Umenza tarehe 19 hadi 23 (jumatano hadi jumapili) 2023
Ujumbe: UFALME WA MBINGUNI UMEKARBIA. Mathayo 3:2
Umenza tarehe 19 hadi 23 (jumatano hadi jumapili) 2023
Ujumbe: UFALME WA MBINGUNI UMEKARBIA. Mathayo 3:2
Ujumbe wa Mkutano huu ulikuwa ni UPENDO WA MUNGU KWA MWANADAMU
Tukuongozwa na Andiko la Yohana 3:16.
Tazama Baadhi ya Picha za Matukio
![]() |
| Picha hii na Zifanazo na hii ni Watu Waliotoka kwa Ajili ya Kuokoka na Maombezi |
![]() |
| Picha hii na hiyo tangulizi hapo juu ni Waimbaji wakiimba Wimbo wa Kichaga na Kucheza "Iriingi". |
Naomba NiRepost
#VIJANA_NISIKILIZENI_Haya_Nayo_Ni_Maneno_ya_Mwenye_Hekima
Moyo Unaweza Kumpenda Mtu Bila Kuwa na Sababu Yoyote ya Msingi ila Usikubali Kuoana na Mtu Asiyetosheleza Vigezo Vya Ndoa kwa Viwango Fulani.
Moyo wa mwanadamu kuna muda unavutiwa na mtu bila hata kukupa sababu zenye mashiko kwanini umempenda. Utamsikia mtu akisema basi nimepanda tu! Ni kweli ni jambo jema, na hatuwezi kuweka sababu kwa kila mtu au maamuzi ya moyo kupenda.
Ndiposa wengine wakasema mapenzi ni upofu, ikiwa na maana kwamba kuna mambo ya msingi mtu anaweza kuya_overloock ama kuyapuuza ifikapo swala la kupenda. Hapa napo sina shinda napo.
Ila msemo huu ndio unaonipa shida; kipendacho roho hula nyama mbichi! Ndugu yangu, nyama mbichi huvimbisha matumbo, huleta kuharisha sanjari na hatari ya magonjwa ya minyoo.
Na Mwalimu Oscar Samba
Ujumbe huu ni Sehemu ya #Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO MZITO AMBAPO MUNGU, BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA. Tunaendelea kidogo plae tulipoishia katika Makala iliyopita, kisha ttutatazama jambo la Kwanza; Karibu:
Ikifika mahali ukiona msisitizo uliopo ndani yako sio kumtwisha tu Mungu mzigo wako, sio Mungu tu kukutia nguvu. Bali swali lako ni kwamba sawa nitavumilia, ila Mungu atanijibu lini? Uwe na hakika kuwa unahitaji msaada mkubwa zaidi.
Maana kuna mambo mawili hapo. Mosi ni la kuchoka na pili ni la kuhoji uaminifu wa Mungu kwamo?
Kwamba huna shaka, hata sasa ukimuita akutie nguvu anweza, ila hoja ni kamba huu ni mwaka wa tano sasa, kumi au miaka naho inaenda, unakaribia 40 na hata 50 sasa ila bado hajakutokea. Ndio maana ukinielewa hapa hutaacha kuyaelewa maandiknya Zabuti kuhusu uaminifu. MUNGUkuna.mahali unasoma na unaona jinsi mtunga Zabuti anavyopitia sehemu ngumu, kisha anataja uaminifu wa Mungu.
KANUNI
1. Fahamu ni Kwanini Mungu Anataka Bado Uendelee Kuubeba au Uendelee Kupitia. Waliowahi kusoma kitabu kile cha Isaya 55 utabaini kuwa watu wale kuna namna walikuwa wamepishana na mipango ya Mungu maishani mwao. Ndio maana Mungu anafika hatua ya kuwaambia kuwa mawazo yenu sio mawazo yangu, wala njia zenu sio njia zangu. Anawapa na kipimo husika, kwamba kama vile mbingu zilivyo mbali na aridhi; ndivyo mimi nanyi tunavyopishana.
Najua unajua kuwa Mungu ana akili kuliko wewe. Ufahamu wake ni mkubwa kukuzidi. (Ikupe kujiuliza kwa nini kakuacha.) Na kubwa zaidi ni kwamba anakupenda kuliko unavyo mpenda. Na kile kitabu chetu cha MUONE MUNGU NYUMA YA PITO LAKO kinafunza kiunagaubaga kuhusu kusudi la Mungu kukupitisha hapo.
Neno la Leo
Zaburi 90:12 Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima.
Psalms 90:12 NIV
[12] Teach us to number our days, that we may gain a heart of wisdom.
Yawe ni Maombi yako, Omba Hekima; Bali Omba Akugundishe Kuzihesabu Siku ili Uweze Kuwa na hiyo Hekima
Uvumilivu na Kuwa Mtu wa Kujifunza kila Uchwao ni Miongoni Mwa Maana ya Kuzihesabu Siku...
Tembelea pia www.ukombozihospel.blogspot.com
![]() |
| Kulia ni Mchungaji Maziko wa Kanisa la PSMA Kitasha Rombo (Mch Mwenyeji) akishika na mkono na Mwl Oscar Samba ikiwa ni Ishara ya kumkaribisha ili shubiri. |
![]() |
| Pichani ni Mwl Oscar Samba akihubiri |
Ndivyo Tulivyo Anza Jana #Kitasha hapa PSMA
Ujumbe unaitwa: KWA NINI SWALA LA UWOKOVU NI LA MUHIMU . Luka 19:10 Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.
Kama ukijua huu umuhimu, ni dhahiri utakubali kuokoka maana Yesu alikuja kutafuta wewe ambaye bado hujaokoka.
Na Yamkini haujaokoka, nawe umeguswa na ujumbe huu na unatamani kuokoka (kumbuka wokovu maana yake ni kumkataa Shetani na mateso yake, dhambi na taabu zake na kumkubali Yesu na Uzima ama mbingu)...
Kama ndivyo basi nikutie moyo kufuatisha Sala hii ya Toba kwa imani, Sema; EWE MUNGU BABA, MIMI NI MWENYE DHAMBI, NIMEGUNDUA MAKOSA YANGU, NISAMEHE YESU, FUTA MAJINA YANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, NIANDIKE KWENYE KITABU CHA UZIMA WA MILELE, Amen.
Hongera kwa Kuokoka na tafadhali tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo, Ameni.
... Zaidi tembelea
www.ukombozigospel.blogspot.com
Tazama na Sikiliza Mahubiri na Mafundisho Yetu hapa, Usisahau Ku-Subcribe ili uyapate kwa haraka zaidi; https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv
Jiunge nasi pia kwenye WhatsApp group letu la mafundisho ya neno la hapa: https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Kundi letu la Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk (Hapa utapata Mahubiri/Mafundisho Yetu kwa Haraka)
Namba ya Telegram au Mawasiliano: +255759859287 inatumika pia kwenye WhatsApp na M-Pesa. Ukiguswa kuachilia Sadaka yako tafadhali usisite kufanya hivyo. Jina ni Oscar Samba.
Usisite Kututembelea pia kwenye Ukurasa (Page) wa Facebook na "Ku-like" https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL
Ama tuandikie email (Baruapepe) ukombozigospel.@gmail.com
tupo kwenye mkutano wa 18
18. Kitasha Kakfua (Chekechea)
Unaendelea 23-27/11/2022
19. Kitasha; Shule ya Msingi Roya,
(umeandaliwa na Kanisa la PSMA)
30/Nov -3/Dec /2022
20. Ubaa, Ushiri. 7-10/12/2022
21. Mamsera Sokoni. 14-17/12/2022
22. Kinyauli, Kerio Mashati. 2-7/1/2022
Ni Rombo Klnjaro. Na Mwl. O. Samba
Na Mwalimu Oscar Samba
Utangulizi
Hakuna eneo muhinu linalompatia Mungu utukufu kama matokeo ya wewe kushinda vita. Jaribu kufikiria Mungu angejisikiaje kama ujasiri huu aliokuwa nao kuhusu Ayubu kama usingalitimia! Ayubu 2:3 Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu?
Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, ujapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu.
Najitoa moyo kurudia tena sifa tajwa hapo juu; na miongoni mwa maneno yaliyonigusa kiupekee nje ya hizo sifa ni hili hapa: ambapo nakiri kiuhakik kwamba japo nimekuwa nikikisoma kitabu hiki mara kwa mara lakini bado sikuwahi kukutana na jambo hili katika sura hii. Ya kwamba Shetani kumbe aliwahi kujaribu kumshawishi Mungu amuangamize Ayubu! Ona hili katika kipengele cha mwisho cha hilo andiko hapo juu; "...ujapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu."
Sasa katika mtu kama huyu, jaribu kufikiria mbinguni kungekuwa na msiba mkubwa kiasi gani kama Ayubu angemuangusha Mungu kwenye jaribu au pito lake? Shetani hapana shaka angalimrejelea Mungu na kumwambia kwamba ni bora tu ungalimwangamiza mapema kama nilivyokushauri pale awali.
Uvumilivu wa Ayubu ulimpatia Mungu heshima. Na wewe kuvumilia kwako kutakupatia heshima vivyo. Hakikisha unavumilia, ili Mungu aweze kukushindia pia. Usikubali kukwama kwenye pito lako, bali hakikisha unavumilia na hatimae kushinda.
Lengo kuu la kitabu hiki ni kukuwezesha kuwa na fikra na morali wa ushindi ili kumpatia Mungu heshima. Naye alishasema kuwa akiinuliwa, atawavuta wote kuja kwake. Hii inatupa kufahamu kuwa Mungu akiinuliwa na aliyelibeba jina lake naye anainuliwa. Huduma itapokea kibali maana watu watavutwa kuja kwake, na aliyelibeba jina lake anainuka na jina lililoinuliwa.
Heshima inakuja mwishoni, sio mwanzoni, mwanzoni ni kudharauliwa na kubezwa, kama ilivyokuwa kwa Ayubu, ni majira ya kuzingirwa na marafiki wataabishaji. Sio majira mazuri bali ni magunu, hakuna anayekuelewa. Ila ukishinda ndipo heshima huja. Kama ilivyokuwa kwa Ayubu, mwisho wake ulijawa na utukufu kiasi cha adui zake kuishilia kwenye matengenezo.
Kwa Meshaki, Shedraka, na Aberinego sanjari na Danieli ndivyo ilivyokuwa, waliinuliwa mara dufu mara baada ya ushindi wao. Na kwako inawezekana kama tu utaamua kumtazama Mungu kwa sura tajwa humu kitahuni. Karibu na Mungu akupe kuyaelewa haha:
Tafadhali Kitabu kikitoka kinunuwe.. zaidi tembelea
www.ukombozigospel.blogspot.com
Jiunge nasi pia kwenye WhatsApp group letu la mafundisho ya neno la hapa: https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Kundi letu la Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Namba ya Telegram au Mawasiliano: +255759859287
Pichani ni Mwalimu Oscar Samba (aliyepo katikati kwenye picha ya Kwanza) akiongoza kikosi kazi cha Wanainjili wakiwa katika maandalizi ya mkutano kwa kufunga Jukwaa.
Mkutano huo ulianza hivi leo katika viwanja vya Kwarogati vilivyopo Shimbi Mashami. Ikiwa ni mfululizo wa mikutano 12 aliyonayo hadi kufikia mwezi wa tisa mwaka huu. Huu ni mkutano wa tatu ukitanguliwa na miwili iliyofanyika shuleni kwaikuru Sekondari juma lilopita na ule wa Shuleni Kwasondo uliotangulia.
Ujumbe: KUU NA UWEZA WA YESU JINSI ULIVYO Waefeso 1:18-23. (Kwa Rogati)
Ujumbe wa Kwasondo :MUNGU, MUNGU ANAYESAMEHE MAKOSA Isaya 43:25
Na Kwaikuru ni : HATIMA YA MAISHA YAKO Yohana 14:3