Kuna Watu Ukiwaambia "Mimi ni Big Brain," Watakuuliza "Do You Have Any Article?" Na Wengine Watakutazama Umevaaje!
#Vijana Wengi Wameamua Kuwa Kundi la Pili.
By Mwalimu Oscar Samba
Kuna Watu Ukiwaambia "Mimi ni Big Brain," Watakuuliza "Do You Have Any Article?" Na Wengine Watakutazama Umevaaje!
#Vijana Wengi Wameamua Kuwa Kundi la Pili.
By Mwalimu Oscar Samba
Tatizo Kubwa la Viongozi wa Kiafrika Sio Kukosa Maono; Ni Kushindwa Kupandikiza Maono Kwa Watu Wanaowaongoza. Hawajui Hakuna Mkuu wa Jeshi Anayeshinda Vita Kutokana na Uwezo Wake Binafsi tu; Bali ni Kwa Sababu Amefanikiwa Kuandaa Jeshi Zuri. Ubora wa Kocha Unapimwa Kutokana na Uwezo Wake wa Kuandaa Timu Nzuri.
Ukifeli Kuwafanya Wafikiri Kama Wewe, Uwe na Hakika Watafikiri Kama Wao; Na Watatenda Kiholela.
By Mwalimu Oscar Samba
Gharama Moja Wapo ya Kulea Ni Kuvumilia, Kujifunza Kumchukulia na Kuchukuliana Huku Ukisalia Katika Lengo na Kusudi la Kutaka Chombo Unachokitaka.
Ni Hatari Kuhitaji Mtu Unayemtaka Awe Unayemtaka Kwa Dakika Moja. Jifunze kwa Fundi Muwashi au Mfinyazi wa Vyungu, Tazama Inavyochukuwa Muda Kukipata Anachokitaka!
Ghrama Kubwa ya Kulea Ipo Kwako Wewe na Sio kwa Anayelelewa; Ustaimilivu na Hekima Vitakusaidia.
Paulo Mtume Hakaanguka Juu ya Mti, Hakujilea...Alilelewa...Wakati Hanania Anasema ni Muuaji, Mungu Alimuona Kuwa Chombo Kiteule..
Unahitaji Jicho la Tatu ili Uweze Kuondokana na la Pili Linalomuona Sauli Muuaji; La Tatu Litamuona Chombo Kiteule.
John Marko Alionekana Hafai, Barnaba Alimuona Anafaa Katika Kipindi Ambacho Alikuwa Hafai.
Ni Muhimu Pia Kuwaheshimu Waliokuona Unafaa Katika Majira ya Ulipokuwa Hufai; Maana Sasa Kila Mtu Anakuona Unafaa kwa Saabu Unawafa; Fahamu Yupo Aliyelipa Gharama.
Ni Kweli Utukufu ni kwa Mungu. Lakini Kumbuka Alimtumia Barnaba Kumuandaa Sauli Aliye Paulo na John Marko.
NB: Tatizo la Sasa sio Wakina John Marko na Wakina Paulo Wanaotufaa Katika Utumishi; Ila Tatizo ni Kukosekana kwa Walezi Wenye Fikra za Ukocha...Walezi Wengi Wana Fikra za Ushindi, Yaani Wamtumie Nani ili Wafanikiwe na Sio Wamuandae Nani ili Wafanikishe Malengo yao. Asante:
"Ukishindwa Kulea, Ni Umeshindwa Kurithisha; Kwa Hiyo Jiandae Kusahaulika."
By Mwalimu Oscar Samba
www.ukombozigospel.blogspot.com
Nina *Mshukuru Mungu* kwa Kufanikiwa Kukamilisha Kitabu Changu Kipya cha Uchambuzi wa Kitabu cha Matendo ya Mitume. Kitabu kinaitwa SIRI YA *MAFANIKIO KWA KANISA LA KWANZA* ( *kanisa la Mitendo ya Mitume) By Mwl Oscar Prospa Samba mwana wa Flora Samba
Kipakiwe Bure Kitabu hiki Free Download Pdf
Bonyeza Hapa Mwalimu Oscar Samba SIRI YA MAFANIKIO KWA KANISA LA KWANZA (Kanisa la Matendo ya Mitume)
Felix Mbwanji:
SAMEHE NA KUSAHAU (BY MWL, C.MWAKASEGE)
TABIA YA MUNGU YA KUSAMEHE NDANI YAKO
Ulipompokea Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako, ulipokea tabia ya aina gani?
