Na _Mwl. Oscar Samba_
4. Tafuta Ushauri Sahihi.
Hapo juu nimekupa mfano wa huyu baba ambaye alifikia mahali
pagumu sana kimaamuzi, ila mkewe alimshauri asimwache Mungu.
Badala yake waombe, nukuu moja wapo inamtaja au inamkariri huyu
baba akiwa anasema kuwa, Mungu amempa mke mzuri sana maana
alimshauri vyema!
Katika nyakati kama hizi ni muhim kujua umhimu wa namna ya
kukabiliana na shauri mbalimbali, maana wapo marafiki wataabishaji
ambao hawataacha kuja kwa nia ya kukuyumbisha kiushauri.
Kwenye fikra zako ni alzima kuwa na akiba ya hekima na maraifa ya
namna ya kukabilina na mamabo au amsuari au hali amahizi;
Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na
utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe.
Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao
wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa
Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu
hakufanya dhambi kwa midomo yake. Ayubu 2:9-10
Kuna watu wamejikuta wakikwama kwa sababu tu ya kutekeleza
ushauri mbovu. Wameoa na kuolewa nje ya mpango wa Mungu,
ameanguka ili tu wapate watoto. Maana mwenzake kapoteza uwezo wa
uzazi, ama ili tu apate kazi! Yaani kwake ni bora apate kazi lakini
ampoteze Yesu. Kwake mtoto ni wa thamani kuliko uhusiano wake na
Mngu! Najua ni pagumu ila lazima uwe tayari kuingia gharama yoyote
kwa ajili ya Kristo. Najua ni vigumu ila kumfuata Yesu kuna gharama
zake mpendwa! Na jaribu sio jaribu hadi limekuacha njia
panda; hadi ufikie hatua ya kuamua Yesu au Njia Nyingine
Ndipo Huwa Jaribu. Nje ya hapo ni Changamoto ya
Kawaida Tu! Ukiona umefikia hatua ya kuamua au eneo
ambalo unalopaswa kuamua aida Yesu au Njia ya Mkato,
uwe na hakika hapo sasa umefika kwenye jaribu!
Mtoto wa mfalme Sulemani alikwamishwa na ushari mbovu.
Alipotekeleza shauri la vijana ambalo lilikuwa baya, alijikuta anaugawa
ufalme alioachiwa na babaye! Sijui katika njia panda yako kama huwa
unajiombea ili uweze kutambua uwepo wa Mungu au roho nyingine
ama ubinadamu katika aina ya mashauri yanayokuzunguka!
Maana kipindi kama hiki adui hushambulia sana uwezo wako
wakufanya maamuzi! Na kadri mashauri yanavyozidi kuwa mengi
ndivyo na nafsi yako huwa katika mazingira magumu zaidi ya kumua.
Husasani kama mshauri hayo ni njia mbalimbali, maana hata waswahili
husema kuwa miluzi mingi humpoteza mbwa.
Maana anaitwa huku, anaitwa kule, hajui pa kuelekea! Ila mbwa makini
atatulia, na kukaa hapohapo au kando ya njia. Akitaka kujua ni ipi sauti
ya bwana wake, ni ipi sauti ya anayemtunza! Ni ipi sauti ya
anayemlindia nyumba yake! Na akiijua huifuta. Maana itakwepo, na
kama haipo atatatumbua bwana wangu sio miongoni mwa wanaoniita.
Kwa hiyo atatulia au ataendelea na pilika-pilika zake na hatafuata njia
ya sauti yoyote ile! Kujifunza kutaka kumjua Mungu, au kulitaka shauri
ama ushauri wake ni muhimu sana katika nyakati kama hizi.
Usipitwe na Ule Ujao Wenye Pointi ya TAFUTA MAPENZI YA MUNGU..
Yamkini Hujaokoka, na Unawiwa Moyoni Mwako Kufanya Vivyo... Tafadhali Fuatisha Pamoja Nami Sala Hii ya Toba..
Sema; MUNGU BABA, NINAKUJA MBELE ZAKO, MIMI NI MWENYE DHAMBI NAKUOMBA UNISAMEHE SASA; Amen.
Kipakue Bure Kitabu Hiki Google
Tafadhali Tafuta Kanisa la Watu Waliokoka Ukasali Hapo..
WhatApp, Tufolo; https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h
Kwa Maombi: +255759859287
http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Tumeunda Channel ya
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL
UWE NA AMANI
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni