Jumatano, 22 Februari 2023

Fahamu ni Sababu za Mungu Kukutaka Uendelee Kuvumilia hilo Pito au Jaribu

 

Na Mwalimu Oscar Samba
Ujumbe huu ni Sehemu ya #Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO MZITO AMBAPO MUNGU, BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA. Tunaendelea kidogo plae tulipoishia katika Makala iliyopita, kisha ttutatazama jambo la Kwanza; Karibu:

Ikifika mahali ukiona msisitizo uliopo ndani yako sio kumtwisha tu Mungu mzigo wako, sio Mungu tu kukutia nguvu. Bali swali lako ni kwamba sawa nitavumilia, ila Mungu atanijibu lini? Uwe na hakika kuwa unahitaji msaada mkubwa zaidi.


Maana kuna mambo mawili hapo. Mosi ni la kuchoka na pili ni la kuhoji uaminifu wa Mungu kwamo?

Kwamba huna shaka, hata sasa ukimuita akutie nguvu anweza, ila hoja ni kamba huu ni mwaka wa tano sasa, kumi au miaka naho inaenda, unakaribia 40 na hata 50 sasa ila bado hajakutokea. Ndio maana ukinielewa hapa hutaacha kuyaelewa maandiknya Zabuti kuhusu uaminifu. MUNGUkuna.mahali unasoma na unaona jinsi mtunga Zabuti anavyopitia sehemu ngumu, kisha anataja uaminifu wa Mungu.

KANUNI
1. Fahamu ni Kwanini Mungu Anataka Bado Uendelee Kuubeba au Uendelee Kupitia. Waliowahi kusoma kitabu kile cha Isaya 55 utabaini kuwa watu wale kuna namna walikuwa wamepishana na mipango ya Mungu maishani mwao. Ndio maana Mungu anafika hatua ya kuwaambia kuwa mawazo yenu sio mawazo yangu, wala njia zenu sio njia zangu. Anawapa na kipimo husika, kwamba kama vile mbingu zilivyo mbali na aridhi; ndivyo mimi nanyi tunavyopishana.

Najua unajua kuwa Mungu ana akili kuliko wewe. Ufahamu wake ni mkubwa kukuzidi. (Ikupe kujiuliza kwa nini kakuacha.) Na kubwa zaidi ni kwamba anakupenda kuliko unavyo mpenda. Na kile kitabu chetu cha MUONE MUNGU NYUMA YA PITO LAKO kinafunza kiunagaubaga kuhusu kusudi la Mungu kukupitisha hapo.

Jumamosi, 18 Februari 2023

NENO LA LEO Zaburi 90:12

 Neno la Leo


Zaburi 90:12 Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima.



‭‭Psalms‬ ‭90:12‬ ‭NIV‬‬

[12] Teach us to number our days, that we may gain a heart of wisdom.


Yawe ni Maombi yako, Omba Hekima; Bali Omba Akugundishe Kuzihesabu Siku ili Uweze Kuwa na hiyo Hekima


Uvumilivu na Kuwa Mtu wa Kujifunza kila Uchwao ni Miongoni Mwa Maana ya Kuzihesabu Siku...


Tembelea pia www.ukombozihospel.blogspot.com

Jumanne, 14 Februari 2023

kitabu chetu cha: CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO MZITO AMBAPO MUNGU, BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA.

Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu chetu cha: CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO MZITO AMBAPO MUNGU, BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA.

Hiki sii kitabu cha kawaida wala si somo tu bali ni ujumbe. Najua kila ujumbe ni somo katika mukutadha wa mafundisho na ufundishaji. Japo sio kila somo ni ujumbe.

Ujumbe huu ni matokeo ya mahali ninapopapitia ambapo mwaka jana palinipatia vitabu kama viwili hivi. Mosi ni kile cha  HAKUFANYA UNAPOKUWA NJIA PANDA. Na pili ni kile cha MUONE MUNGU NYUMA YA PITO LAKO.

Kwa lugha nyingine unaweza kusema kuwa sii jumbe za kawaida. Bali ni maelekezo. Mfano wa ujumbe kibiblia ni pale mfalme Nebukaddeza alipoota ile ndoto na kisha kujikuta hana tafsiri yake na kuomba msaada kwa Danieli nabii wa Mungu. Tukiachana na yote pale, yale maneno, "Danieli 4:27 Kwa sababu hiyo, Ee mfalme, shauri langu lipate kibali kwako; ukaache dhambi zako kwa kutenda haki, ukaache maovu yako kwa kuwahurumia maskini; huenda ukapata kuzidishiwa siku zako za kukaa raha."


Kwa hiyo, kama Mungu amekupa kukisoma kitabu hiki, moja kwa moja fikra zako zielekeze kwenye ujumbe uliopo ndani yake. Ambao unanuia kumsaidia kwa kumpa mtu husika maelekezo muhimu ya kufanya ili kuendelea mbele na pito au jaribu analolipitia.

Ni matoke ya mimi katika jana ya leo, baada ya kuzungumza na kiongozi wangu mmoja juu ya pito ninalolipitia na majibu ya Mungu juu yangu. Majibu hayo yalinitaka niendelee kuvumilia. Na aliniambia hadi nimalize masomo. Nikauliza je nikimaliza Mungu ndo atanijibu?

Akaniambia hata yeye hajui kama atanijibu au la, ila alichoambiwa ni kwamba kwa wakati huu usijaribu kubeba mambo mawili. Kwa mujibu wa mukutadha wa hekima ile ni kwamba inaonekana maamuzi yangu dhidi ya pito husika nyuma yake hayana mapenzi makamilifu ya Mungu. 

Jumatatu, 2 Januari 2023

Rombo

#Mkutano #Mkutano #Mkutano Wiki hii; 4-8/1/2023 Katika Viwanja vya Zambia, Mengeni Chini Rombo . Muhubiri: Mwalimu Oscar Samba Walete wagonjwa na wenye mateso mbalimbali na Yesu Mtenda miujiza Atawaponya. Karibu Umsikie Mungu Akisema na Maisha Yako. Tafadhali watakatifu na Wengine

Ijumaa, 16 Desemba 2022

Mngoje Bwana kwa Saburi

rr*MNGOJE BWANA KWA UVUMILIVU* Zaburi 40:1 Nalimngoja Bwana kwa saburi, Akaniinamia akakisikia kilio changu. (Anatuambia kuwa alimnyonga Bwana kwa saburi naye akamuinamia! Kumuinamia maana yake ni kumsikiliza, ni kuweka umakini katika kumsikiliza. Kumuinamia ni sawa na mtu mrefu anapoongeleswa na mfupi, au mtu mzima kwa mtoto mdogo hulazimika kuinama kidogo ili sikio lake lifikile kimo cha kinywa chake.) Endelea na maandiko mengine kisha nitakujuza ninalotamani kukufahamisha hapa: "kichwani weka neno Saburi akiba" :2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu. :3 Akatia wimbo mpya kinywani mwangu, Ndio sifa zake Mungu wetu. Wengi wataona na kuogopa, Nao watamtumaini Bwana :4 Heri aliyemfanya Bwana kuwa tumaini lake, Wala hakuwaelekea wenye kiburi, Wala hao wanaogeukia uongo. Heri aliyemfanya Bwana kuwa tumaini lake! Neno tumaini jumlisha na saburi. Natumai unakumbuka kuwa nilikutaka kuweka akiba akilini neno "Saburi"! Katika mstari ule anatuambia kuwa alimngoja Bwana kwa saburi naye akamuinamia. Yaani anamshinikiza ama kumjibu. Nataka uone neno kumngoja Bwana..kisha neno kwa linatupa kufahamu ni njia ipi au kanuni ipi ilitumika hapa...ni saburi.. Saburi ni nini basi? ... Saburi ni aina ya uvumilivu ambao ndani yake una unyenyekevu, utulivu, amani ya Roho ni pamoja na tumaini katika Bwana kuwa siku moja atamjibu. Nataka kukwambia nini? Haijalishi unapitia mahali pagumu kiasi gani, wewe jifunze kumngoja Bwana kwa saburi..uwe na uvumilivu ambao ndani yake umebeba tumaini thabiti kuwa ipo siku Mungu atakujibu...haijalishi leo kuna ukimya mgumu kiasi gani ila siku moja najua yaja nitajibiwa tu. Nikutie moyo kuwa mngoje Bwana kwa saburi naye atakujibu tu....siku moja yaja, nawe utapokea majibu yako. Na Yamkini haujaokoka, nawe umeguswa na ujumbe huu na unatamani kuokoka (kumbuka wokovu maana yake ni kumkataa Shetani na mateso yake, dhambi na taabu zake na kumkubali Yesu na Uzima ama mbingu)... Kama ndivyo basi nikutie moyo kufuatisha Sala hii ya Toba kwa imani, Sema; EWE MUNGU BABA, MIMI NI MWENYE DHAMBI, NIMEGUNDUA MAKOSA YANGU, NISAMEHE YESU, FUTA MAJINA YANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, NIANDIKE KWENYE KITABU CHA UZIMA WA MILELE, Amen. Hongera kwa Kuokoka na tafadhali tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo, Ameni. ... Zaidi tembelea www.ukombozigospel.blogspot.com Tazama na Sikiliza Mahubiri na Mafundisho Yetu hapa, Usisahau Ku-Subcribe ili uyapate kwa haraka zaidi; https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv Jiunge nasi pia kwenye WhatsApp group letu la mafundisho ya neno la hapa: https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD Kundi letu la Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk (Hapa utapata Mahubiri/Mafundisho Yetu kwa Haraka) Namba ya Telegram au Mawasiliano: +255759859287 inatumika pia kwenye WhatsApp na M-Pesa. Ukiguswa kuachilia Sadaka yako tafadhali usisite kufanya hivyo. Jina ni Oscar Samba. Usisite Kututembelea pia kwenye Ukurasa (Page) wa Facebook na "Ku-like" https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL Ama tuandikie email (Baruapepe) ukombozigospel.@gmail.com

Jumanne, 13 Desemba 2022

Bibi Kikongwe katika Mkutano wa Injili

Huyu Bibi Alinifuraisha na kunitia Moyo sana, Aliudhuria mkutano wangu wote wa Ubaa Posta ya Zamani au Mahakama ya Mwanzo Rombo siku zote. Alikuwa anakaa migombani na kiti chake. Siku nyingine namkuta kashanitangulia. Siku moja akaniambia kwamba yale maneno niliyoyasema, (kuyahubiri) ameyasikia na atayafanyia kazi! Katika stori niligundua pia anakumbukumbu sana maana anakumbuka hadi tarehe ya Arusi yake. Alisema ni 1957, Mwezi wa 2 tarehe 22. Kwangu huyu ni hazina. Nilimuhaidi kumtembelea siku moja (japo naye alinialika nyumba) ili kufahamiana zaidi. Kwangu hii ni furaha moja wapo inayonifanya kuhubiri. Maana hadi vikongwe nao wanamkimbilia Yesu.

Alhamisi, 8 Desemba 2022

Mkutano Ubaa Posta ya Zamani au Mahakama ya Mwanzo Rombo

Jana Ndivyo Tulivyoanza Mkutano wetu wa 20 hapa Ubaa Posta ya Zamani au Mahakama ya Mwanzo Rombo. Hakika Sijawahi kuona mkutano wenye mwitikio mkubwa km huu! Watu wa Ubaa Hongereni. Nitajitahidi kuhifadhi matukio vyema km nitajaliwa. #Pia_tafadhali_Endelea_Kutuombea

Jumapili, 4 Desemba 2022

Mabadiliko Machache RATIBA ZA MIKUTANO YETU (iliyosalia)

Hadi sasa tangu mwezi wa 7/2022 tupo kwenye mkutano wa 19 18. Kitasha Kakfua (Chekechea) 23-27/11/2022 19. Kitasha; Shule ya Msingi Roya, (umeandaliwa na Kanisa la PSMA) 30/Nov -4/Dec /2022 20. Ubaa, Ushiri. 7-11/12/2022 21. Sio Makalema tena, (badala ya Yamerejea Mamsera ktk Kanisa la Kingdom kwa Mch Daniel.) 14-18/12/2022 22. Himo, 21-25/12/2022 (Moshi Vjjn) 23. Kinyauli, Kerio Mashati. 2-8/1/2022 Mingine Rombo Klnjaro. Na Mwl. O. Samba

Neno la Leo Jumapili

Neno la Leo
Zaburi 127:5 Heri mtu yule Aliyelijaza podo lake hivyo. Naam, hawataona aibu Wanaposema na adui langoni. Maana yake Heri au Amebarikiwa mtu yule ambaye podo lake limewekwa mishale kwa ajili ya vita ama silaha Hataogopa adui zake inapofika majira ya msimu mpya (langoni) au anapohitahi mpenyo fulani au kuvuka ktk eneo fulani

Alhamisi, 1 Desemba 2022

Habari Picha za Mkutano Kitasha Rombo

Kulia ni Mchungaji Maziko wa Kanisa la PSMA Kitasha Rombo (Mch Mwenyeji) akishika na mkono na Mwl Oscar Samba ikiwa ni Ishara ya kumkaribisha ili shubiri.



Na Picha tatu zilizotangulia ni waudhuriaji wa mkutano huo
Pichani ni Mwl Oscar Samba akihubiri



 

Ndivyo Tulivyo Anza Jana #Kitasha hapa PSMA

Ujumbe unaitwa: KWA NINI SWALA LA UWOKOVU NI LA MUHIMU . Luka 19:10 Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.

Kama ukijua huu umuhimu, ni dhahiri utakubali kuokoka maana Yesu alikuja kutafuta wewe ambaye bado hujaokoka.

Na Yamkini haujaokoka, nawe umeguswa na ujumbe huu na unatamani kuokoka (kumbuka wokovu maana yake ni kumkataa Shetani na mateso yake, dhambi na taabu zake na kumkubali Yesu na Uzima ama mbingu)...
Kama ndivyo basi nikutie moyo kufuatisha Sala hii ya Toba kwa imani, Sema; EWE MUNGU BABA, MIMI NI MWENYE DHAMBI, NIMEGUNDUA MAKOSA YANGU, NISAMEHE YESU, FUTA MAJINA YANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, NIANDIKE KWENYE KITABU CHA UZIMA WA MILELE, Amen.
Hongera kwa Kuokoka na tafadhali tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo, Ameni.
... Zaidi tembelea
www.ukombozigospel.blogspot.com
Tazama na Sikiliza Mahubiri na Mafundisho Yetu hapa, Usisahau Ku-Subcribe ili uyapate kwa haraka zaidi; https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv

Jiunge nasi pia kwenye WhatsApp group letu la mafundisho ya neno la hapa: https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Kundi letu la Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk (Hapa utapata Mahubiri/Mafundisho Yetu kwa Haraka)

Namba ya Telegram au Mawasiliano: +255759859287 inatumika pia kwenye WhatsApp na M-Pesa. Ukiguswa kuachilia Sadaka yako tafadhali usisite kufanya hivyo. Jina ni Oscar Samba.
Usisite Kututembelea pia kwenye Ukurasa (Page) wa Facebook na "Ku-like" https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL
Ama tuandikie email (Baruapepe) ukombozigospel.@gmail.com

Jumatatu, 28 Novemba 2022

NENO LA LEO



Warumi 5:3 Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi;

:4 na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini;

:5 na tumaini halitahayarishi; kwa maana pendo la Mungu limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Mtakatifu tuliyepewa sisi.

:6 Kwa maana hapo tulipokuwa hatuna nguvu, wakati ulipotimia, Kristo alikufa kwa ajili ya waovu.

 .. Zaidi tembelea
www.ukombozigospel.blogspot.com

Jiunge nasi pia kwenye WhatsApp group letu la mafundisho ya neno la hapa: https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Kundi letu la Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk (Hapa utapata Mahubiri/Mafundisho Yetu kwa Haraka)

Namba ya Telegram au Mawasiliano: +255759859287 inatumika pia kwenye WhatsApp na M-Pesa. Ukiguswa kuachilia Sadaka yako tafadhali usisite kufanya hivyo. Jina ni Oscar Samba.

