Utakutana na Ujumbe huu kwenye Kitabu Chetu Kipya Kinachoandikwa Hivi Sasa cha UMUHIMU WA KUMPENDA NA KUMJUA MUNGU KWA MTOTO AU KIJANA CHIPUKIZI
NA Mwl Oscar Samba
Andiko hili linagusa nyanya zote muhimu kwako wewe kama mtumishi wa Mungu. Mosi ni eneo la kifamilia yaani baba mama na watoto au ndugu zako wengine. Pili eneo la kiserikali, anaposema muheshimu mfalme, hapo pia pana gusa viongozi wako wa kikanisa, viongozi wa kiroho na hata wakitaasisi au kampuni. Kwa ujumla ni kuheshimu utawala.
Anatupa dhima ya kumcha Mungu, kumpa Mungu heshima yake. Nasi twajua habari za kumcha Mungu! Ya kwamba ni kumuhofu, kuukataa na kuuchukia ovu. Yusufu akasema nitendeje uovu huu ni mkose Mungu? Linaanza na kukutaka kutoa heshima kwa watu wote. Bila kubagua umri, dini, ama kabila na kadhalika. Anasema katika watu wote.
1 Petro 2:17 Waheshimuni watu wote. Wapendeni ndugu. Mcheni Mungu. Mpeni heshima mfalme.
Zaidi Soma: www.ukombozigospel.blogspot.com
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni