Shalom Mtu wa Mungu, Karibu katika Makala hii, ikiwa ni Sehemu ya Kitabu Chetu Kipya cha JIFUNZE KUMUAMINI ROHO MTAKATIFU KATIKA HILO ENEO*..
Na Mwl Oscar Samba
Katika Badiliko la Tabia
. Unageuzwa/Hutugeuza Na Kutupa Maisha Mapya . Dhambi ilipoingia ulimwenguni ilitupatia mwili wenye tabia au vinasaba vya chembechembe za dhambi. Ile mauti iliyonenwa, iliua sehemu kubwa ya asili au ya tabia ama ya vinasaba vya Kiungu katika maisha yetu. Na badala yake, tukatwa asili ya Shetani. Ndiposa kuna kitu Paulo hukiita utu wa kale, pia tabia za mwilini ama mwili huu wa tamaa ama tamaa za mwili. Ndiposa suluhu hutajwa ni kuokoka, ili uwe au uusulubishe mwili wako pamoja na Kristo pale msalabani. Waruni 5-8, na Wagalatia 5 inatusaidia sana katika hili.
Paulo anatufundisha sana kuwa, Yesu alipokuwa anakufa, aliufia mwili wa dhambi. Yaani mauti yake, ilikuwa inauwa asili ya Shetani katika miili yetu; japo kwa lugha ya Kibiblia neno nguvu ya mauti, au utawala wa mauti katika miili yetu linaonekana kutumika zaidi. Kwa lugha nyingine tunasema mfumo wa dhambi. Lile andiko la tulio wa Kristo hatutendi dhambi (1 Yohana 3:6, 8, 9; "ukisoma utakuna na neno mbegu, tafakari kwa kina neno hilo" wa 10, 'unakupa matokeo:') maana yake, tuliookoka hatupo au hatutawaliwi na mfumo au utawala wa dhambi. Ikimaanisha nguvu ya mauti, au mauti twajua ni nguvu ya Shetani kupenyeza dhambi.
Soma; Waebrania 2:14 Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi,