Jumatatu, 12 Februari 2024

Ni Sehemu ya Kitabu Chetu Tarajiwa cha IMANI SAHIHI, Katika Mada ya Misingi na Tabia za Imani Sahihi.

 


Mwalimu Oscar:

Mwl OSCAR SAMBA ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu: #Usiogope
 Lengo la kitabu hiki ni kukuwezesha kuijua au kuitambua imani ya kweli, na kuzifahamu hila za adui Shetani katika imani potofu; ikiwemo namna ya kuzitofautisha na ile ya kweli na jinsi ya kuzishinda.

Misingi na Tabia za Imani Sahihi
Maana ya Imani. Katika Biblia na hata maisha yetu ya kawaida, neno imani limegawanyika katika maana zaidi ya moja, na huweza kuwa na maana kuu mbili. Mosi ni ile imani kama kuwa na hakika ya jambo unalolitarajia ambalo bado hujalipata ama kuliona ila unamatumaini nalo. Waebrania 11:1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.
Unganisha na hili andiko; Warumi 8:24 Kwa maana tuliokolewa kwa taraja; lakini kitu kilichotarajiwa kikionekana, hakuna taraja tena. Kwa maana ni nani anayekitarajia kile akionacho?

Maana ya Pili ya Neno Imani: Ni mfumo au "settings" ya mambo muhimu yenye kunuia kuunda aina fulani ya njia ya mtu; kimtazamo, fikra na hatimaye kimatendo, (kiimani "faith:") yenye kufuma namna ya kuabudu kwake, kusali, miiko fulani na maadili muhimu ya kuishi hapa

Jumanne, 23 Januari 2024

KUSAMEHE, MSAMAHA Na Christopher Mwakasege

 Felix Mbwanji:

SAMEHE NA KUSAHAU (BY MWL, C.MWAKASEGE)

                            

TABIA YA MUNGU YA KUSAMEHE NDANI YAKO

         Ulipompokea Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako, ulipokea tabia ya aina gani?

"  Bali wote waliompokea (Kristo) aliwapa uwezo wa  kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu." (Yohana 1:12,13)


         Ulipozaliwa mara ya pili kwa Neno la Kristo ulifanyika kuwa mtoto wa Mungu.

Watoto wa Mungu wana tabia ya namna gani?

         Kwa kuwa wamehamishwa toka ufalme mwingine na uzazi mwingine, na kuingizwa katika ufalme wa Mungu na uzazi wake (Wakolosai 1:13); watoto hawa wanatakiwa wawe na tabia nyingine.


          Kabla ya kuzaliwa mara ya pili, kabla ya kumkiri Kristo ya kuwa ni Bwana: ulikuwa na tabia ya dunia hii iliyoongozwa na mfalme wa dunia hii ambaye ni shetani.

          Ulipozaliwa mara ya pili na kuukiri wokovu katika Kristo, ulipokea tabia mpya inayoongozwa na Mungu mwenyewe aliye ndani yako.


"  Kwa kuwa uwezo wake wa Uungu umetukirimia  vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa (Utakatifu), kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe. Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno; za thamani,ili kwamba kwa hizo mpate kuwa Washirika wa TABIA YA UUNGU, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa." (2 Petro 1:3,4)

Jumatatu, 8 Januari 2024

NDOTO ZA UZINIFU au MAPEPO MAHABA, ama Kuota Unazini Ndotoni Maana yake ni Nini?

Na Christopher Mwakasege_


 Leo nataka tujifunze juu ya “Mwongozo wa kutafakari na kuombea ndoto zenye UZINIFU AU UASHERATI ndani yake”.

Maneno haya ‘uzinifu na uasherati’ yanahusu ufanyikaji wa tendo la ndoa usio halali kibiblia. Uzinifu linatumika zaidi wakati tendo la ndoa limefanywa na mtu ambaye hajaoa au hajaolewa. ‘Uasherati’ linatumika zaidi wakati tendo la ndoa limefanywa nje ya ndoa na mtu ambaye ameoa au ameolewa.


Mtu anayepata ndoto zenye mambo hayo, huwa zina madhara makubwa sana ya kiroho, na ya kimwili – kwa aliyeota ndoto hizo!

Kumbuka kwamba: Neno la Mungu la biblia, kwa kushirikiana na Roho Mtakatifu, linatuongoza kujua namna ya kutafsiri na kuziombea ndoto za aina yo yote – ambazo ni pamoja na hizi zenye mambo ya uzinifu au uasherati ndani yake.

Jumatano, 3 Januari 2024

Ni Sehemu ya Kitabu Chetu Tarajiwa cha MAANA YA UZIMA, NA UZIMA WA MILELE. Pwenti ya 2, katika mada ya pili ya Uzima wa Milele

 Mwl OSCAR SAMBA ( #NasahazaMwlOscar )

#FaidayaJaribu: #Usiogope

Na Mwl. Oscar Samba

Kwenye Kipengele cha Faida za Uzima wa Milele

2. Tunakula Matunda ya Mti wa Uzima. Huu ni mti wa ajabu sana. Kumbuka mti huu ndio uliowafanya Adamu na mkewe kuondolewa kwenye bustani ya Edeni. Mimi na wewe leo hatupo hapo bustanini kwa sababu ya hii dhambi. 

Mungu alihofia wasije wakala na kisha wakaishi milele. 

Ufunuo wa Yohana 2:7 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu. (Nikutie moyo pia kuhakikisha unashinda vita, majaribu, maana mbingu ni mji wa washindi! Sio sehemu ya walioshindwa! Hili lijue na ulifikiri daima maana ni taswira halisi unayopaswa kuwa nayo kwenye fahamu zako.) 

Tujione Siri hii muhimu kule Edeni:

Mwanzo 3:22 Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele; 23 kwa hiyo Bwana Mungu akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo katika hiyo alitwaliwa.

24 Basi akamfukuza huyo mtu, akaweka Makerubi, upande wa mashariki wa bustani ya Edeni, na upanga wa moto uliogeuka huko na huko, kuilinda njia ya mti wa uzima.

Kilichowafanya kuondolewa sio uzuri wa bustani! Sio kwamba wameshafanya dhambi kwa hiyo hawastaili tena kuendelea kula mema ya hiyo bustani, la! Bali ni kwa sababu ya uwepo wa huu mti. Ndiyo sababu kubwa Mungu anayoitoa anapowaondosha hapo. 

Ijumaa, 29 Desemba 2023

Mwalimu Oscar Samba FIKRA SAHIHI KATIKA SHAMBA LA BWANA Kitabu cha Kiroho Kipakuwe Bure free download

Mwalimu Oscar Samba FIKRA SAHIHI KATIKA SHAMBA LA BWANA Kitabu cha Kiroho Kipakuwe Bure free download 




Sabato Maana Yake ni Nini ? MAANA YA SABATO KIBIBLIA Ielewe Sabato ya Kweli

 


Na Mwl Oscar Samba

#FaidayaJaribu: #Usiogope

Ni Sehemu ya Kitabu Chetu Tarajiwa cha MAANA YA UZIMA, NA UZIMA WA MILELE. Pwenti ya Pumziko Kuu.

Kwenye Kipengele cha Taswira ya Uzima wa Milele

Pumziko Kuu; Yaani Sabato Kukuu. Watu wengi hawajui ya kuwa Sabato maana yake ni pumziko katika kilele cha uzima wa milele yaani wakati huu hapa ulimwenguni kwa kuokoka, (kupumzika katika Kristo Yesu kama mtua mizigo ya dhambi na kila mateso.) Na pili kama sehemu ya kupumzika kutoka katika dunia iliyopo chini ya umiliki wa Shetani kama mungu wa dunia hii, na pamoja na dunia yenye pigo la laana la kosa la Adamu na Hawa. 

Unapookoka ni umeingia katika Sabato. Kwa hiyo, msabato halisi ni mtu aliyeokoka. Kama hujaokoka wewe sio Msabato, maana bado upo chini ya utumwa wa Shetani. Wokovu unakupa pumziko. Kanuni na sheria zile za Agano la Kale hususani sabato na taratibu zake zote, zilinuia kutufikisha hapa kwenye wokovu na hatimaye katika Sabato kamilifu ile ya Mbingu Mpya na Nchi Mpya.

Ndiposa Yesu alipokuja, mkazo wa sheria za kisabato ule wa Agano la Kale haukwepo tena. Maana amekuja Sabato Mwenyewe. Ndio maana alijibu hivi; Marko 2:27 Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato. 28 Basi Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato pia. ( Kwa hiyo kama utaendelea kusingizia kumsikiliza mjumbe wa Sabato Musa na kumuacha Bwana wa Sabato; basi utakuwa umekwama sana.

Mathayo 12:5 Wala hamkusoma katika torati, kwamba siku ya sabato makuhani hekaluni huinajisi sabato wasipate hatia? 6 Lakini nawaambieni, kwamba hapa yupo aliye mkuu kuliko hekalu.

7 Lakini kama mngalijua maana yake maneno haya, Nataka rehema, wala si sadaka, msingaliwalaumu wasio na hatia. 8 Kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.

Tuone kisa kingine:

Jumapili, 17 Septemba 2023

Kila Jaribu Lina Mlango wa Kutokea JIPE MOYO

 

Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu:

1 Wakorintho 10:9 Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.

:11 Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.

:12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.

:13 Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.

http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL

Nikutakie Siku Njema

Jumamosi, 16 Septemba 2023

Neno la Leo #Nenola Leo #NenolaMungu #NenolaBiblia #Ujumbe waSiku

 

Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu:

Waebrania 4:2 Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema vile vile kama hao. Lakini neno lile lililosikiwa halikuwafaa hao, kwa sababu halikuchanganyika na imani ndani yao waliosikia.

:6 Basi, kwa kuwa neno hili limebaki kwamba wako watu watakaoingia humo, na wale waliohubiriwa habari ile zamani walikosa kuingia kwa sababu ya kuasi kwao,..

:7 aweka tena siku fulani, akisema katika Daudi baada ya muda mwingi namna hii, Leo; kama ilivyonenwa tangu zamani, Leo,kama mtaisikia sauti yake, Msifanye migumu mioyo yenu.

Usiufanye Mgumu Moyo Wako..(Safari ya Wokovu Ni Kila Siku) Hakikisha Unafanya Matengenezo Kila Uonapo Dosari Maishani Mwako..ikihubiriwa Injili Usiikatae, na Usiseme Wananisema... Shinda Vikwazo Ili Uingie Rahani Mwake Yesu..

http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL

Nikutakie Siku Njema

Ijumaa, 8 Septemba 2023

Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar ) #FaidayaJaribu: Waebrania 5 inatupa Kufahamu Umuhimu wa Aina ya Chakula cha Kiroho

 

Waebrania 5:12 Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu.

:13 Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga.


:14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya.

Kama Nilivyokuhaidia Jana, ni Kwamba Aina ya Chakula Unachokula Ndicho Kinachoamuwa kama Uendelee kuwa Mwanafunzi au Mwalimu. Na kwa mujibu wa Jana Washindi Wana Aina Yao ya Vyakula, (Mana Iliyofichwa.)

http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv

Kwa Maombi +255759859287 

Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/Mafun

Alhamisi, 7 Septemba 2023

Neno la Leo: MANA ILIYOFICHWA KWA ASHINDAYE

 

Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu:

Ufunuo wa Yohana 2:17 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea.

Kuna aina ya Viwango vya Kiroho Vinavyoamua Upewe Chakula Gani cha Kiroho, Kutokana na Kushinda Kwako Majaribu..Kwa Wahubiri; Ukihitaji Kuwa na Mafundisho Tofauti yasiyoyakawaida, Huna Budi Kushinda Vikwazo ili Upewe Mana Isiyo ya Viwango vya Kawaida. (Natumai Kesho Utanielewa Zaidi..)

http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL

Nikutakie Siku Njema

Jumanne, 29 Agosti 2023

Faida ya Jaribu na Dhima ya Utoaji au Kumtunza Mtumishi wa Mungu ( soma sura yote ya Wafilipi 4 )


 Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )

#FaidayaJaribu:

Wafilipi 4:8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.

:9 Mambo mliyojifunza kwangu na kuyapokea, na kuyasikia na kuyaona kwangu, yatendeni hayo; na Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.

:10 Nalifurahi sana katika Bwana, kwa kuwa sasa mwisho mmehuisha tena fikira zenu kwa ajili yangu, kama vile mlivyokuwa mkinifikiri hali yangu lakini hamkupata nafasi.


:19 Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.

(Baraka Hizi za Paulo Zinakuja Baada ya Hawa Watu Kusimama Kwenye Nafasi Yao)

http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv

Jumanne, 22 Agosti 2023

Faida ya Majaribu au Mapito ( Mtazame Yesu )


 Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )








 Faida ya Jaribu :

Waebrania 12:3 Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu.


:4 Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi;


Tunapewa Nasaha za Kumtazama Yesu Aliyestahimili Mambo Magumu kwa Ajili Yetu, Hata Akautoa Uhai wake..Mimi Na wewe Hatujafikia Kipimo Hicho cha Kuimwaga Damu...Nasi Hatuna Budi Kuyastahimili kama Yeye Alivyofanya kwa Ajili Yetu..Nasi Tufanye kwa Ajili Yake..


http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD


Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk


Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv

Kwa Maombi +255759859287 


Nikutakie Siku Njema

Jumatano, 16 Agosti 2023

SEMINA KKKT MWANZA 2016. NA MWL CHRISTOPHER MWAKASEGE KOSA LA SABA. 7.YESU AKIAMUA KUTOITULIZA DHORUBA USIMKASIRIKIE BALI ENDELEA KUOMBA NA KUFUATA MAELEKEZO YAKE.

 7⃣SOMO:JIEPUSHE NA MAKOSA YAFUATAYO UKITAKA KUVUKA KWA USHINDI MWAKA HUU


Hili ni eneo ambalo unahitaji kulielewa sana kwa sababu si kila mtu atapita mahali ambako pako shwari.

Kila mtu anapita kwenye dhoruba yake na si kila dhoruba ni mbaya.

Warumi 8:28.
28 Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.

Simama kwenye kusudi la Mungu shetani hawezi kukuzamisha atajaribu kila namna lakini atashangaa ukisimama kwa upya.

Kuna matatizo mengine Mungu anayaruhusu kwa ajili ya kukujengea msuli wako kwa ajili ya mambo yaliyopo mbele yako.

Yesu aliomba “kikombe hiki kiniepuke” alikuwa anajua kabisa angeweza kuamuru jeshi la malaika kumtetea na kumpigania, angeweza kuwatoroka, lakini Biblia inasema mbigu zilinyamaza kwa sababu Mungu hakuwa na mpango wa kumwondolea msalaba,kwa sababu msalaba ungeondolewa hakuna mahala tungekombolewa.

Mungu akinyamaza usikasirike, endelea tu kuomba kwa sababu inawezekana ni jambo bado majira yake.

Tatizo tunambea katika majira ambayo tunahisi tunapopata matatizo tunahisi tumepungukiwa imani lakini kumbe hatujajua ni sehemu ya safari au sehemu ya maisha.

Hakuna mtu hapa Duniani atayekuambia matatizo ni mazuri. Lakini tunapotembea hapa Duniani hakuna mtu yeyote ambaye hatakutana na matatizo, kwa hiyo usijaribu kuishi na mawazo kwamba hautakutana na matatizo.


 Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )


Yakobo 5:10 Ndugu, watwaeni manabii walionena kwa jina la Bwana, wawe mfano wa kustahimili mabaya, na wa uvumilivu.

:11 Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.

http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287

Nikutakie Siku Njema

Jumanne, 15 Agosti 2023

BWANA ANA HAJA NAWE


Na Mwl Oscar Samba 

Duniani hatukuja kwa bahati mbaya, lipo kusudio la kuumbwa kwetu. Kama vile mtu anavyomuajiri mfanyakazi na kisha kuwa na malengo naye katika eneo analohitaji asaidiwe kazi, ndivyo na Mungu wetu alivyotuumba akiwa na kusudio maalumu la uumbaji wake kwetu.

Nimfano wa mtu aliyenunua chombo chake cha usafiri! Hapana shaka huyu mtu huwa na malengo katika matumizi fulani ya hicho chombo. Mimi na wewe ni chombo cha Mungu. Mungu hakutuumba kwa bahati mbaya, wala hukuzaliwa kwa bahati yoyote kama vile wengineo huweza kuzania. Kila mtu amezaliwa kwa kusudi la Mungu lililo kamili kabisa.

Wasomaji wa kitabu kile cha Zekaria wanajuwa kuna unabii ulitolewa kuhusu punda ambaye Yesu alikuja kumtumia miaka kadhaa mbele katika Agano Jipya. Najuwa kuna jinsi jambo kama hili huweza kuonekana kuwa ni dogo, lakini lilishatabiriwa au kuangaziwa toka miaka mingi yenye oroda ya mamia ya miaka ama mlolongo wa karne nyingi.

Usipojuwa unaweza kuliona hili tukio kuwa ni la kawaida ila kiuhalisia lilishaandaliwa; Marko 11:2 akawaambia, Nendeni mpaka kile kijiji kinachowakabili; na katika kuingia ndani yake, mara mtaona mwana-punda amefungwa, asiyepandwa na mtu bado; mfungueni, kamleteni.

3 Na mtu akiwaambia, Mbona mnafanya hivi? Semeni, Bwana anamhitaji na mara atamrudisha tena hapa.

Luka 19.33 Na walipokuwa wakimfungua mwana-punda, wenyewe waliwaambia, Mbona mnamfungua mwana-punda? 34 Wakasema, Bwana ana haja naye.

Sasa jaribu kufikiia kama punda anaandaliwa hivi kwa ajili ya tuko la siku moja tu! Je, wewe sii Zaidi? Ambaye unatarajiwa kutumika miaka na miaka! 

Jumatano, 9 Agosti 2023

Neno la Leo, Kufurahia Pito au Majatibu, kwa Ajili ya Injili au Kristo

 

Neno la Leo (Nasaha za Mwl Oscar)

Mathayo 5:11 Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu.

:12 Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.

*Kesho nitakupa Mfano wa Watu Waliofurahia Mateso na Dhiki ikiwemo Kupigwa kwa Ajili ya Yesu au Injili..Unapaswa Kufurahia Kufukuzwa Kazi, Kuonewa na Hata Kubaguliwa ama Kuchukiwa kwa Ajili tu Wewe Umeokoka...Kila Dhaa kwa Ajili ya Imani Yako, Kwako Lifurahie Maana Malipo Yake ni Mkaubwa Mbinguni... Maana Bila Hayo Taji Yako ni Ndogo* ...

www.ukombozigospel.blogspot.com

Jiunge na Kundi Letu la Telegram

https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Kwa Maombi: +255759859287

Uwe na Siku Njema