Jumapili, 24 Aprili 2022

NI KWA NINI MUNGU ANAKUTAKA UMKABITHI NJIA ZAKO

Na Mwalimu Oscar Samba (Tafadhali #Share na kwa wengine ili nao Wanufaike)

Utangulizi wa kitabu chetu cha NI KWA NINI MUNGU ANAKUTAKA UMKABITHI NJIA ZAKO

Nilifanikiwa kuzungumza na mtu mmoja aliyeokoka ambaye Mungu amebariki kiuchumi, naye alinipa maneno magumu ambayo yalinifanya kufikiri sana. Aliniambia kuwa alisikia msukumo wa kunipigia simu na gafula akijikuta akiniuliza maswali kadhaa kuhusu mipango yangu ya kihuduma na kieleimu. 

Kisha alinipa maneno ambayo yalinifanya kufikiri sana na kuona hapa kuna kitu ambacho walimu wengi wa somo la maono hatukitendei haki. Aliniambi; Kuwa na maono sio kazi, Mungu anaweza kukupa maono, hata wewe unawea kutengeneza maono. Ila kazi na tatizo ni njia. Kuzijua njia za Mungu na kuzikubali hapo ndipo kazi ilipo.

Alisema watu wengi wana maono, ila tatizo ni njia za Mungu. Aliniambia kuwa njia za Mungu ni ngumu sana. Yusufu kutupwa kwenye shimo, ilikuwa ni njia ya kutimiza ndoto zake. Kuuzwa kwake na kuwekwa gerezani pia. 

Akaniuliza ni nani angezikubali hizo njia? Akaniambia tena kuwa unaweza kujiona unaenda mbele ila Mungu akakwambia rudi nyuma na ikawa ndio njia ambayo Mungu anaitaka.

Ananiambia haya wakati mimi nipo katika mapito magumu na mazito. Kikawaida ni mahali ambapo mtu huoni mbele wala nyuma. Ni sawa na kuwa kwenye kisiwa kile cha Patimo katika majira mbayo bado hujamuona Malaika wa Bwana ili akupe maono yale. Ukigeuka unasikia tu ngurumo za simba, ukijilaza nakutana na michirizi ya chatu, ukijikaza kufunga macho unahisi mitambao ya nyoka, ukigeuka tembo wapo kwenye misafara.

Nilimuelewa sana huyu maana mimi binafsi huwa ninamuheshimu sana mtu aliyeokoka ambaye ndani yake kafanikiwa kiuchumi kihali yaani kwa kumtegemea Mungu na hadi wakati huo bado moto wa wokovu ndani yake haujazimika. Huyu ninamuheshimu sana. Kwanza kufika hapo; lazima kuna mahali kapitia: pili wengi tunawaombea ila wakichanua tu kijinga kinazimika. 

Mtu kama huyu huwa na kanuni. Aliniambi kuwa mtu kuwa na maono sio kazi, wengi wana maono. Ila tatizo njia za Mungu. Akaniambi unajua ni kwa nini maandiko hukutaka umepea Bwana moyo wako ili macho yako yapendezwe na njia zake! Mithali 23:26 Mwanangu, nipe moyo wako; Macho yako yapendezwe na njia zangu.

 Alinipeleka kwa Musa kwenye Kutoka ile 33:13. Ambapo Musa namwambia Mungu ikiwa amepata kibali machoni pake, basi Mungu amuonyeshe njia zake ili nini? Ili apate kumjua kisha aweze kupata neema mbele za Mungu.

Nakuelezaukweli unayesoma kitabu hiki kuwa wengi tunataka kupata neema mbele za Mungu ila hatutaki kujua njia zake kwanza. Hili ni kosa kubwa sana ambalo hulifanya. 

Ndiposa nimeonelea ni vyema kukuletea kitabu hiki ili tuweze kunufaika vilivyyo na jambo hili. Tujifunze kumtumaini Mungu, na kumkabithi njia/kazi zetu ili mawazo yetu yaweze kuthibitika. 

Kitabu kikitoka kitafute tafadhali...

Kama hujaokoka nikutie moyo kufanya hivyo tafadhali. Maana maisha ya dhambi hayampendezi Mungu. Wanaokufa kwenye dhambi mshahara wao ni moto, ila wanaokufa katika neema ya wokovu ni kuishi na Mungu milele. Tafadhali usiseme leo sijajiandaa, ama kesho, au kesho kuta, siku nyingine sio jibu sahihi. Hujui siku wala saa ya kuondoka kwako hapa ulimwenguni. Wapo wanaokufa kwa kugongwa na gari, kuugua ghafula na hata kufia usingizini. Alilala vizuri ila ndo hakuamka tena, alipoaga usiku mwema, kumbe alimaanisha usiku mwingine! Nani ajuaye wako! Huna hakikisho la kuishi milele na hujui siku wala saa, huwa inakuja ghafula.

Sasa fuatisha kwa imani Sala hii ya Toba pamoja nami: Sema, MUNGU BABA, NINAKUJA MBELE ZAKO, NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NISAMEHE, NIOSHE, NITAKASE KWA ILE DAMU YAKO, FUTA JINA LANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, LIANDIKE SASA KWENYE KITABU CHA UZIMA WA MILELE; Amen.

Hongera kwa kuokoka, na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo. 

Kwa maombezi, Maswali, Ushauri na hata Sadaka yako kwa Mpesa, Usisite kuwasilaina nasi. 

Mawasiliano; Simu au WhatApp: +255759859287 Baruapepe: ukombozigospel@gmail.com au tembelea pia YouTube Channel yetu ya Ukombozi Gospel au Ug Tv , www.ukombozigospel.blogspot.com Asante.

Jumapili, 17 Aprili 2022

FAIDA ZA USHINDI WA MATESO NA KIFO CHA YESU KATIKA SURA YA PITO LAKO

 Na Mwalimu Oscar Samba (Tafadhali #Share na kwa wengine ili nao Wanufaike)

Sehemu nyingine (3) ya Kitabu chetu cha MUONE MUNGU NYUMA YA PITO AU JARIBU LAKO. Ni katika mada yetu ya kwanza ya ; 1. Jinsi Mungu Anavyoweza Kuwa Nyuma ya Jambo Gumu Linalokusonga. Na katika pwenti ya mwisho ya mada hii: 

. Mfano wa Mateso ya Yesu na Msalabani: Nawiwa kukuhitimishia mada hii kwa mfano wa Yesu katika mauti ya msalaba. Leo sisi tunaweza kulielewa jambo hili maana faida zake kwetu zi dhairi ila kwa wanafunzi wake na jamii ile halikuwa jambo jepesi. Ndio mana ukisoma kisa kile katika Luka 24 cha wananchi wale waliokuwa wakielekea Emau utaelewa kiupana sana. Kuna mitazamo walikuwa nayo kuhusu ujio wa Yesu. Walimtazama kama mfalme na mkombozi wa dunia ile au kwa Wayahudi kwa jinsi ya kisiasa na kibinadamu.

Maana taifa hili lilikuwa chini ya utawala wa dola ya Kirumi. Kipindi cha nyuma walipokuwa chini ya tawala kama hizo kuna namna kuliibuka watu maalumu waliowakomboa; mfano walipokuwa chini ya Wafilisti Mungu alimuinua Samsoni na kuwakomboa: Waamuzi 13 na kuendelea. Walipokuwa chini wa Wamidiani waliibuka Gideoni na kuwatoa utumwani kwa mkono wa Bwana; soma Waamuzi sita utajionea pale.

