Jumamosi, 20 Juni 2020

Usizike Ndoto Zako.



Na Mwalimu Oscar Samba
Utangulizi
Ninamshukuru Mungu kwa kibali na upendeleo alionipa kuhusu kitabu hiki, ni kweli nimeandika vitabu vingi ila hiki kinaupekee wa aina yake! Vipo vingi kweli vyenye kutia moyo watu, ila hiki nacho kina kitu chake cha upekee.

Kitabu hiki kinaitwa USIZIKE NDOTO ZAKO, haikuwa jambo la akili zangu kukipata, nilikuwa najisomea darasani muda wa usiku, na ghafula nikasikia Roho Mtakatifu anaugua, nilijitahidi kuhakikisha kuwa ninamaliza kwa haraka ratiba yangu ya kuhakikisha nasoma biblia kabla ya kwenda kulala maana niligundua moyoni kuwa muda wangu wa kukaaa darasani umeniishia!

Lakini haikuwa rahisis kukubaliana na wazo hili la Roho Mtakatifu maaana nilitakiwa au nilihitajika kusoma zaidi kwa mujibu wa ratiba yangu, natumai ndio maana aliamua kutumia njia ya kuugua ili kunishindikiza!


Wakati nikiwa natoka kujisomea saa naenda bwenini kulala, naliwaona wanfunzi wenzangu wakijifanyia mazoezi ya kuhubiri, ghafula nikapata wazo la kuungana nao, nilijitahidi kulitii maana ni wa darasa jingine, na ngazi ya chini kidogo
 kitaaluma, kwa hiyo nilijitia moyo kuwa yamkini nikapata kibali kwao, walinipokea na kujiungana nao, kisha alisimama Mchungaji mwanafunzi mmoja aitwae Ben, na kuhubiri ujumbe huu!

Moja kwa moja, nilifahamu moyoni mwangu kuwa ndicho ambacho Mungu alinuia nikipate, kwanza kutokana na mahali nilipokuwa ninapapitia, pili niligundua moyoni mwangu! Ujumbe huu nimepewa niuendeleze kama kitabu!

Maana alipoutaja tu, nilipewa picha nzima ya anapoelekea na kuanza kufunuliwa kana kwamba nilikwepo naye wakati anauandaa, alipomtaja mwanamke husika nilipewa picha yote kabla ya kudadavua zaidi!

Nilimshukuru Mungu na kuanza kukimungunya kitabu hiki nafsini mwangu (moyoni) mwangu!

Kwa hiyo kitabu hiki kimenuia kukutia moyo, kwa njia ya kimaarifa, ambayo yanakutaka kutokufanya makosa au maamuzi ambayo moja kwa moja yatazika ndoto, mipango, maono, au mambo uliyonuia kuyafanya au mahali ulipotaka ama unapotamani kupafikia!

Msingi mkubwa wa kitabu hiki upo katika kisa kile cha mwanamke yule tajiri wa Shunami, mama huyu alikuwa hana mwana, na alipopata mwana alifariki, lakini mtoto alipofariki hakumzika, bali alimwendea Elisha, na wewe yamkini ndoto zako zimekufa, kuna jambo ambalo umeliona haliwezekani, usikubali kukata tamaa bali muendee Yesu!

Kuna makosa kadhaa ambayo wengi huyafanya hususani tunapokutwa na tatizo, badala ya kuchukuwa hatua ya kuliponya, au kulihuisha moja kwa moja huenda kulizika!

Sijui kama huwa unajifunza kwa mwanmke yule mjane wa mji wa Naini, kuwa mwana wake alipofariki moja kwa moja alichukuwa hatua za mazishi kama watu wengine! Ila ashukuriwe Mungu alimuonea huruma na kuzua kuzikwa kwa mtoto!

