

kuonekana ni zenye mashiko maana nyuma ya pazia jambo langu

limeonekana ni matokeo ya mimi kuwa na tabia ya kutetea na kudai haki. Pamoja na kusema ukweli pale ambapo ninapoona mambo

hayajaka sawa.

Wazo hili halikwepo kabisa kichwani mwangu, maana nilishapitia

mahali kama hapa mara baada ya uongozi wangu wa sehemu huko

Arusha kutofautina nami na kunichukulia mamuzi ambayo sikuyapenda

maana sikusikilizwa kimapana!