Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Jipe Moyo. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Jipe Moyo. Onyesha machapisho yote

Jumatano, 19 Februari 2025

Yesu Hata Kuacha


 Hakuna Aliyewahi Kuja Kwa Yesu Akamtupa

Haijalishi Unapitia Mahali Pagumu Kiasi Gani, Huna Budi Kuhakikisha ya Kwamba Unaamua Kuokoka

Wokovu Utampa Yesu Nafasi ya Kuyapigania Maisha yako...Anasema Hata Kutupa Kamwe....Hili Ni Andiko la Ajabu Kabisa Katika Biblia.





Jumanne, 21 Januari 2025

Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba KALAMU YA HISTORIA

 

Usiongeze, Wala Kupunguza Wino Kwenye Kalamu ya Historia ya Maisha Yako. Uliopo Unatosha.

By Mwalimu Oscar Samba


Jumamosi, 2 Novemba 2024

Nukuu ya Mwalimu Oscar Samba, Wokovu, Maisha, Usikate Tamaa, Usivunjike Moyo, Jipe Moyo


Maisha ya Wokovu: Kuna Wakati Hata Kama Huoni mbele; Muamini Aliyekutangulia, yaani Kristo. Kwa hiyo usitumie Nguvu Nyingi Sana Kutazama Mbele, Bali Tazama Alipokanyaga ili Na Wewe Ukanyage.

By Mwalimu Oscar Samba

Jumatano, 3 Januari 2024

Ni Sehemu ya Kitabu Chetu Tarajiwa cha MAANA YA UZIMA, NA UZIMA WA MILELE. Pwenti ya 2, katika mada ya pili ya Uzima wa Milele

 Mwl OSCAR SAMBA ( #NasahazaMwlOscar )

#FaidayaJaribu: #Usiogope

Na Mwl. Oscar Samba

Kwenye Kipengele cha Faida za Uzima wa Milele

2. Tunakula Matunda ya Mti wa Uzima. Huu ni mti wa ajabu sana. Kumbuka mti huu ndio uliowafanya Adamu na mkewe kuondolewa kwenye bustani ya Edeni. Mimi na wewe leo hatupo hapo bustanini kwa sababu ya hii dhambi. 

Mungu alihofia wasije wakala na kisha wakaishi milele. 

Ufunuo wa Yohana 2:7 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu. (Nikutie moyo pia kuhakikisha unashinda vita, majaribu, maana mbingu ni mji wa washindi! Sio sehemu ya walioshindwa! Hili lijue na ulifikiri daima maana ni taswira halisi unayopaswa kuwa nayo kwenye fahamu zako.) 

Tujione Siri hii muhimu kule Edeni:

Mwanzo 3:22 Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele; 23 kwa hiyo Bwana Mungu akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo katika hiyo alitwaliwa.

24 Basi akamfukuza huyo mtu, akaweka Makerubi, upande wa mashariki wa bustani ya Edeni, na upanga wa moto uliogeuka huko na huko, kuilinda njia ya mti wa uzima.

Kilichowafanya kuondolewa sio uzuri wa bustani! Sio kwamba wameshafanya dhambi kwa hiyo hawastaili tena kuendelea kula mema ya hiyo bustani, la! Bali ni kwa sababu ya uwepo wa huu mti. Ndiyo sababu kubwa Mungu anayoitoa anapowaondosha hapo. 

Ijumaa, 29 Desemba 2023

Sabato Maana Yake ni Nini ? MAANA YA SABATO KIBIBLIA Ielewe Sabato ya Kweli

 


Na Mwl Oscar Samba

#FaidayaJaribu: #Usiogope

Ni Sehemu ya Kitabu Chetu Tarajiwa cha MAANA YA UZIMA, NA UZIMA WA MILELE. Pwenti ya Pumziko Kuu.

Kwenye Kipengele cha Taswira ya Uzima wa Milele

Pumziko Kuu; Yaani Sabato Kukuu. Watu wengi hawajui ya kuwa Sabato maana yake ni pumziko katika kilele cha uzima wa milele yaani wakati huu hapa ulimwenguni kwa kuokoka, (kupumzika katika Kristo Yesu kama mtua mizigo ya dhambi na kila mateso.) Na pili kama sehemu ya kupumzika kutoka katika dunia iliyopo chini ya umiliki wa Shetani kama mungu wa dunia hii, na pamoja na dunia yenye pigo la laana la kosa la Adamu na Hawa. 

