Tusipoishi Tunayo Yahubiri; Kuna Siku Tutaishi Tunayo Yatenda.
Zaidi Endelea Kutembelea www.ukombozigospel.blogspot.com
Zaidi Endelea Kutembelea www.ukombozigospel.blogspot.com
"Ubarikiwe sana mwalim Oscar Samba, kwa kitabu hiki, kimenitia moyo sana kwa hali ninayopitia saiv chuoni, Siku sita nyuma nimekuwa mtu wa kuchoka, kuwa na mawazo mengi na kuhuzunika sana na kukata tamaa, nimekosa amani kulingana na Nafsi niliyonayo katika huduma ya Yesu kristo. Ila jana usiku roho inalisii na kunisisitiza kusoma kitabu hiki, nimekisoma hadi sa nane usk asubuhi nimekimaliza, kweli Mungu akubariki kwa huduma hii, niliwaza hadi kuachia nafasi niliyonayo ya huduma ili nipambane na masomo, ila najikuta nina nguvu za kusimama kuwaongoza tena watu ambao Mungu amenipa kuwaongoza, nimengi sana ya kusema Ahsante sana Mungu kwa neema ya kunikutanisha na Mwalimu Oscar Samba, Mungu akubariki na kukuinua kwa kazi hii.
Tuzidi kuombeana
Kesho yangu ni bora kuliko leo yangu, sitakubari kuzimia Moyo, Licha ya changamoto ninazopitia"
Ukikihitaji Kitabu Niandikie Ujumbe huu Wasapu +255759859287
Haijalishi Unapitia Mahali Pagumu Kiasi Gani, Huna Budi Kuhakikisha ya Kwamba Unaamua Kuokoka
Wokovu Utampa Yesu Nafasi ya Kuyapigania Maisha yako...Anasema Hata Kutupa Kamwe....Hili Ni Andiko la Ajabu Kabisa Katika Biblia.
Ujumbe huu ni Sehemu ya Toleo la Pili la Kitabu Chetu cha NAFASI YA MAMA MCHUNGAJI; KATIKA HUDUMA YA MUMEWE.
Kwenye Pointi ya . Ishinde Hofu ya Kesho Kimkakati, (Maisha Baada ya Huduma au Uwepo wa Mume Wako). Kuna maisha baada au nje ya wito ama Utumishi. Umri ni kigezo muhimu cha kuweza kuwaondoa katika utumishi wa madhabahuni. Kifo pia ni njia ya jambo hili.
Ni kweli kabisa kumekwepo na maisha magumu, na hata manyanyaso mara baada ya mchungaji kufariki, kuondoshwa katika utumishi ama kustaafu. Mke na watoto au familia hujikuta wakiwa katika maisha yasiyo mepesi. Machozi ya uchungu na huzuni uwaandama. Malalmo na majeraha huwa sehemu ya maisha yao.
Hali hii imepelekea hofu kubwa katika nyumba nyingi za kitumishi. Watoto kwa mama wachungaji wamejikuta wakizungukwa na tatizo hili. Na hii
Follow the Mwalimu Oscar Samba Mafundisho Ya Neno La Mungu channel on WhatsApp: https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h
Na Mwalimu Oscar Samba
Katika hii pointi ya Chunga Mnasema Nini Mbele ya Familia, Uzao Wako, Washirika au Kanisa Kuhusu Dhehebu, Viongozi Wako wa Kiroho Dhidi ya Wito Wenu au Utumishi.
Unachopanda Kinaota. Linda Sana Unapanda nini katika fikra na mioyo yao. Watoto ndio kanisa la sasa na kesho. Washirika ndio watumishi wanaoandaliwa. Unaandaa watumishi wa aina gani?
Kumbuka, Upandacho Ndicho Uvunacho. Au Upandacho, Ndicho Tuvunacho!
Iwe ni wewe au mmeo, ama mtumishi mwingine katika madhabahu mliyopewa na Bwana, huna budi kuhakikisha udhaifu huo unaondoka miongoni mwenu. Mbegu nyingi za uasi zinapandwa mioyoni mwa washirika, au watoto kama sehemu ya manung'uniko kutoka kwa wazazi au watumishi wao. Wataponda dhehebu lao, watachambua kila madhaifu, lakini wao hawatoki; wanakuja kushangaa baadae wana watoto au washirika wasiopenda dhehbu la wazazi wao! Wanaanza kutafuta na kujaribu kuwarudisha bila mafanikio!
Hakuna sehemu isiyokuwa na madhaifu, hakuna viongozi waliokamilika. Sema tu, unafanya nini kukabiliana na hayo madhaifu ya wengine hapo ndipo swali lilipo. Malalamiko ya kwamba katika dini hii mchungaji binafsi huwezi kuendelea, michango ni mingi, mara mimi mchungaji nikifa leo mke wangu hatathaminiwa, ni miongoni mwa mambo ya kulinda sana. Mioyo ya watoto huumia wanaposhirikishwa maumivu ya wazazi, na tena huumia zaidi. Wanaanza kukua na "mentality" ya kwamba dini hii inawanyanyasa wazazi wangu. Fikra hizi zinakuja kuamia kwenye mioyo yao.
Machozi unayolizwa na viongozi yalilie bafuni, ili ukimaliza kulia maji unayoogea yaweze kuyasafirisha machozi yote; na lisisalie hata moja. Daudi hakuruhusu ubaya wa Sauli mfalme kuendelea kwenye moyo wa Sulemani mwanaye. Lazima hekima ya namna hii tuwe nayo. Ni hatari tukampa adui Shetani nafasi ya kutufanya kuandaa kizazi chenye "elements" au chembechembe za uasi ndani yake. Na uasi unaotokana na maumivu ni mbaya sana. Magumu unayoyapitia mengine umeandikiwa na Mungu ili baadae ukijakuwa kiongozi uweze kuja kuwa mtu sahihi kwa watu wako.
Nimeshuhudia mtoto wa mchungaji mmoja toka akiwa shule ya msingi na kisha sekondari akijisemea ya kuwa: siku nikiwa mkubwa sitafungua kanisa TAG, Kisa maneno ya malalamiko kutoka kwa wazazi wake. Wenzangu niliokuwa nao wengi walihama dini, kisa mbegu kama hizi. Baadae wanakuja kugundua ya kuwa walifanya maamuzi yasiyo sahihi!
Chunga sana, unalalamika nini kuhusu dhehebu, viongozi wako wa kidini, au utumishi ulio nao mbele ya watoto, uzao wako, mwenza wako na hata kanisa kwa ujumla! Kile unachokifanya kinapandwa ndani yao kama mbegu. Kuotesha mchongoma ni kazi ndogo sana, ila kuung'oa ni kubwa mno.
Baya zaidi, wengine wanachambua madhaifu kama haya, hata mbele ya watumishi ambao wapo chini yao, au ambao tayari anawaanda kabisa kuwa watumishi. Hili ni tatizo kubwa sana. Ni sawa na kubandua vipande vya boti vilivyowekwa kwenye nyufa au maungio ya mbao ya boti mliyoipanda.
Muungwana hutafuta na gundi ili kuziba vizuri kwa nia ya kupaimarisha zaidi. Ni lazima fikra zetu zifikie mahali pa kukua na kukomaa vizuri kabisa katika hili.
Kitabu Kikitoka Kitafute:
Mawasiliano:
Tutembele ama Wasiliana Nasi
http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Tumeunda Channel ya WhatApp, Tufolo;
https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287, Email: ukombozigospel@gmail.com
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook:
https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbW
KwL
Tuandikie pia Maoni Yako; mwalimuoscarvitabu@gmail.com