Sasa usiniulize mimi ujumbe huu ulipotolewa ulinisaidiaje kutokuzikwa kwa jambo fulani maishani mwangu ila hapa jitazame wewe maana ya mkini upo kwenye msafara wa mazishi ya ndoto yako ya kutaka kuja kuwa mwalimu kisa tu umefeli mtihani wa kidato cha nne, mwingine amejikatia tamaa na kuona kuwa hawezi tena kuwa dakitari kisa na mkasa ni mara baada ya yeye kushindwa kupata ada ya masomo, wapo walioacha kabisa ama kufikiri hata kufanya hivyo maana ndoto yao ya kuwa mfanya biashara aliyefanikiwa ni kama vile haiwezekani tena kwa sababu tu ya hali ya uchumi kuwa ngumu, na sasa wapo kenye maandalizi ya mazishi ya ndoto zao kama yule mjane wa mji wa Naini!

Mpendwa! Ingekuwa hivyo, basi Mungu asingekuwa ni Mungu wa utukufu! Ili atukuzwe ni lazima kuwe na bahari ya Shamu mbele, na nyuma kuwe na jeshi kubwa la Misri, alafu akiigawa bahari ya Shamu utukufu uje kwake! Kufa kwa mtoto sio mwisho wa maisha ya mototo! Inawezekana ndio mwanzo mpya wa maisha yake!

Ni kwamba Shetani anaweza kuua ndoto, ila wewe ukamsaidia kuizika! Ndoto inaweza kuzimia lakini wewe ukaisaidia kuimalizia kabisa, na huu ni ukatili mbaya sana ni sawa na madakitari wanao wadunga wagonjwa sindano za vifo eti kwa kuwahurumia maana wameteseka sana!

Tutakapokuwa tukianza uchambuzi wa kisa hiki, utajionea mambo kadhaa ambayo huyu mwanamke aliyafanya, kwani wengine wangepiga ukunga na kuanza kuandaa mipango ya mazishi!
Ni sawa na yule ambaye aliyekosa ada na kuamua kuondoka chuoni mwenyewe bila hata kufukuzwa na mwalimu husika, na kukata tamaa kabisa na elimu! Ni sawa na mchungaji aliyekimbia eneo la huduma kisa ni ligumu kiroho, bila kujua kuwa penye mwamba ndipo Musa alipoamriwa apapige ili maji ya toke! Na hakuna dhahabu inayochimbuliwa vumbini, bali ni mchangani!

Huduma ikiwa ngumu, na washirika wote kukukimbia, na kufikia hatua hadi mwenzi wako wa ndoa kuwa kizuizi, wewe nawe usianze kuisema vibaya, huko ni kuimalizia, kwa maana kwamba yamkini imezimia sasa kwa maneno yako ni kwamba unaiua!

Na usifikie hatua pa kuanza kuwa na mipango ya kukimbia, au kuondoka, maana huko ni kumpangia marehemu mipango ya kumzika, wewe kata rufaa mbele za Mungu, maana kama mifupa mikavu iliweza kuishi uwe na hakika kuwa huduma yako yaweza fufuka, la muhimu wewe usiizike ndoto yako, maana ni kweli adui anaweza kuiuwa, ila jambo la kuzika ni lako, ajali ya barabarani inaweza kuondoa uhai wa mpendwa wako sawa, ila swala la kuzika ni lako! Sio la ugonjwa wa malaria, au ebola, ama ugonjwa fulani, bali wazikao ni wanadamu, kwa hiyo usiruhusu na wengine kukuhubiria kushindwa maana hao ndio wachonga majeneza ama  wachimba kaburi wa ndoto zako!

Ukija katika kitabu kile cha Ezekieli 37, kuna jambo muhimu sana pale najifunza, “Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi BWANA, nitakapoyafunua makaburi yenu, na kuwatoa ninyi katika makaburi yenu, enyi watu wangu.”

Anazungumza na watu wake! Lakini wapo makaburini! Sasa hawa sio marehemu kwa jinsi ya kawaida, maana huwezi kuongea na waliokufa, ninachotaka ukione hapa ni hii picha ya kiroho kwamba kuna namna matumaini yalikauka ndani yao, kuna namna waliishiwa kabisa muono wa mbele, sasa na Mungu ananuia kuwatoa kwenye makaburi, ambayo yalizika ndoto zao! Ni kweli maisha waliyokuwa wakiyaishi yalisadifu hayo kutokana na ugumu wake maana walimuasi Mungu, ila la muhimu hapa ni wewe kufahamu kuwa haijalishi upo katika wakati mgumu kiasi gani, ni chini ya adhabu ya Kiungu, au ni mapito, juwa tu kwamba hutakiwi kuzika ndoto yako, na kama ilishazikwa, usiwe na shaka; mifupa mikavu ya elimu yako, utumishi wako, ndoa yako, biashra yako ni lazima vifufuke.

Kwa hiyo ninawiwa kukukaribisha katika kitabu hiki ambacho kinanuia kukujengea ulinzi maalumu kimaarifa, ambao utakusaidia kutokuchukuwa maamuzi mabovu, ama ambayo siyo sahihi punde unapokuwa katika hali ngumu! Elia aliwahi kupitia hapo! Na kufikia hatua ya kutamani kuzika ndoto zake za utumishi! Alimwambia Mungu amuuwe! Sasa nawe usifike hapo! Nafasi bado unayo, yakikushinda wewe; wewe yaache msalabani! Karibu:

Kwa hiyo kitabu kikitoka tafadhali kitafute, na tunavyo vingi vya kutia moyo, pamoja na vile vyenye kukuwezesha kutimiza ndoto zako, vya kukuza kiroho na kadhalika:

Lakini mpendwa kuna jambo muhimu sana nataka ulifahamu, sijui kama umeokoka, kama la, nakutia moyo kuhakikisha ya kwamba unamruhusu Yesu leo aingie katika maisha yako, kuokoka sio habari ya dini mpya, ni Yesu kuingia ndani yako, na kukuwezesha kuishi maisha matakatifu, ili ukifa uwe na hakika ya kwenda mbinguni, nje ya wokovu ni jehanum ya moto milele, moto uunguzao na kuchoma, maandiko husema kutakuwa na kilio na kusaga meno, jaribu kufikiri hayo ni maumivu makubwa kiasi gani!

Ila waliookoka wataishi na Mungu milele, wataishi naye na kukaa naye karibu, watakula raha za mbinguni! Sasa amuoa leo, wala usiseme kesho! Mapito na maisha ya hapa duniani ni ya muda mfupi sana, huna uwakika na hiyo kesho au wewe usemaye kuwa ipo siku, hujui ni lini, fikiri ni wangapi waliopanga kuwepo leo ila hatunao tena! Ni wangapi ambao hukutarajia kuwa kama wangekufa mapema lakini hatuko nao tena! Yesu anakupenda, namuona akibisha katika mlango wa moyo wako, ili aingia wewe sasa mpe nafasi! Anakuita kwa huruma, yu tayari kuikupa faraja ya milele, kukuponya majeraha ya moyo wako! mruhusu awe Baba yako sasa ili akusaidie katika mambo ambayo ni magumu kwako, yamkini ni uchumi, fedha, hazipatikani, unazingirwa na nuksi na mikosi, kila unalofanya haliendi, unakabwa na mapepo, ! Wewe njoo kwa Yesu na hayo yote yatapita kabisa        ! Sasa natumi u tayari!
Sema; MUNGU BABA, NINAKUPENDA, ASANTE KWA KUNIPENDA KWANZA, LEO NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NA NIPO TAYARI KUOKOOKA, TAFADHALI INGIA NDANI YANGU, SAMEHE DHAMBI ZANGU, NA FUTA JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKU, NA ULIANDIKE SASA KATIKA KITABU CHA UZIMA WA MILELE, Ameni.

Kwa kufanya hiyo umekwisha kuokoka sasa, na tafadhali tafuta kanisa la watu waliokoka lililopo karibu nawe ukasali, hapo, waambie kuwa umeokoa hivi karibuni, ili wakulee vyema kiroho.
Mawasiliano yetu, kwa M-Pesa au Simu: +255 759 859 287, barua pepe: ukombozigospel@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni