Jumatatu, 7 Aprili 2025

Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba, Uhuru wa Maoni na Kukosoa. Quote of Teacher Oscar Samba, Freedom of Option and Criticizing

If I Don't Have the Freedom of Criticizing; I will Bury My Chance of Praising 

Kama Sina Uhuru Wakukosoa; Nitazika Nafasi  Yangu Ya Kusifia.

By Mwalimu Oscar Samba

Kwa hiyo, Uhuru Wangu Wakusifia, Umefungwa Kwenye Uhuru wa Kukosoa. "Kukosoana ni Afya na Sio Fedheha."

Alhamisi, 3 Aprili 2025

Moto wa Uamsho Katika Biblia

 

Ujumbe huu ni Sehemu ya Kitabu Chetu Kipya cha; MOTO WA UAMSHO KATIKA BIBLIA
(Mwanzo Hadi Ufunuo.)
Na Mwalimu Oscar Samba 
Utangulizi:
1.Kitabu hiki kimenuia kukusaidia kuona mbinu, kanuni, au matukio na matendo ya Kiungu ya kiuamsho katika Biblia.

2. Kina muwezesha Mkristo kwa muhubiri, kuisoma Biblia yote kwa sura ya kiuamsho.

3. Kinanuia kuibuisha tena kusudio la Kiungu lakuleta uamsho, au kuturejesha katika viwango vya kiroho.

4. Kinanuia kuunga mkono na kivitendo ajenda ya kanisa la nchi ya Tanzania na Afrika na baadhi ya makanisa ya nchi nyinginezo: inayohusu uamsho.

5. Ni muongozo wa Kibiblia wa kujifunza uamsho.

Alhamisi, 27 Machi 2025

Amani na Umoja ni Nguvu, na Ni Ishara ya Upako

*Ujumbe wa Leo* 


Chumvi Ndani Yetu (Roho Mtakatifu/Ushuhuda wa Kristo/Utakatifu/Utu Wema


Hutuwezesha Kukaa Kwa Amani Baina Yetu (Sisi kwa Sisi)


Kwa hiyo, Tukipoteza Umoja, Mapendano Baina ya Ndugu, ni ishara ya kwamba Hatuna Chumvi. Au Magomvi Baina Yetu, Hutuondolea Chumvi.


Marko 9:50 Chumvi ni njema; lakini chumvi ikiwa si chumvi tena, mtaitia nini ikolee? Mwe na chumvi ndani yenu, mkakae kwa *amani ninyi kwa ninyi.* 


 Salt is good: but if the salt have lost his saltness, wherewith will ye season it? Have salt in yourselves, and have peace one with another.


By Mwalimu Oscar Samba


Zaidi Soma: https://ukombozigospel.blogspot.com/?m=1

Jumamosi, 22 Machi 2025

Kitabu cha CHAKUFANYA UKIWA NJIA PANDA, Kitakufikia Punde.

 

Ni kwa Njia ya PDF free. Zidi Kutuombea

Utakipata kwa Namba hizi hapa kwa WhatsApp +255759859287

Andika Neno Vitabu

Utatumiwa na Vitabu Vinginevyo Vingi vya Mwl. Oscar Samba 

Jumatano, 19 Machi 2025

Quote of Teacher Oscar Samba in Learning and Teaching

 











Any Good Preacher Should Remember This: We Are Still Learning, We Are Still Teaching.

It will help us from too much self condemnation.


By Mwalimu Oscar Samba

Zaidi Tembelea:

https://ukombozigospel.blogspot.com/?m=1

#quote #t #teaching #learning #Oscarsambaquotes #preacher

Jumanne, 18 Machi 2025

Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba MAOMBI DHIDI YA JARIBU


Usipotumia Nguvu Nyingi Katika Maombi, ili Kuyashinda Majaribu: Utalazimika Kutumia Jitihada Nyingi Katika Kuyavumilia na Kukabiliana Nayo.

 

By Mwalimu Oscar Samba 


Zaidi Tembelea: https://ukombozigospel.blogspot.com/?m=1

Jumamosi, 15 Machi 2025

Mwl Oscar Samba Nukuu ya Watoto au Kijana ama Vijana Chipukizi na Utumishi

 

Kumjua Mungu na Kumpenda


































"Tusiwasukumie Watoto Wetu Kwenye Utumishi ili Wamjue Mungu. Bali Tuwasaidie Kwanza Kumjua Mungu Ndipo Wamtumikie."

By Mwalimu Oscar Samba 

Utaukuta Kwenye Kiatabu Chetu cha 

UMUHIMU WA KUMJUA NA KUMPENDA MUNGU KAMA MTOTO AU KIJANA CHOPUKIZI.

 Zaidi Tembelea: www.ukombozigospel.blogspot.com

Mwalimu Oscar Samba Nukuu ya Wanaokufuatilia

 


Mwalimu Oscar Samba Nukuu, KUKATALIWA NA KUKUBALIWA

 

Dunia Ina Makundi Mawili ya Ndugu: Ana Akili Sana, Tumtenge, Tumchukie, Tumnyime Nafasi Asije Akapata Kibali Kuliko Sisi. Ana Akili Nyingi, Tumpe Nafasi Atatusaidia Miaka Saba ya Njaa.


Mara Nyingi Kundi la Kwanza Huwa Linatangulia. Usikubali Likakuvunja Moyo; Wape Muda Tu, Na Kundi la Pili Litakuja.

By Mwalimu Oscar Samba

Alhamisi, 13 Machi 2025

Andiko Muhimu Katika Biblia

 Utakutana na Ujumbe huu kwenye Kitabu Chetu Kipya Kinachoandikwa Hivi Sasa cha UMUHIMU WA KUMPENDA NA KUMJUA MUNGU KWA MTOTO AU KIJANA CHIPUKIZI

NA Mwl Oscar Samba 

Andiko hili linagusa nyanya zote muhimu kwako wewe kama mtumishi wa Mungu. Mosi ni eneo la kifamilia yaani baba mama na watoto au ndugu zako wengine. Pili eneo la kiserikali, anaposema muheshimu mfalme, hapo pia pana gusa viongozi wako wa kikanisa, viongozi wa kiroho na hata wakitaasisi au kampuni. Kwa ujumla ni kuheshimu utawala. 

Anatupa dhima ya kumcha Mungu, kumpa Mungu heshima yake. Nasi twajua habari za kumcha Mungu! Ya kwamba ni kumuhofu, kuukataa na kuuchukia ovu. Yusufu akasema nitendeje uovu huu ni mkose Mungu? Linaanza na kukutaka kutoa heshima kwa watu wote. Bila kubagua umri, dini, ama kabila na kadhalika. Anasema katika watu wote.

1 Petro 2:17 Waheshimuni watu wote. Wapendeni ndugu. Mcheni Mungu. Mpeni heshima mfalme.



Zaidi Soma: www.ukombozigospel.blogspot.com

Jumanne, 4 Machi 2025

Kwenye Jina Tanzania Kuna Dini Fulani Imejumuishwa Hapo

 The Ahmadiyya is an Islamic reform movement that originated in British India in 1889. Its members believe that Mirza Ghulam Ahmad (1835-1908) was the promised Messiah and Mahdi.



Ijumaa, 28 Februari 2025

Nukuu za Mwalimu Oscar Samba KUISHI TUNAYOYAHUBIRI


 Tusipoishi Tunayo Yahubiri; Kuna Siku Tutaishi Tunayo Yatenda.

Zaidi Endelea Kutembelea  www.ukombozigospel.blogspot.com

Jumatatu, 24 Februari 2025

#Ushuhuda Ni wa Kiongozi wa CASFETA Baada ya Kusoma Kitabu Changu cha KESHO YAKO NI BORA KULIKO LEO YAKO

 


"Ubarikiwe sana mwalim Oscar Samba, kwa kitabu hiki, kimenitia moyo sana kwa hali ninayopitia saiv chuoni, Siku sita nyuma nimekuwa mtu wa kuchoka, kuwa na mawazo mengi na kuhuzunika sana na kukata tamaa, nimekosa amani kulingana na Nafsi niliyonayo katika huduma ya Yesu kristo. Ila jana usiku roho inalisii na kunisisitiza kusoma kitabu hiki, nimekisoma hadi sa nane usk asubuhi nimekimaliza, kweli Mungu akubariki kwa huduma hii, niliwaza hadi kuachia nafasi niliyonayo ya huduma ili nipambane na masomo, ila najikuta nina nguvu za kusimama kuwaongoza tena watu ambao Mungu amenipa kuwaongoza, nimengi sana ya kusema Ahsante sana Mungu kwa neema ya kunikutanisha na Mwalimu Oscar Samba, Mungu akubariki na kukuinua kwa kazi hii. 

    Tuzidi kuombeana

Kesho yangu ni bora kuliko leo yangu, sitakubari kuzimia Moyo, Licha ya changamoto ninazopitia"


Ukikihitaji Kitabu Niandikie Ujumbe huu Wasapu +255759859287

Jumatano, 19 Februari 2025

Yesu Hata Kuacha


 Hakuna Aliyewahi Kuja Kwa Yesu Akamtupa

Haijalishi Unapitia Mahali Pagumu Kiasi Gani, Huna Budi Kuhakikisha ya Kwamba Unaamua Kuokoka

Wokovu Utampa Yesu Nafasi ya Kuyapigania Maisha yako...Anasema Hata Kutupa Kamwe....Hili Ni Andiko la Ajabu Kabisa Katika Biblia.





Jumatatu, 17 Februari 2025

Mama Mchungaji: ISHINDE HOFU YA MAISHA YA BAADAE.


  Na Mwl Oscar Samba 

Ujumbe huu ni Sehemu ya Toleo la Pili la Kitabu Chetu cha NAFASI YA MAMA MCHUNGAJI; KATIKA HUDUMA YA MUMEWE.

Kwenye Pointi ya . Ishinde Hofu ya Kesho Kimkakati, (Maisha Baada ya Huduma au Uwepo wa Mume Wako). Kuna maisha baada au nje ya wito ama Utumishi. Umri ni kigezo muhimu cha kuweza kuwaondoa katika utumishi wa madhabahuni. Kifo pia ni njia ya jambo hili.

Ni kweli kabisa kumekwepo na maisha magumu, na hata manyanyaso mara baada ya mchungaji kufariki, kuondoshwa katika utumishi ama kustaafu. Mke na watoto au familia hujikuta wakiwa katika maisha yasiyo mepesi. Machozi ya uchungu na huzuni uwaandama. Malalmo na majeraha huwa sehemu ya maisha yao.

Hali hii imepelekea hofu kubwa katika nyumba nyingi za kitumishi. Watoto kwa mama wachungaji wamejikuta wakizungukwa na tatizo hili. Na hii

Alhamisi, 13 Februari 2025

Follow the Mwalimu Oscar Samba Mafundisho Ya Neno La Mungu channel on WhatsApp

 Follow the Mwalimu Oscar Samba Mafundisho Ya Neno La Mungu channel on WhatsApp: https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h 

CHUNGA MNASEMA NINI MBELE YA FAMILIA NA WASHIRIKA.


Ujumbe huu ni Sehemu ya Kitabu cha NAFASI YA MAMA MCHUNGAJI; KATIKA HUDUMA YA MUMEWE, Toleo la Pili.

Na Mwalimu Oscar Samba
Katika hii pointi ya Chunga Mnasema Nini Mbele ya Familia, Uzao Wako, Washirika au Kanisa Kuhusu Dhehebu, Viongozi Wako wa Kiroho Dhidi ya Wito Wenu au Utumishi.

Unachopanda Kinaota. Linda Sana Unapanda nini katika fikra na mioyo yao. Watoto ndio kanisa la sasa na kesho. Washirika ndio watumishi wanaoandaliwa. Unaandaa watumishi wa aina gani?

Kumbuka, Upandacho Ndicho Uvunacho. Au Upandacho, Ndicho Tuvunacho!
Iwe ni wewe au mmeo, ama mtumishi mwingine katika madhabahu mliyopewa na Bwana, huna budi kuhakikisha udhaifu huo unaondoka miongoni mwenu. Mbegu nyingi za uasi zinapandwa mioyoni mwa washirika, au watoto kama sehemu ya manung'uniko kutoka kwa wazazi au watumishi wao. Wataponda dhehebu lao, watachambua kila madhaifu, lakini wao hawatoki; wanakuja kushangaa baadae wana watoto au washirika wasiopenda dhehbu la wazazi wao! Wanaanza kutafuta na kujaribu kuwarudisha bila mafanikio!

Hakuna sehemu isiyokuwa na madhaifu, hakuna viongozi waliokamilika. Sema tu, unafanya nini kukabiliana na hayo madhaifu ya wengine hapo ndipo swali lilipo. Malalamiko ya kwamba katika dini hii mchungaji binafsi huwezi kuendelea, michango ni mingi, mara mimi mchungaji nikifa leo mke wangu hatathaminiwa, ni miongoni mwa mambo ya kulinda sana. Mioyo ya watoto huumia wanaposhirikishwa maumivu ya wazazi, na tena huumia zaidi. Wanaanza kukua na "mentality" ya kwamba dini hii inawanyanyasa wazazi wangu. Fikra hizi zinakuja kuamia kwenye mioyo yao.

Machozi unayolizwa na viongozi yalilie bafuni, ili ukimaliza kulia maji unayoogea yaweze kuyasafirisha machozi yote; na lisisalie hata moja. Daudi hakuruhusu ubaya wa Sauli mfalme kuendelea kwenye moyo wa Sulemani mwanaye. Lazima hekima ya namna hii tuwe nayo. Ni hatari tukampa adui Shetani nafasi ya kutufanya kuandaa kizazi chenye "elements" au chembechembe za uasi ndani yake. Na uasi unaotokana na maumivu ni mbaya sana. Magumu unayoyapitia mengine umeandikiwa na Mungu ili baadae ukijakuwa kiongozi uweze kuja kuwa mtu sahihi kwa watu wako.

Nimeshuhudia mtoto wa mchungaji mmoja toka akiwa shule ya msingi na kisha sekondari akijisemea ya kuwa: siku nikiwa mkubwa sitafungua kanisa TAG, Kisa maneno ya malalamiko kutoka kwa wazazi wake. Wenzangu niliokuwa nao wengi walihama dini, kisa mbegu kama hizi. Baadae wanakuja kugundua ya kuwa walifanya maamuzi yasiyo sahihi!

Chunga sana, unalalamika nini kuhusu dhehebu, viongozi wako wa kidini, au utumishi ulio nao mbele ya watoto, uzao wako, mwenza wako na hata kanisa kwa ujumla! Kile unachokifanya kinapandwa ndani yao kama mbegu. Kuotesha mchongoma ni kazi ndogo sana, ila kuung'oa ni kubwa mno.

Baya zaidi, wengine wanachambua madhaifu kama haya, hata mbele ya watumishi ambao wapo chini yao, au ambao tayari anawaanda kabisa kuwa watumishi. Hili ni tatizo kubwa sana. Ni sawa na kubandua vipande vya boti vilivyowekwa kwenye nyufa au maungio ya mbao ya boti mliyoipanda.

Muungwana hutafuta na gundi ili kuziba vizuri kwa nia ya kupaimarisha zaidi. Ni lazima fikra zetu zifikie mahali pa kukua na kukomaa vizuri kabisa katika hili.

Kitabu Kikitoka Kitafute:
Mawasiliano:
Tutembele ama Wasiliana Nasi

http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Tumeunda Channel ya WhatApp, Tufolo;

https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv

Kwa Maombi +255759859287, Email: ukombozigospel@gmail.com

Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook:

https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbW

KwL

Tuandikie pia Maoni Yako; mwalimuoscarvitabu@gmail.com

Jumanne, 11 Februari 2025

Jumatatu, 3 Februari 2025

Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba: Ufunguo wa Uamsho

 


Kumtafuta Mungu Kuna Maana Kuu Mbili
Mosi; Kuna Kitu Kimepotea au Unakitaka, na pili Nia Dhabiti ya Mtafutaji ni Hadi Akipate anachokitaka.
 Huu Ndio Ufunguo wa Uamsho.

By Mwalimu Oscar Samba 
Zaidi Endelea Kutembelea: www.ukombozigospel.blogspot.com 

#Uamsho
#nukuu