Alhamisi, 14 Aprili 2022

FAIDA ZA KUSHINDA JARIBU AU PITO ( Majaribu ni Mtaji)

 Na Mwalimu Oscar Samba (Tafadhali #Share na kwa wengine ilia nao Wanufaikae)

Sehemu nyingine ya Kitabu chetu cha MUONE MUNGU NYUMA YA PITO AU JARIBU LAKO. Ni katika mada yetu ya kwanza ya ; 1. Jinsi Mungu Anavyoweza Kuwa Nyuma ya Jambo Gumu Linalokusonga. Na pwenti ya kwanza pia ya mada hiyo: 

 1. Mfano wa Shadraka, na Meshaki, na Abednego. Napenda sana sentensi yao hii muhimu katika pito, na kwa wale wasomaji wa kitabu cha CHAKUFANYA UNAPOKUWA NJIA PANDA; wanaweza kunielewa kwa upana. Vijana hawa walimnenea mfalme kuwa hata kama Mungu hatawaokoka bado hawawezi kumuacha.

Kwamba kuwaokoa ni jambo jema, na ndilo wanalolisubiria, la hata asipofanya hivyo bado hawawezi kumuacha. Wasomaji wa kitabu cha Waebrania hususani ile sura ya 11 wanaweza kuelewa kuwa kuna aina mbili ya imani tajwa pale. Ya kwanza ni ile iliyoleta wokovu na ya pili ni ile iliyowawezesha kufa katika Bwana yaani bila wokovu kwa jinsi ya mwilini. Hawa nao ni mashujaa japo hawakuokoka katika mateso bali waliyafia mateso;

35….Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora; 36 wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani; 

Jumanne, 12 Aprili 2022

JIFUNZE KUMUONA MUNGU NYUMA YA PITO AU JARIBU LAKO

 Ujumbe huu ni Utangulizi wa kitabu chetu cha MUONE MUNGU NYUMA YA PITO AU JARIBU LAKO

Na Mwalimu Oscar Samba (#Share ujumbe huu kwa Wengine ili Tuvuke pamoja nao)

Kimwili tunaweza kuwaona adui zako kuwa ndio waliokusukumiza kwenye hilo shimo, ndugu zako, wapendwa na hata mchungaji wako. Kumbe Mungu yupo nyuma ya tatizo hilo ili akufanye kuwa waziri mkuu kwenye nchi ya Misri.

Unaweza ukawa na kila sababu za kuwalaumu viongozi waliokuwa wakimzunguka mfalme Nebukadreza ama Dario kwa kutengeneza sheria batili na kisha kumfanya mfalme kukutupa kwenye tundu la simba ama lile tanuru la moto! Kumbe nyuma yake Yesu yupo ili ajitukuze kwa mfalme, dunia yote na kisha kukuokoa ukiwa mshindi na mwenye kuinuliwa kicheo.

Jifunze kumuona Yesu kwenye kila nyuma ya pito au tatizo, ama nyakati ngumu unazokuwa unazipitia. Hii itakupa kunufaika vilivyo na nyakati hizo. Kuna tatizo limenikuta kipindi hiki; limetumika sana kunisukumia kwenye kusudi lake.

Jumanne, 5 Aprili 2022

Elewa ni Kwa nini Ndoa ni Zaidi ya Ulendo

 #VIJANA_NISIKILIZENI_Haya_Nayo_Ni_Maneno_ya_Mwenye_Hekima


Moyo Unaweza Kumpenda Mtu Bila Kuwa na Sababu Yoyote ya Msingi ila Usikubali Kuoana na Mtu Asiyetosheleza Vigezo Vya Ndoa kwa Viwango Fulani.

Moyo wa mwanadamu kuna muda unavutiwa na mtu bila hata kukupa sababu zenye mashiko kwanini umempenda. Utamsikia mtu akisema basi nimepanda tu! Ni kweli ni jambo jema, na hatuwezi kuweka sababu kwa kila mtu au maamuzi ya moyo kupenda.

Ndiposa wengine wakasema mapenzi ni upofu, ikiwa na maana kwamba kuna mambo ya msingi mtu anaweza  kuya_overloock ama kuyapuuza ifikapo swala la kupenda. Hapa napo sina shinda napo.

Alhamisi, 31 Machi 2022

Sehemu ya Kitabu Chetu cha CHAKUFANYA UNAPOKUWA NJIA PANDA, Kuna na Ushuhuda wa Mwalimu Oscar, Nia ya Ujumbe ni Kukutana Unipe Moyo Usikate Tamaa

 Na Mwalimu Oscar Samba

Ujumbe huu ni shehemu ya Kitabu chetu cha CHAKUFANYA UNAPOKUWA NJIA PANDA, katika mada ya Kwanza inayohusu aina ya Imani inayohitajika Ukiwa Njia Panda. Kumbuka ni kitabu chenye kuelezea mazingira ya mtu aliyegubikwa na maamuzi zaidi ya moja ikiwa ni matokeo ya mahali anapopitia. Yaani Njia panda ya kiroho au Kifikra na hapa ni katika pwenti ya pili

2. Tazama Nguvu Zako. Kwanza fahamu mtu anapokata tamaa, hususani katika kiwango cha kuwa radhi kuachana na mapenzi ya Mungu hata kama anayajua dhairi, au kufikia kiwango cha kutamani kufa; ni nguvu zimemuishia! Kwa kifupi amelemewa na aina ya dhiki aliyonayo;

Maana ndugu, hatupendi, msijue habari ya dhiki ile iliyotupata katika Asia, ya kwamba tulilemewa mno kuliko nguvu zetu, hata tukakata tamaa ya kuishi. 2 Wakorintho 1:8

Nguvu zao zilizidiwa, kilichofuata ni wao kukta tamaa ya kuishi! Sasa utaelewa ni kwa nini Elia alijiombea kufa katika ile 1Wafalme 19! Wengi wanashangaa na kukosa majibu maana huku nyuma tu katoka kufanya tukio kubwa na la kushangaza! Ni kwamba vita viliibuka upya, na nguvu hakuwa nayo!

Imani haikai hewani, kuna mahali inakaa. Eneo moja wapo ni kwenye nafsi, na inategemea sana nguvu zilzizopo kwenye nafsi yako. Ndio maana Yesu alipoishiwa nguvu alianza janja ya kutaka kukwepa mapenzi ya Baba yake! Sio kwamba alikuwa hajui umuhimu wake, la! Alijua sana tu. Ila nguvu zilipunguka. 

Jumatatu, 3 Januari 2022

BAADA YA MAFUTA, CHUMVI, STIKA, MAFUTA, JALENDA NA MAJI YA UPAKO, SASA WAJA NA NGUO ZA NDANI, Hizi ni Imani Potofu

Imani Potofu, sasa ya zalisha na Chupi au Nguo za ndani za Upako, ni baada ya mafuta, maji na Chumvi za upako

SIPENDI SANA KUSHAMBULIA IMANI NYINGINE..ila tunapaswa kuwa Makini sana na Wahuni walioivamia kazi ya MUNGU wakifanya vituko kwa vigezo vya Ufunuo... Wewe Mshirika usiweke akili mfukoni na kukubali kukubaliana na kila kitu kisa kimetoka kwa mtumishi anayejiita wa Mungu kwa kisingizio cha Ufunuo..

Ndio maana watu wananyweshwa hadi Jick ya kuondolea madoa kwenye nguo, waDada wanatomaswa viungo vyao na kupakwa mafuta sehemu nyeti..ukiuliza unaambiwa alifunuliwa!

Maji na Mafuta vimegeuka kuwa uganga wa Kilokole siku hizi..Yesu hapewi heshima bali ni maji yaliniponya, mafuta ya upako yalinisaidia sana..Imani kwa Yesu hakuna tena.

Jumatatu, 13 Desemba 2021

SULUHU KWA JAMIII AU ENEO LENYE KUKABILIWÀ NA TATIZO LA WATU KUJIUA

Na Mwalimu Oscar Samba

Mithali 28:17 Aliyelemewa na damu ya mtu Atalikimbilia shimo; wala mtu asimzuie.

Andiko hilo hapo la Mithali linatupa kufahamu kuwa watu wanaojiua au kukimbilia mauti (ambao hapo imetumika au yametumika maneno kukimbilia shimo) ni matokeo ya kulemewa au kuwa na deni au mzigo wa damu iliyowahi kumwagika.

Sasa inawezekani aliimwaga yeye, au imemwaga kwenye eneo anaoloishi ama i juu ya uzao au jamii yake. Kwa ujumla ni kwamba kuna deni juu yake.

Damu huweza kukaa kwenye uzao nasi twajua hivyo, maana hata wale waliomsulibisha Yesu walikiri kuwa iwe juu yao na uzao wao. Pia eneo laweza kubeba damu maana hata aridhi iliyonunuliwa na fedha za usaliti wa Yuda ilitwa konde la damu.

Lakini pia damu ya Habili ililia kutoka aridhini. Kuna somo au kipengele cha kwenye kitabu fulani nichowahi kukiandika kinaitwa, ARIDHI KAMA KIUMBE HAI. Hapo nafunza vyema namna ya kushughulika na mambo kama haya.

Jumatano, 24 Novemba 2021

NI JUKUMU LAKO KUITUMIA MAMLAKA Mathayo 28:18










Mathayo 28:18 Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.

Ni wajibu na jukumu lako, na jitihada zako kuhakikisha ya kwamba unaweka imani na unaipa matendo tena kwa kujiamini ili mamlaka hiyo iweze kuwa halisi kwako.

Wewe ni sawa na askari mwenye bunduki, aspojua kuitumia bado hataweza kumdhuru adui. Na adui akijua muhuska hajui kuitumia basi naye hatamuogopa.

Tumia mamlaka uliyonayo vilivyo.

*Kumbuka* : Sio Jukumu la Yesu kuitumia. Ni lako. Yesu yupo kuiwezesha ifanaye kazi.

Ni muhimu kulielewa hili maana kuna wakati tunamlaumu Yesu na kumuona hajatusaidia kanakwamba Yeye ndie aliyepaswa kuitumia..hapana..alipokabithiwa yote ama vyote, alitukabithi sisi.

Nikikupa bunduki, usipofwetua risasi ni makosa kuilaumu bunduki ama aliyekukabithi... www.ukombozigospel.blogspot.com

 

Alhamisi, 18 Novemba 2021

Maelekezo Muhimu kwa Watumishi na Wapendwa

 Kuna wakati tunampa adui nafasi sisi wenyewe, wanapata nafasi ya kutushitaki kutokana na makosa ya ulimi na mwenendo.


Ila tukijifunza kutenda vyema, kwa akili kama Daudi alivyokuwa akitegewa mitego na mfalme Sauli kisha naye kutenda kwa maarifa, hakika adui hatapata uhalali wa kututia hatiani.


Hata akipambana itakuwa ni kwa hila tu, na hila zinamwisho wake.


1 Samweli 18:21 Naye Sauli akasema moyoni, Mimi nitamwoza huyu, awe mtego kwake, tena kwamba mkono wa Wafilisti uwe juu yake. Basi Sauli akamwambia Daudi mara ya pili, Leo utakuwa mkwe wangu.


:29 Naye Sauli akazidi kumwogopa Daudi; Sauli akawa adui yake Daudi sikuzote.


Mbinu pekee ya kumshinda adui wa namna hii ni kutenda kwa akili, hususani adui anapokuwa ni mwenye nafasi fulani ikiwemo kubwa kukuzidi kama ya mchungaji wako, mwangalizi, askofu na kadhalika, na hata mkuu wako wa idara au kiongozi fulani.


Ama akiwa ni mwanandoa mwenzako. Busara inahitajika siku zote, maana kwa nafasi yake anaweza kukushitaki na kukuhesabia hatia japo nia yake sio kosa alilokushitakia bali ni ile chuki iliyopo moyoni, na wewe ili kumdhibiti ni kuhakikisha unamnyima nafasi.



:30 Wakati huo wakuu wa Wafilisti wakatoka; kisha ikawa, kila mara walipotoka, Daudi akatenda kwa busara zaidi ya watumishi wote wa Sauli hivyo jina lake likawa na sifa kuu.


Zaidi tembelea:

www.ukombozigospel.blogspot.com


Zaburi 119:110 Watendao uovu wamenitegea mtego, Lakini sikuikosa njia ya mausia yako.


Jumanne, 5 Oktoba 2021

KUPENDA MAFUNDISHO au NENO

 Na Mwalimu Oscar Samba

Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu chetu cha NGUVU YA NENO LA MUNGU KWENYE MAISHA YA MWANADAMU, pwenti ya; . PENDA MAFUNDISHO. Kiu ya Mafundisho imepotea kwenye kanisa leo; kuna kiu ya mambo mengine! Hata kwa wale wenye kiu ya Kiungu, wamejikuta wakitekwa na misisimko wa wahubiri wenye mbwembwe na kujisifia mali, na vitu vya dunia hii sanjari na ujanja wa maneno kuliko neno la kweli na yale yenye maarifa ya kiungu ndani yake. Itisha semina ya VIKOBA au ujasiriamali kanisani, utashangaa hata mwenye wiki tatu ambaye hajaja kanisani atakavyowahi, siku hiyo hakuna mchelewaji! Tuendelee;

Mahubiri, mawaitha ya Yesu,

Jumatano, 29 Septemba 2021

KWETU NI MBINGUNI



Waebrania 13:14 Maana hapa hatuna mji udumuo, bali twautafuta ule ujao.

Sijui wewe! Ila nijualo ni kwamba Sisi Tuliokoka, ama Tuliomuamini Bwana Yesu kwetu ni Mbinguni hapa Duniani sio kwetu!

Ni sawa na kituo cha Mabasi cha Ubungo ama kile cha Mbezi, ni sawa na stendi ya Daladala au Matatu! 

Hapa Duniani ni sawa na Njiani..mimi sijafika wala wewe hujafika, bali tunapaswa kukaza mwendo, huku tukiwa na taraja ama shabaha yetu ikiwa ni kuvikwa taji ama kupata Thawabu ile isiyoharibuka..

Kwa hiyo huna haja ya kujitaabisha na mateso na shida ama manyanyaso ya dunia hii..

Jumanne, 28 Septemba 2021

Mtazame Yesu Sio Wimbi

 

MTAZAME YESU NA SIO WIMBI

Mathayo 14:29 Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu.

30 Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe.

Sijui umekwamia wapi..? Nina chojua ni kwamba ulianza au ulipokea wazo hilo la biashara katika imani kubwa, na moyoni mwako ulisema huyu ni Mungu ndie aliyenipatia wazo hili, kazi hii, mke au mume huyu..ila mara baada ya kuanza kumeanza kuinuka vikwazo naq ghafula ukajikuta unaanza kukata tamaa kiasi cha kuyumbisha imani yako sio katika hilo jambo tu bali hata kwa Mungu kama kweli ulimsikia sawasawa ama kama kweli bado yu pamoja nawe..


Alhamisi, 16 Septemba 2021

KARAMA YA KUONYA

Bwana Yesu asifiwe ndugu yangu katika Bwana. Hapana shaka u mzima tena buheri wa afya? Kama sivyo basi Bwana Yesu akupe amani na furaha tele, huku ukimtwika Yeye yale yaliyokulemea na iruhusu furaha yake itawale maisha yako.

Leo Bwana amenipaka mafuta kukuletea ujumbe huu muhimu sana. Sio mara kwa mara utasikia ukifundishwa japo ni kitu ambacho hutakiwa kukifanya kila sehemu. Mashuleni kuna maonyo, kazini, njiani, kwenye vyombo vyetu vya usafiri utasikia nako wakionyana, kwenye makusanyiko mbalimbali hili nalo lipo. Nyumbani na hata makanisani twapaswa kuonyana.

Nawiwa kukueleza kwa upana wake namna ambavyo tunapaswa kuonyana, na jinsi ambavyo karama hii hutakiwa kuwa na vitu muhimu ambatanishi aidha iwe tabia au roho fulani au karama saidizi kwayo. Haijalishi ni karama zinazojitegemea ila hapa zinapaswa kuambatana na hii, alikadhalika tabia ama tunda la Roho.

MSINGI WA KARAMA KIUJUMLA

1 Wakorintho kinaeleza kiupana kuhusu aina 9 za karama, na mbele yake kuna huduma tano zinatajwa. Lengo la karama na huduma ni kujenga mwili wa Kristo kama Waefeso inavyotanabaisha;

Ijumaa, 30 Julai 2021

UPENDO WA MUNGU KWAKO NI WA MILELE, HAUFUNGWI NA MSIMU WALA MUDA

Na Mwalimu Oscar Samba

Ujumbe hu ni Sehemu ya Kitabu chetu cha MUNGU ANAKUPENDA. Kitabu kinachonuia kukusaidia kuliona pendo lake hata kama upo wakati mgumu, ukifahamu kuwa haupitii kwa sababu Mungu amekuacha, hakupendi ama amekukatataa.

Yeremia 31:3-7

Bwana alinitokea zamani, akisema, Naam nimekupenda kwa upendo wa milele, ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu.
 Mara ya pili nitakujenga, nawe utajengwa, Ee bikira wa Israeli mara ya pili utapambwa kwa matari yako, nawe utatokea katika michezo yao wanaofurahi. Mara ya pili utapanda mizabibu juu ya milima ya Samaria; wapanzi watapanda, nao watayafurahia matunda yake.
Maana kutakuwa siku moja, ambayo walinzi watalia juu ya vilima vya Efraimu, Inukeni, tukaende Sayuni, kwa Bwana, Mungu wetu.
Maana Bwana asema hivi, Mwimbieni Yakobo kwa furaha, mkampigie kelele mkuu wa mataifa, tangazeni, sifuni, mkaseme, Ee Bwana, uwaokoe watu wako, mabaki ya Israeli.

 

Jumatano, 21 Julai 2021

KAWIA UFIKE

 Na Mwalimu Oscar Samba

Ni kweli ngoja ngoja huumiza matumbo, au fahamu pia simba mwendapole ndie mla nyama! Maana mtaka yote kwapupa hukosa yote! Hawakuwahi kukosea waliosema kuwa subra yavuta heri!

 Ni hakika haraka haraka haina baraka! Maana hata waingereza ama wenye kingereza chao husema kuwa, njia ya kato siku zote ni njia isiyo sahihi.

 Kuna watu wengi wamjejikuta wakiingia hasara maishani mara baada ya kutaka mafanikio kwa haraka! Wamejikuta wakipoteza ama wakiharibikiwa kimaisha, ni kweli ni tajiri ila kapoteza mke na woto kwa sababu ya mashariti ya mganga! Ni kweli ana fedha sawa na elimu sawa ila ni muadhirika wa UKIMWI! Kapenda chipsi hatimae ni mjamzito na ndoto za kusoma zimakomea hapo!

 Ni heri ukawie lakini ufike uendako, kuliko kukimbia ukajikuta unakimbia hadi unasahau nyumbani ama unashindwa kuangalia taadhari ya alama za barabarani na hatimae ukaingia katika kusababisha ama kujisababishia ajali!

Narudia tena na tena kuwa kawia ufike, pole pole ndio mwendo! Unaonaje mkulima akapanda mbegu leo na kutaka kuvuna siku hiyo hiyo! Kama kwa mkulima haiwezekani uwe na uwakika kuwa na katika safari ya mafanikio ndivyo ilivyo.   

Embu tujionee jinsi maandiko mtakatifu ya Biblia yanavyotufunza katika kitabu kile cha Yakobo: 5:5 Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho.

8 Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia.9 Ndugu, msinung'unikiane, msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.