Ujumbee huu ni Sehemu ya Kitabu Chetu Kipya Cha: KILI ZILIZO MACHO KATIKA UFALME WA MBINGUNI
Mathayo 24:45
Na Mwalimu Oscar Samba
Hiyo ni picha muhimu unayopaswa kuwa nayo, wakati huu unapoelekea kukisoma kitabu hiki. Ni muhimu sana kufahamu ya kuwa maana moja wapo ya Yesu ya kututaka tusilale usingizi yaani tuwe macho; ama tukeshe ililenga eneo la akili zetu.
Tazama mfano ule wa Wana Wali watano wenye Busara na watano Wapumbavu. Ndipo utakapotambua ya kuwa upumbavu unaotajwa pale, ni unaotokana na hali ya kutokujua ni nini cha kufanya katika nyakati kama hizi.
Malengo ya Kitabu:
1. Kuyafumbua Macho ya Aliyefumbwa, Kuziamsha Akili za Asinziaye ili Aweze Kuwa na Utayari wa Kutumika Kiusahihi (kama impasavyo), Katika Kulielekea Kusudi Aliloitiwa Kinyakati.
2. Kumpatia Ufahamu, Utakaotumika Vyema na Akili Zake, ili Kujua Ni Nini Kimpasacho Kukifanya Katika Majira Husika.
1 Mambo ya Nyakati 12:32 Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.
3. Kumjengea Fikra za Kumuwezesha Kuzitambua Hila za Adui Shetani; Katika Mpango wa Kumnyamazisha au Kutaka Kumpoozesha Kiroho na Kiutumishi, (au Kiutumishi/Kiroho.) 2 Wakorintho 2:11 Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikra zake.
4....
Lengo Kuu: Kukujengea Fikra za Kiuamsho, Ili Kuibua Hari na Kuamsha .... Kukuumbia Nia ya Kiuamsho Ndani Yako. (Penye Nia, Pana Utayari).
.....,....
1. Maonevu na Migogoro Katika Kanisa, Ama Baina ya Watumishi, au Washirika: Ni Ishara ya Kujisahau Kiroho. Watu waliopoteza kusudi, au kulisahau ama walioshindwa kujitambua ndio pekee huweza kuanza kuumana. Unapoona