Jumapili, 27 Novemba 2022

RATIBA ZA MIKUTANO YETU (iliyosalia)



Hadi sasa tangu mwezi wa 7/2022

 tupo kwenye mkutano wa 18

18. Kitasha Kakfua (Chekechea) 

Unaendelea  23-27/11/2022

19. Kitasha; Shule ya Msingi Roya, 

(umeandaliwa na Kanisa la PSMA)

30/Nov -3/Dec /2022

20. Ubaa, Ushiri. 7-10/12/2022

21. Mamsera Sokoni. 14-17/12/2022

22. Kinyauli, Kerio Mashati. 2-7/1/2022

Ni Rombo Klnjaro. Na Mwl. O. Samba


Alhamisi, 24 Novemba 2022

Bunner au Bango letu Jipya la Huduma ya Ukombozi Gospel iliyopo chini ya Mwalimu Oscar Samba


 

Utangulizi wa #Kitabu chetu cha VUMILIA WAMJUE MUNGU WAKO

Na Mwalimu Oscar Samba

Utangulizi

Hakuna eneo muhinu linalompatia Mungu utukufu kama matokeo ya wewe kushinda vita. Jaribu kufikiria Mungu angejisikiaje kama ujasiri huu aliokuwa nao kuhusu Ayubu kama usingalitimia! Ayubu 2:3 Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu?

 Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, ujapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu.

Najitoa moyo kurudia tena sifa tajwa hapo juu; na miongoni mwa maneno yaliyonigusa kiupekee nje ya hizo sifa ni hili hapa: ambapo nakiri kiuhakik kwamba japo nimekuwa nikikisoma kitabu hiki mara kwa mara lakini bado sikuwahi kukutana na jambo hili katika sura hii. Ya kwamba Shetani kumbe aliwahi kujaribu kumshawishi Mungu amuangamize Ayubu! Ona hili katika kipengele cha mwisho cha hilo andiko hapo juu; "...ujapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu."

Sasa katika mtu kama huyu, jaribu kufikiria mbinguni kungekuwa na msiba mkubwa kiasi gani kama Ayubu angemuangusha Mungu kwenye jaribu au pito lake? Shetani hapana shaka angalimrejelea Mungu na kumwambia kwamba ni bora tu ungalimwangamiza mapema kama nilivyokushauri pale awali.

Uvumilivu wa Ayubu ulimpatia Mungu heshima. Na wewe kuvumilia kwako kutakupatia heshima vivyo. Hakikisha unavumilia, ili Mungu aweze kukushindia pia. Usikubali kukwama kwenye pito lako, bali hakikisha unavumilia na hatimae kushinda.

Lengo kuu la kitabu hiki ni kukuwezesha kuwa na fikra na morali wa ushindi ili kumpatia Mungu heshima. Naye alishasema kuwa akiinuliwa, atawavuta wote kuja kwake. Hii inatupa kufahamu kuwa Mungu akiinuliwa na aliyelibeba jina lake naye anainuliwa. Huduma itapokea kibali maana watu watavutwa kuja kwake, na aliyelibeba jina lake anainuka na jina lililoinuliwa.

Heshima inakuja mwishoni, sio mwanzoni, mwanzoni ni kudharauliwa na kubezwa, kama ilivyokuwa kwa Ayubu, ni majira ya kuzingirwa na marafiki wataabishaji. Sio majira mazuri bali ni magunu, hakuna anayekuelewa. Ila ukishinda ndipo heshima huja. Kama ilivyokuwa kwa Ayubu, mwisho wake ulijawa na utukufu kiasi cha adui zake kuishilia kwenye matengenezo.

Kwa Meshaki, Shedraka, na Aberinego sanjari na Danieli ndivyo ilivyokuwa, waliinuliwa mara dufu mara baada ya ushindi wao. Na kwako inawezekana kama tu utaamua kumtazama Mungu kwa sura tajwa humu kitahuni. Karibu na Mungu akupe kuyaelewa haha:

Tafadhali Kitabu kikitoka  kinunuwe.. zaidi tembelea

www.ukombozigospel.blogspot.com

Jiunge nasi pia kwenye WhatsApp group letu la mafundisho ya neno la hapa: https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD


Kundi letu la Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk


Namba ya Telegram au Mawasiliano: +255759859287

Jumanne, 21 Juni 2022

Mwalimu Katika Maandalizi ya Mkutano


Pichani ni Mwalimu Oscar Samba (aliyepo katikati kwenye picha ya Kwanza) akiongoza kikosi kazi cha Wanainjili wakiwa katika maandalizi ya mkutano kwa kufunga Jukwaa.


Mkutano huo ulianza hivi leo katika viwanja vya Kwarogati vilivyopo Shimbi Mashami. Ikiwa ni mfululizo wa mikutano 12 aliyonayo hadi kufikia mwezi wa tisa mwaka huu. Huu ni mkutano wa tatu ukitanguliwa na miwili iliyofanyika shuleni kwaikuru Sekondari juma lilopita na ule wa Shuleni Kwasondo uliotangulia.

Ujumbe: KUU NA UWEZA WA YESU JINSI ULIVYO Waefeso 1:18-23. (Kwa Rogati)

Ujumbe wa Kwasondo :MUNGU, MUNGU ANAYESAMEHE MAKOSA Isaya 43:25

Na Kwaikuru ni : HATIMA YA MAISHA YAKO Yohana 14:3

Jumamosi, 11 Juni 2022

TARATIBA ZA MIKUTANO YETU YA INJILI Shimbi, Maharo Makiidi, Mokala, na Ushirikiano Mkuu Rombo

 Kata ya Shimbi

1. Shuleni KwaSondo 11-24 June 2022

2. Shuleni Kwaikuru 15-19 June 2022

3. Kwa Rogati 22-28 June 2022 

Majira ya 10:30 Jioni 


Jumapili, 24 Aprili 2022

NI KWA NINI MUNGU ANAKUTAKA UMKABITHI NJIA ZAKO

Na Mwalimu Oscar Samba (Tafadhali #Share na kwa wengine ili nao Wanufaike)

Utangulizi wa kitabu chetu cha NI KWA NINI MUNGU ANAKUTAKA UMKABITHI NJIA ZAKO

Nilifanikiwa kuzungumza na mtu mmoja aliyeokoka ambaye Mungu amebariki kiuchumi, naye alinipa maneno magumu ambayo yalinifanya kufikiri sana. Aliniambia kuwa alisikia msukumo wa kunipigia simu na gafula akijikuta akiniuliza maswali kadhaa kuhusu mipango yangu ya kihuduma na kieleimu. 

Kisha alinipa maneno ambayo yalinifanya kufikiri sana na kuona hapa kuna kitu ambacho walimu wengi wa somo la maono hatukitendei haki. Aliniambi; Kuwa na maono sio kazi, Mungu anaweza kukupa maono, hata wewe unawea kutengeneza maono. Ila kazi na tatizo ni njia. Kuzijua njia za Mungu na kuzikubali hapo ndipo kazi ilipo.

Alisema watu wengi wana maono, ila tatizo ni njia za Mungu. Aliniambia kuwa njia za Mungu ni ngumu sana. Yusufu kutupwa kwenye shimo, ilikuwa ni njia ya kutimiza ndoto zake. Kuuzwa kwake na kuwekwa gerezani pia. 

Akaniuliza ni nani angezikubali hizo njia? Akaniambia tena kuwa unaweza kujiona unaenda mbele ila Mungu akakwambia rudi nyuma na ikawa ndio njia ambayo Mungu anaitaka.

Ananiambia haya wakati mimi nipo katika mapito magumu na mazito. Kikawaida ni mahali ambapo mtu huoni mbele wala nyuma. Ni sawa na kuwa kwenye kisiwa kile cha Patimo katika majira mbayo bado hujamuona Malaika wa Bwana ili akupe maono yale. Ukigeuka unasikia tu ngurumo za simba, ukijilaza nakutana na michirizi ya chatu, ukijikaza kufunga macho unahisi mitambao ya nyoka, ukigeuka tembo wapo kwenye misafara.

Nilimuelewa sana huyu maana mimi binafsi huwa ninamuheshimu sana mtu aliyeokoka ambaye ndani yake kafanikiwa kiuchumi kihali yaani kwa kumtegemea Mungu na hadi wakati huo bado moto wa wokovu ndani yake haujazimika. Huyu ninamuheshimu sana. Kwanza kufika hapo; lazima kuna mahali kapitia: pili wengi tunawaombea ila wakichanua tu kijinga kinazimika. 

Mtu kama huyu huwa na kanuni. Aliniambi kuwa mtu kuwa na maono sio kazi, wengi wana maono. Ila tatizo njia za Mungu. Akaniambi unajua ni kwa nini maandiko hukutaka umepea Bwana moyo wako ili macho yako yapendezwe na njia zake! Mithali 23:26 Mwanangu, nipe moyo wako; Macho yako yapendezwe na njia zangu.

 Alinipeleka kwa Musa kwenye Kutoka ile 33:13. Ambapo Musa namwambia Mungu ikiwa amepata kibali machoni pake, basi Mungu amuonyeshe njia zake ili nini? Ili apate kumjua kisha aweze kupata neema mbele za Mungu.

Nakuelezaukweli unayesoma kitabu hiki kuwa wengi tunataka kupata neema mbele za Mungu ila hatutaki kujua njia zake kwanza. Hili ni kosa kubwa sana ambalo hulifanya. 

Ndiposa nimeonelea ni vyema kukuletea kitabu hiki ili tuweze kunufaika vilivyyo na jambo hili. Tujifunze kumtumaini Mungu, na kumkabithi njia/kazi zetu ili mawazo yetu yaweze kuthibitika. 

Kitabu kikitoka kitafute tafadhali...

Kama hujaokoka nikutie moyo kufanya hivyo tafadhali. Maana maisha ya dhambi hayampendezi Mungu. Wanaokufa kwenye dhambi mshahara wao ni moto, ila wanaokufa katika neema ya wokovu ni kuishi na Mungu milele. Tafadhali usiseme leo sijajiandaa, ama kesho, au kesho kuta, siku nyingine sio jibu sahihi. Hujui siku wala saa ya kuondoka kwako hapa ulimwenguni. Wapo wanaokufa kwa kugongwa na gari, kuugua ghafula na hata kufia usingizini. Alilala vizuri ila ndo hakuamka tena, alipoaga usiku mwema, kumbe alimaanisha usiku mwingine! Nani ajuaye wako! Huna hakikisho la kuishi milele na hujui siku wala saa, huwa inakuja ghafula.

Sasa fuatisha kwa imani Sala hii ya Toba pamoja nami: Sema, MUNGU BABA, NINAKUJA MBELE ZAKO, NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NISAMEHE, NIOSHE, NITAKASE KWA ILE DAMU YAKO, FUTA JINA LANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, LIANDIKE SASA KWENYE KITABU CHA UZIMA WA MILELE; Amen.

Hongera kwa kuokoka, na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo. 

Kwa maombezi, Maswali, Ushauri na hata Sadaka yako kwa Mpesa, Usisite kuwasilaina nasi. 

Mawasiliano; Simu au WhatApp: +255759859287 Baruapepe: ukombozigospel@gmail.com au tembelea pia YouTube Channel yetu ya Ukombozi Gospel au Ug Tv , www.ukombozigospel.blogspot.com Asante.

Jumapili, 17 Aprili 2022

FAIDA ZA USHINDI WA MATESO NA KIFO CHA YESU KATIKA SURA YA PITO LAKO

 Na Mwalimu Oscar Samba (Tafadhali #Share na kwa wengine ili nao Wanufaike)

Sehemu nyingine (3) ya Kitabu chetu cha MUONE MUNGU NYUMA YA PITO AU JARIBU LAKO. Ni katika mada yetu ya kwanza ya ; 1. Jinsi Mungu Anavyoweza Kuwa Nyuma ya Jambo Gumu Linalokusonga. Na katika pwenti ya mwisho ya mada hii: 

. Mfano wa Mateso ya Yesu na Msalabani: Nawiwa kukuhitimishia mada hii kwa mfano wa Yesu katika mauti ya msalaba. Leo sisi tunaweza kulielewa jambo hili maana faida zake kwetu zi dhairi ila kwa wanafunzi wake na jamii ile halikuwa jambo jepesi. Ndio mana ukisoma kisa kile katika Luka 24 cha wananchi wale waliokuwa wakielekea Emau utaelewa kiupana sana. Kuna mitazamo walikuwa nayo kuhusu ujio wa Yesu. Walimtazama kama mfalme na mkombozi wa dunia ile au kwa Wayahudi kwa jinsi ya kisiasa na kibinadamu.

Maana taifa hili lilikuwa chini ya utawala wa dola ya Kirumi. Kipindi cha nyuma walipokuwa chini ya tawala kama hizo kuna namna kuliibuka watu maalumu waliowakomboa; mfano walipokuwa chini ya Wafilisti Mungu alimuinua Samsoni na kuwakomboa: Waamuzi 13 na kuendelea. Walipokuwa chini wa Wamidiani waliibuka Gideoni na kuwatoa utumwani kwa mkono wa Bwana; soma Waamuzi sita utajionea pale.