" Bali wote waliompokea (Kristo) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu." (Yohana 1:12,13)
Ulipozaliwa mara ya pili kwa Neno la Kristo ulifanyika kuwa mtoto wa Mungu.
Watoto wa Mungu wana tabia ya namna gani?
Kwa kuwa wamehamishwa toka ufalme mwingine na uzazi mwingine, na kuingizwa katika ufalme wa Mungu na uzazi wake (Wakolosai 1:13); watoto hawa wanatakiwa wawe na tabia nyingine.
Kabla ya kuzaliwa mara ya pili, kabla ya kumkiri Kristo ya kuwa ni Bwana: ulikuwa na tabia ya dunia hii iliyoongozwa na mfalme wa dunia hii ambaye ni shetani.
Ulipozaliwa mara ya pili na kuukiri wokovu katika Kristo, ulipokea tabia mpya inayoongozwa na Mungu mwenyewe aliye ndani yako.
" Kwa kuwa uwezo wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa (Utakatifu), kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe. Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno; za thamani,ili kwamba kwa hizo mpate kuwa Washirika wa TABIA YA UUNGU, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa." (2 Petro 1:3,4)
Na Christopher Mwakasege_
Leo nataka tujifunze juu ya “Mwongozo wa kutafakari na kuombea ndoto zenye UZINIFU AU UASHERATI ndani yake”.
Maneno haya ‘uzinifu na uasherati’ yanahusu ufanyikaji wa tendo la ndoa usio halali kibiblia. Uzinifu linatumika zaidi wakati tendo la ndoa limefanywa na mtu ambaye hajaoa au hajaolewa. ‘Uasherati’ linatumika zaidi wakati tendo la ndoa limefanywa nje ya ndoa na mtu ambaye ameoa au ameolewa.
Mtu anayepata ndoto zenye mambo hayo, huwa zina madhara makubwa sana ya kiroho, na ya kimwili – kwa aliyeota ndoto hizo!
Kumbuka kwamba: Neno la Mungu la biblia, kwa kushirikiana na Roho Mtakatifu, linatuongoza kujua namna ya kutafsiri na kuziombea ndoto za aina yo yote – ambazo ni pamoja na hizi zenye mambo ya uzinifu au uasherati ndani yake.
Mwl OSCAR SAMBA ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu: #Usiogope
Na Mwl. Oscar Samba
Kwenye Kipengele cha Faida za Uzima wa Milele
2. Tunakula Matunda ya Mti wa Uzima. Huu ni mti wa ajabu sana. Kumbuka mti huu ndio uliowafanya Adamu na mkewe kuondolewa kwenye bustani ya Edeni. Mimi na wewe leo hatupo hapo bustanini kwa sababu ya hii dhambi.
Mungu alihofia wasije wakala na kisha wakaishi milele.
Ufunuo wa Yohana 2:7 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu. (Nikutie moyo pia kuhakikisha unashinda vita, majaribu, maana mbingu ni mji wa washindi! Sio sehemu ya walioshindwa! Hili lijue na ulifikiri daima maana ni taswira halisi unayopaswa kuwa nayo kwenye fahamu zako.)
Tujione Siri hii muhimu kule Edeni:
Mwanzo 3:22 Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele; 23 kwa hiyo Bwana Mungu akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo katika hiyo alitwaliwa.
24 Basi akamfukuza huyo mtu, akaweka Makerubi, upande wa mashariki wa bustani ya Edeni, na upanga wa moto uliogeuka huko na huko, kuilinda njia ya mti wa uzima.
Kilichowafanya kuondolewa sio uzuri wa bustani! Sio kwamba wameshafanya dhambi kwa hiyo hawastaili tena kuendelea kula mema ya hiyo bustani, la! Bali ni kwa sababu ya uwepo wa huu mti. Ndiyo sababu kubwa Mungu anayoitoa anapowaondosha hapo.
Na Mwl Oscar Samba
#FaidayaJaribu: #Usiogope
Ni Sehemu ya Kitabu Chetu Tarajiwa cha MAANA YA UZIMA, NA UZIMA WA MILELE. Pwenti ya Pumziko Kuu.
Kwenye Kipengele cha Taswira ya Uzima wa Milele
Pumziko Kuu; Yaani Sabato Kukuu. Watu wengi hawajui ya kuwa Sabato maana yake ni pumziko katika kilele cha uzima wa milele yaani wakati huu hapa ulimwenguni kwa kuokoka, (kupumzika katika Kristo Yesu kama mtua mizigo ya dhambi na kila mateso.) Na pili kama sehemu ya kupumzika kutoka katika dunia iliyopo chini ya umiliki wa Shetani kama mungu wa dunia hii, na pamoja na dunia yenye pigo la laana la kosa la Adamu na Hawa.
Unapookoka ni umeingia katika Sabato. Kwa hiyo, msabato halisi ni mtu aliyeokoka. Kama hujaokoka wewe sio Msabato, maana bado upo chini ya utumwa wa Shetani. Wokovu unakupa pumziko. Kanuni na sheria zile za Agano la Kale hususani sabato na taratibu zake zote, zilinuia kutufikisha hapa kwenye wokovu na hatimaye katika Sabato kamilifu ile ya Mbingu Mpya na Nchi Mpya.
Ndiposa Yesu alipokuja, mkazo wa sheria za kisabato ule wa Agano la Kale haukwepo tena. Maana amekuja Sabato Mwenyewe. Ndio maana alijibu hivi; Marko 2:27 Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato. 28 Basi Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato pia. ( Kwa hiyo kama utaendelea kusingizia kumsikiliza mjumbe wa Sabato Musa na kumuacha Bwana wa Sabato; basi utakuwa umekwama sana.
Mathayo 12:5 Wala hamkusoma katika torati, kwamba siku ya sabato makuhani hekaluni huinajisi sabato wasipate hatia? 6 Lakini nawaambieni, kwamba hapa yupo aliye mkuu kuliko hekalu.
7 Lakini kama mngalijua maana yake maneno haya, Nataka rehema, wala si sadaka, msingaliwalaumu wasio na hatia. 8 Kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.
Tuone kisa kingine:
Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )
Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )
Waebrania 5:12 Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu.
:13 Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga.
:14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya.
Kama Nilivyokuhaidia Jana, ni Kwamba Aina ya Chakula Unachokula Ndicho Kinachoamuwa kama Uendelee kuwa Mwanafunzi au Mwalimu. Na kwa mujibu wa Jana Washindi Wana Aina Yao ya Vyakula, (Mana Iliyofichwa.)
http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/Mafun
Neno la Leo ( #NasahazaMwlOscar )
#FaidayaJaribu:
Wafilipi 4:8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.
:9 Mambo mliyojifunza kwangu na kuyapokea, na kuyasikia na kuyaona kwangu, yatendeni hayo; na Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
:10 Nalifurahi sana katika Bwana, kwa kuwa sasa mwisho mmehuisha tena fikira zenu kwa ajili yangu, kama vile mlivyokuwa mkinifikiri hali yangu lakini hamkupata nafasi.
:19 Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.
(Baraka Hizi za Paulo Zinakuja Baada ya Hawa Watu Kusimama Kwenye Nafasi Yao)
http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Faida ya Jaribu :
Waebrania 12:3 Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu.
:4 Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi;
Tunapewa Nasaha za Kumtazama Yesu Aliyestahimili Mambo Magumu kwa Ajili Yetu, Hata Akautoa Uhai wake..Mimi Na wewe Hatujafikia Kipimo Hicho cha Kuimwaga Damu...Nasi Hatuna Budi Kuyastahimili kama Yeye Alivyofanya kwa Ajili Yetu..Nasi Tufanye kwa Ajili Yake..
http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Kwa Maombi +255759859287
Nikutakie Siku Njema