Unapookoka ni umeingia katika Sabato. Kwa hiyo, msabato halisi ni mtu aliyeokoka. Kama hujaokoka wewe sio Msabato, maana bado upo chini ya utumwa wa Shetani. Wokovu unakupa pumziko. Kanuni na sheria zile za Agano la Kale hususani sabato na taratibu zake zote, zilinuia kutufikisha hapa kwenye wokovu na hatimaye katika Sabato kamilifu ile ya Mbingu Mpya na Nchi Mpya.

Ndiposa Yesu alipokuja, mkazo wa sheria za kisabato ule wa Agano la Kale haukwepo tena. Maana amekuja Sabato Mwenyewe. Ndio maana alijibu hivi; Marko 2:27 Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato. 28 Basi Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato pia. ( Kwa hiyo kama utaendelea kusingizia kumsikiliza mjumbe wa Sabato Musa na kumuacha Bwana wa Sabato; basi utakuwa umekwama sana.

Mathayo 12:5 Wala hamkusoma katika torati, kwamba siku ya sabato makuhani hekaluni huinajisi sabato wasipate hatia? 6 Lakini nawaambieni, kwamba hapa yupo aliye mkuu kuliko hekalu.

7 Lakini kama mngalijua maana yake maneno haya, Nataka rehema, wala si sadaka, msingaliwalaumu wasio na hatia. 8 Kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.

Tuone kisa kingine:

Jumapili, 17 Septemba 2023

Kila Jaribu Lina Mlango wa Kutokea JIPE MOYO

 

Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu:

1 Wakorintho 10:9 Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.

:11 Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.

:12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.

:13 Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.

http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL

Nikutakie Siku Njema

Jumamosi, 16 Septemba 2023

Neno la Leo #Nenola Leo #NenolaMungu #NenolaBiblia #Ujumbe waSiku

 

Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu:

Waebrania 4:2 Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema vile vile kama hao. Lakini neno lile lililosikiwa halikuwafaa hao, kwa sababu halikuchanganyika na imani ndani yao waliosikia.

:6 Basi, kwa kuwa neno hili limebaki kwamba wako watu watakaoingia humo, na wale waliohubiriwa habari ile zamani walikosa kuingia kwa sababu ya kuasi kwao,..

:7 aweka tena siku fulani, akisema katika Daudi baada ya muda mwingi namna hii, Leo; kama ilivyonenwa tangu zamani, Leo,kama mtaisikia sauti yake, Msifanye migumu mioyo yenu.

Usiufanye Mgumu Moyo Wako..(Safari ya Wokovu Ni Kila Siku) Hakikisha Unafanya Matengenezo Kila Uonapo Dosari Maishani Mwako..ikihubiriwa Injili Usiikatae, na Usiseme Wananisema... Shinda Vikwazo Ili Uingie Rahani Mwake Yesu..

http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL

Nikutakie Siku Njema

Ijumaa, 8 Septemba 2023

Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar ) #FaidayaJaribu: Waebrania 5 inatupa Kufahamu Umuhimu wa Aina ya Chakula cha Kiroho

 

Waebrania 5:12 Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu.

:13 Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga.


:14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya.

Kama Nilivyokuhaidia Jana, ni Kwamba Aina ya Chakula Unachokula Ndicho Kinachoamuwa kama Uendelee kuwa Mwanafunzi au Mwalimu. Na kwa mujibu wa Jana Washindi Wana Aina Yao ya Vyakula, (Mana Iliyofichwa.)

http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv

Kwa Maombi +255759859287 

Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/Mafun

Alhamisi, 7 Septemba 2023

Neno la Leo: MANA ILIYOFICHWA KWA ASHINDAYE

 

Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu:

Ufunuo wa Yohana 2:17 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea.

Kuna aina ya Viwango vya Kiroho Vinavyoamua Upewe Chakula Gani cha Kiroho, Kutokana na Kushinda Kwako Majaribu..Kwa Wahubiri; Ukihitaji Kuwa na Mafundisho Tofauti yasiyoyakawaida, Huna Budi Kushinda Vikwazo ili Upewe Mana Isiyo ya Viwango vya Kawaida. (Natumai Kesho Utanielewa Zaidi..)

http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL

Nikutakie Siku Njema

Jumanne, 22 Agosti 2023

Faida ya Majaribu au Mapito ( Mtazame Yesu )


 Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )








 Faida ya Jaribu :

Waebrania 12:3 Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu.


:4 Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi;


Tunapewa Nasaha za Kumtazama Yesu Aliyestahimili Mambo Magumu kwa Ajili Yetu, Hata Akautoa Uhai wake..Mimi Na wewe Hatujafikia Kipimo Hicho cha Kuimwaga Damu...Nasi Hatuna Budi Kuyastahimili kama Yeye Alivyofanya kwa Ajili Yetu..Nasi Tufanye kwa Ajili Yake..


http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD


Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk


Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv

Kwa Maombi +255759859287 


Nikutakie Siku Njema

Jumatano, 16 Agosti 2023

SEMINA KKKT MWANZA 2016. NA MWL CHRISTOPHER MWAKASEGE KOSA LA SABA. 7.YESU AKIAMUA KUTOITULIZA DHORUBA USIMKASIRIKIE BALI ENDELEA KUOMBA NA KUFUATA MAELEKEZO YAKE.

 7⃣SOMO:JIEPUSHE NA MAKOSA YAFUATAYO UKITAKA KUVUKA KWA USHINDI MWAKA HUU


Hili ni eneo ambalo unahitaji kulielewa sana kwa sababu si kila mtu atapita mahali ambako pako shwari.

Kila mtu anapita kwenye dhoruba yake na si kila dhoruba ni mbaya.

Warumi 8:28.
28 Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.

Simama kwenye kusudi la Mungu shetani hawezi kukuzamisha atajaribu kila namna lakini atashangaa ukisimama kwa upya.

Kuna matatizo mengine Mungu anayaruhusu kwa ajili ya kukujengea msuli wako kwa ajili ya mambo yaliyopo mbele yako.

Yesu aliomba “kikombe hiki kiniepuke” alikuwa anajua kabisa angeweza kuamuru jeshi la malaika kumtetea na kumpigania, angeweza kuwatoroka, lakini Biblia inasema mbigu zilinyamaza kwa sababu Mungu hakuwa na mpango wa kumwondolea msalaba,kwa sababu msalaba ungeondolewa hakuna mahala tungekombolewa.

Mungu akinyamaza usikasirike, endelea tu kuomba kwa sababu inawezekana ni jambo bado majira yake.

Tatizo tunambea katika majira ambayo tunahisi tunapopata matatizo tunahisi tumepungukiwa imani lakini kumbe hatujajua ni sehemu ya safari au sehemu ya maisha.

Hakuna mtu hapa Duniani atayekuambia matatizo ni mazuri. Lakini tunapotembea hapa Duniani hakuna mtu yeyote ambaye hatakutana na matatizo, kwa hiyo usijaribu kuishi na mawazo kwamba hautakutana na matatizo.


 Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )


Yakobo 5:10 Ndugu, watwaeni manabii walionena kwa jina la Bwana, wawe mfano wa kustahimili mabaya, na wa uvumilivu.

:11 Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.

http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287

Nikutakie Siku Njema

Jumanne, 15 Agosti 2023

BWANA ANA HAJA NAWE


Na Mwl Oscar Samba 

Duniani hatukuja kwa bahati mbaya, lipo kusudio la kuumbwa kwetu. Kama vile mtu anavyomuajiri mfanyakazi na kisha kuwa na malengo naye katika eneo analohitaji asaidiwe kazi, ndivyo na Mungu wetu alivyotuumba akiwa na kusudio maalumu la uumbaji wake kwetu.

Nimfano wa mtu aliyenunua chombo chake cha usafiri! Hapana shaka huyu mtu huwa na malengo katika matumizi fulani ya hicho chombo. Mimi na wewe ni chombo cha Mungu. Mungu hakutuumba kwa bahati mbaya, wala hukuzaliwa kwa bahati yoyote kama vile wengineo huweza kuzania. Kila mtu amezaliwa kwa kusudi la Mungu lililo kamili kabisa.

Wasomaji wa kitabu kile cha Zekaria wanajuwa kuna unabii ulitolewa kuhusu punda ambaye Yesu alikuja kumtumia miaka kadhaa mbele katika Agano Jipya. Najuwa kuna jinsi jambo kama hili huweza kuonekana kuwa ni dogo, lakini lilishatabiriwa au kuangaziwa toka miaka mingi yenye oroda ya mamia ya miaka ama mlolongo wa karne nyingi.

Usipojuwa unaweza kuliona hili tukio kuwa ni la kawaida ila kiuhalisia lilishaandaliwa; Marko 11:2 akawaambia, Nendeni mpaka kile kijiji kinachowakabili; na katika kuingia ndani yake, mara mtaona mwana-punda amefungwa, asiyepandwa na mtu bado; mfungueni, kamleteni.

3 Na mtu akiwaambia, Mbona mnafanya hivi? Semeni, Bwana anamhitaji na mara atamrudisha tena hapa.

Luka 19.33 Na walipokuwa wakimfungua mwana-punda, wenyewe waliwaambia, Mbona mnamfungua mwana-punda? 34 Wakasema, Bwana ana haja naye.

Sasa jaribu kufikiia kama punda anaandaliwa hivi kwa ajili ya tuko la siku moja tu! Je, wewe sii Zaidi? Ambaye unatarajiwa kutumika miaka na miaka! 

Jumatano, 9 Agosti 2023

Neno la Leo, Kufurahia Pito au Majatibu, kwa Ajili ya Injili au Kristo

 

Neno la Leo (Nasaha za Mwl Oscar)

Mathayo 5:11 Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu.

:12 Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.

*Kesho nitakupa Mfano wa Watu Waliofurahia Mateso na Dhiki ikiwemo Kupigwa kwa Ajili ya Yesu au Injili..Unapaswa Kufurahia Kufukuzwa Kazi, Kuonewa na Hata Kubaguliwa ama Kuchukiwa kwa Ajili tu Wewe Umeokoka...Kila Dhaa kwa Ajili ya Imani Yako, Kwako Lifurahie Maana Malipo Yake ni Mkaubwa Mbinguni... Maana Bila Hayo Taji Yako ni Ndogo* ...

www.ukombozigospel.blogspot.com

Jiunge na Kundi Letu la Telegram

https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Kwa Maombi: +255759859287

Uwe na Siku Njema


Jumatano, 2 Agosti 2023

Neno la Leo, Amani na Maendeleo

 

Neno la Leo (Nasaha za Mwalimu Oscar)

Maombolezo 3:17 Umeniweka nafsi yangu mbali na amani; Nikasahau kufanikiwa.

*Kumbe Amani Ikitoweka na Mafanikio nayo Hupotea au Huwa Adimu..! Kwa hiyo; Hakikisha Amani Haipotei Moyoni Mwako ili Kulinda au Kuchunga na Kudumisha Mafanikio...Tazama Toka Uchungu, Hasira na Msongo wa Mawazo Vilipokukabili..Utakuta na Kasi ya Mafanikio Imepungua na Hata Mambo ya Msingi km Ujenzi na Biashara Kukwama* ..

www.ukombozigospel.blogspot.com

Kundi Letu la Telegram

https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Nikutakie Siku Njema


Jumanne, 14 Februari 2023

kitabu chetu cha: CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO MZITO AMBAPO MUNGU, BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA.

Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu chetu cha: CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO MZITO AMBAPO MUNGU, BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA.

Hiki sii kitabu cha kawaida wala si somo tu bali ni ujumbe. Najua kila ujumbe ni somo katika mukutadha wa mafundisho na ufundishaji. Japo sio kila somo ni ujumbe.

Ujumbe huu ni matokeo ya mahali ninapopapitia ambapo mwaka jana palinipatia vitabu kama viwili hivi. Mosi ni kile cha  HAKUFANYA UNAPOKUWA NJIA PANDA. Na pili ni kile cha MUONE MUNGU NYUMA YA PITO LAKO.

Kwa lugha nyingine unaweza kusema kuwa sii jumbe za kawaida. Bali ni maelekezo. Mfano wa ujumbe kibiblia ni pale mfalme Nebukaddeza alipoota ile ndoto na kisha kujikuta hana tafsiri yake na kuomba msaada kwa Danieli nabii wa Mungu. Tukiachana na yote pale, yale maneno, "Danieli 4:27 Kwa sababu hiyo, Ee mfalme, shauri langu lipate kibali kwako; ukaache dhambi zako kwa kutenda haki, ukaache maovu yako kwa kuwahurumia maskini; huenda ukapata kuzidishiwa siku zako za kukaa raha."


Kwa hiyo, kama Mungu amekupa kukisoma kitabu hiki, moja kwa moja fikra zako zielekeze kwenye ujumbe uliopo ndani yake. Ambao unanuia kumsaidia kwa kumpa mtu husika maelekezo muhimu ya kufanya ili kuendelea mbele na pito au jaribu analolipitia.

Ni matoke ya mimi katika jana ya leo, baada ya kuzungumza na kiongozi wangu mmoja juu ya pito ninalolipitia na majibu ya Mungu juu yangu. Majibu hayo yalinitaka niendelee kuvumilia. Na aliniambia hadi nimalize masomo. Nikauliza je nikimaliza Mungu ndo atanijibu?

Akaniambia hata yeye hajui kama atanijibu au la, ila alichoambiwa ni kwamba kwa wakati huu usijaribu kubeba mambo mawili. Kwa mujibu wa mukutadha wa hekima ile ni kwamba inaonekana maamuzi yangu dhidi ya pito husika nyuma yake hayana mapenzi makamilifu ya Mungu. 

Ijumaa, 16 Desemba 2022

Mngoje Bwana kwa Saburi

rr*MNGOJE BWANA KWA UVUMILIVU* Zaburi 40:1 Nalimngoja Bwana kwa saburi, Akaniinamia akakisikia kilio changu. (Anatuambia kuwa alimnyonga Bwana kwa saburi naye akamuinamia! Kumuinamia maana yake ni kumsikiliza, ni kuweka umakini katika kumsikiliza. Kumuinamia ni sawa na mtu mrefu anapoongeleswa na mfupi, au mtu mzima kwa mtoto mdogo hulazimika kuinama kidogo ili sikio lake lifikile kimo cha kinywa chake.) Endelea na maandiko mengine kisha nitakujuza ninalotamani kukufahamisha hapa: "kichwani weka neno Saburi akiba" :2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu. :3 Akatia wimbo mpya kinywani mwangu, Ndio sifa zake Mungu wetu. Wengi wataona na kuogopa, Nao watamtumaini Bwana :4 Heri aliyemfanya Bwana kuwa tumaini lake, Wala hakuwaelekea wenye kiburi, Wala hao wanaogeukia uongo. Heri aliyemfanya Bwana kuwa tumaini lake! Neno tumaini jumlisha na saburi. Natumai unakumbuka kuwa nilikutaka kuweka akiba akilini neno "Saburi"! Katika mstari ule anatuambia kuwa alimngoja Bwana kwa saburi naye akamuinamia. Yaani anamshinikiza ama kumjibu. Nataka uone neno kumngoja Bwana..kisha neno kwa linatupa kufahamu ni njia ipi au kanuni ipi ilitumika hapa...ni saburi.. Saburi ni nini basi? ... Saburi ni aina ya uvumilivu ambao ndani yake una unyenyekevu, utulivu, amani ya Roho ni pamoja na tumaini katika Bwana kuwa siku moja atamjibu. Nataka kukwambia nini? Haijalishi unapitia mahali pagumu kiasi gani, wewe jifunze kumngoja Bwana kwa saburi..uwe na uvumilivu ambao ndani yake umebeba tumaini thabiti kuwa ipo siku Mungu atakujibu...haijalishi leo kuna ukimya mgumu kiasi gani ila siku moja najua yaja nitajibiwa tu. Nikutie moyo kuwa mngoje Bwana kwa saburi naye atakujibu tu....siku moja yaja, nawe utapokea majibu yako. Na Yamkini haujaokoka, nawe umeguswa na ujumbe huu na unatamani kuokoka (kumbuka wokovu maana yake ni kumkataa Shetani na mateso yake, dhambi na taabu zake na kumkubali Yesu na Uzima ama mbingu)... Kama ndivyo basi nikutie moyo kufuatisha Sala hii ya Toba kwa imani, Sema; EWE MUNGU BABA, MIMI NI MWENYE DHAMBI, NIMEGUNDUA MAKOSA YANGU, NISAMEHE YESU, FUTA MAJINA YANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, NIANDIKE KWENYE KITABU CHA UZIMA WA MILELE, Amen. Hongera kwa Kuokoka na tafadhali tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo, Ameni. ... Zaidi tembelea www.ukombozigospel.blogspot.com Tazama na Sikiliza Mahubiri na Mafundisho Yetu hapa, Usisahau Ku-Subcribe ili uyapate kwa haraka zaidi; https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv Jiunge nasi pia kwenye WhatsApp group letu la mafundisho ya neno la hapa: https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD Kundi letu la Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk (Hapa utapata Mahubiri/Mafundisho Yetu kwa Haraka) Namba ya Telegram au Mawasiliano: +255759859287 inatumika pia kwenye WhatsApp na M-Pesa. Ukiguswa kuachilia Sadaka yako tafadhali usisite kufanya hivyo. Jina ni Oscar Samba. Usisite Kututembelea pia kwenye Ukurasa (Page) wa Facebook na "Ku-like" https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL Ama tuandikie email (Baruapepe) ukombozigospel.@gmail.com

Alhamisi, 24 Novemba 2022

Utangulizi wa #Kitabu chetu cha VUMILIA WAMJUE MUNGU WAKO

Na Mwalimu Oscar Samba

Utangulizi

Hakuna eneo muhinu linalompatia Mungu utukufu kama matokeo ya wewe kushinda vita. Jaribu kufikiria Mungu angejisikiaje kama ujasiri huu aliokuwa nao kuhusu Ayubu kama usingalitimia! Ayubu 2:3 Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu?

 Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, ujapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu.

Najitoa moyo kurudia tena sifa tajwa hapo juu; na miongoni mwa maneno yaliyonigusa kiupekee nje ya hizo sifa ni hili hapa: ambapo nakiri kiuhakik kwamba japo nimekuwa nikikisoma kitabu hiki mara kwa mara lakini bado sikuwahi kukutana na jambo hili katika sura hii. Ya kwamba Shetani kumbe aliwahi kujaribu kumshawishi Mungu amuangamize Ayubu! Ona hili katika kipengele cha mwisho cha hilo andiko hapo juu; "...ujapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu."

Sasa katika mtu kama huyu, jaribu kufikiria mbinguni kungekuwa na msiba mkubwa kiasi gani kama Ayubu angemuangusha Mungu kwenye jaribu au pito lake? Shetani hapana shaka angalimrejelea Mungu na kumwambia kwamba ni bora tu ungalimwangamiza mapema kama nilivyokushauri pale awali.

Uvumilivu wa Ayubu ulimpatia Mungu heshima. Na wewe kuvumilia kwako kutakupatia heshima vivyo. Hakikisha unavumilia, ili Mungu aweze kukushindia pia. Usikubali kukwama kwenye pito lako, bali hakikisha unavumilia na hatimae kushinda.

Lengo kuu la kitabu hiki ni kukuwezesha kuwa na fikra na morali wa ushindi ili kumpatia Mungu heshima. Naye alishasema kuwa akiinuliwa, atawavuta wote kuja kwake. Hii inatupa kufahamu kuwa Mungu akiinuliwa na aliyelibeba jina lake naye anainuliwa. Huduma itapokea kibali maana watu watavutwa kuja kwake, na aliyelibeba jina lake anainuka na jina lililoinuliwa.

Heshima inakuja mwishoni, sio mwanzoni, mwanzoni ni kudharauliwa na kubezwa, kama ilivyokuwa kwa Ayubu, ni majira ya kuzingirwa na marafiki wataabishaji. Sio majira mazuri bali ni magunu, hakuna anayekuelewa. Ila ukishinda ndipo heshima huja. Kama ilivyokuwa kwa Ayubu, mwisho wake ulijawa na utukufu kiasi cha adui zake kuishilia kwenye matengenezo.

Kwa Meshaki, Shedraka, na Aberinego sanjari na Danieli ndivyo ilivyokuwa, waliinuliwa mara dufu mara baada ya ushindi wao. Na kwako inawezekana kama tu utaamua kumtazama Mungu kwa sura tajwa humu kitahuni. Karibu na Mungu akupe kuyaelewa haha:

Tafadhali Kitabu kikitoka  kinunuwe.. zaidi tembelea

www.ukombozigospel.blogspot.com

Jiunge nasi pia kwenye WhatsApp group letu la mafundisho ya neno la hapa: https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD


Kundi letu la Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk


Namba ya Telegram au Mawasiliano: +255759859287