Jumatano, 29 Septemba 2021
KWETU NI MBINGUNI
Jumanne, 28 Septemba 2021
Mtazame Yesu Sio Wimbi
MTAZAME YESU NA SIO WIMBI
Mathayo 14:29 Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu.
30 Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe.
Sijui umekwamia wapi..? Nina chojua ni kwamba ulianza au ulipokea wazo hilo la biashara katika imani kubwa, na moyoni mwako ulisema huyu ni Mungu ndie aliyenipatia wazo hili, kazi hii, mke au mume huyu..ila mara baada ya kuanza kumeanza kuinuka vikwazo naq ghafula ukajikuta unaanza kukata tamaa kiasi cha kuyumbisha imani yako sio katika hilo jambo tu bali hata kwa Mungu kama kweli ulimsikia sawasawa ama kama kweli bado yu pamoja nawe..
Jumatano, 22 Septemba 2021
Alhamisi, 16 Septemba 2021
KARAMA YA KUONYA
Bwana Yesu asifiwe ndugu yangu katika Bwana. Hapana shaka u mzima tena buheri wa afya? Kama sivyo basi Bwana Yesu akupe amani na furaha tele, huku ukimtwika Yeye yale yaliyokulemea na iruhusu furaha yake itawale maisha yako.
Leo Bwana amenipaka mafuta kukuletea ujumbe huu muhimu sana. Sio mara kwa mara utasikia ukifundishwa japo ni kitu ambacho hutakiwa kukifanya kila sehemu. Mashuleni kuna maonyo, kazini, njiani, kwenye vyombo vyetu vya usafiri utasikia nako wakionyana, kwenye makusanyiko mbalimbali hili nalo lipo. Nyumbani na hata makanisani twapaswa kuonyana.
Nawiwa kukueleza kwa upana wake namna ambavyo tunapaswa kuonyana, na jinsi ambavyo karama hii hutakiwa kuwa na vitu muhimu ambatanishi aidha iwe tabia au roho fulani au karama saidizi kwayo. Haijalishi ni karama zinazojitegemea ila hapa zinapaswa kuambatana na hii, alikadhalika tabia ama tunda la Roho.
MSINGI WA KARAMA KIUJUMLA
1 Wakorintho kinaeleza kiupana kuhusu aina 9 za karama, na mbele yake kuna huduma tano zinatajwa. Lengo la karama na huduma ni kujenga mwili wa Kristo kama Waefeso inavyotanabaisha;
Jumatano, 4 Agosti 2021
Ijumaa, 30 Julai 2021
UPENDO WA MUNGU KWAKO NI WA MILELE, HAUFUNGWI NA MSIMU WALA MUDA
Na Mwalimu Oscar Samba
Ujumbe hu ni Sehemu ya Kitabu chetu cha MUNGU ANAKUPENDA. Kitabu kinachonuia kukusaidia kuliona pendo lake hata kama upo wakati mgumu, ukifahamu kuwa haupitii kwa sababu Mungu amekuacha, hakupendi ama amekukatataa.
Yeremia 31:3-7
Bwana alinitokea zamani, akisema, Naam nimekupenda kwa upendo wa milele,
ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu.
Mara
ya pili nitakujenga, nawe utajengwa, Ee bikira wa Israeli mara ya pili
utapambwa kwa matari yako, nawe utatokea katika michezo yao wanaofurahi. Mara ya pili utapanda mizabibu juu ya milima ya
Samaria; wapanzi watapanda, nao watayafurahia matunda yake.
Maana kutakuwa siku moja, ambayo walinzi
watalia juu ya vilima vya Efraimu, Inukeni, tukaende Sayuni, kwa Bwana, Mungu
wetu.
Maana Bwana asema hivi, Mwimbieni Yakobo kwa
furaha, mkampigie kelele mkuu wa mataifa, tangazeni, sifuni, mkaseme, Ee Bwana,
uwaokoe watu wako, mabaki ya Israeli.
Jumatano, 21 Julai 2021
KAWIA UFIKE
Na Mwalimu Oscar Samba
Ni kweli ngoja ngoja huumiza matumbo, au fahamu pia simba mwendapole ndie mla nyama! Maana mtaka yote kwapupa hukosa yote! Hawakuwahi kukosea waliosema kuwa subra yavuta heri!
Narudia tena
na tena kuwa kawia ufike, pole pole ndio mwendo! Unaonaje mkulima akapanda
mbegu leo na kutaka kuvuna siku hiyo hiyo! Kama kwa mkulima haiwezekani uwe na uwakika
kuwa na katika safari ya mafanikio ndivyo ilivyo.
Embu tujionee jinsi maandiko
mtakatifu ya Biblia yanavyotufunza katika kitabu kile cha Yakobo: 5:5 Kwa hiyo
ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi
yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na
ya mwisho.
8 Nanyi vumilieni, mthibitishe
mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia.9 Ndugu, msinung'unikiane,
msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.
Jumamosi, 10 Julai 2021
Jumapili, 4 Julai 2021
Jumamosi, 3 Julai 2021
Mwalimu Oscar Samba THAMANI YA KUMKABITHI MUNGU MAISHA YAKO YA BAADAE na...
Jumanne, 6 Aprili 2021
Jumatano, 24 Machi 2021
Ujumbe huu ni sehemu ya #kitabu chetu cha MTUMIKIE MUNGU, UKubali #Wito, #Kuna Faida katika Kumtumikia Mungu, na Kuna Hasara za Kukaidi Wito.
Na Mwalimu Oscar Samba
Usipoelewa jambo hili, huwezi elewa ni kwa nini Mungu aliamua kumfuata Yona baharini! Angeweza kuamuacha na kuinua mtu mwingine!
Jumamosi, 6 Machi 2021
Muombee Elia ama Yusufu wako, Ni Msaada wa kutoka kwenye Majanga kama ya Corona. #Corona #Covd19
nA mWALIMU oSCAR sAMBA
Ujumbe huu ni sehemu ya #kitabu chetu cha MAMBO MUHIMU YA KUFANYA AU KUZINGATIA KUNAPOKUWA NA ADHABU YA KIUNGU INYOIJUMUISHA ENEO ULILOPO AU JAMII
Jumamosi, 27 Februari 2021
Kitabu chetu cha: MAMBO MUHIMU YA KUFANYA AU KUZINGATIA KUNAPOKUWA NA ADHABU YA KIUNGU INYOIJUMUISHA ENEO ULILOPO AU JAMII.
Na Mwalimu Oscar Samba
Neno Kiungu huwakilisha kutoka kwa Mungu au Shetani,
ujumbe huu ni sehemu ya hiki kitabu chenye mada na pwenti kadhaa, ila hapa
nimezicha,bua mbili tu; #Corona #Covd19 #Tsunam #Majanga #Kimbunga #magonjwayamlipuko #tanzania
1. Lifanye Eneo Unloishi kuwa Ghosheni yako. 2. Ijue
na Uitumie Damu ya Yesu ya Pasaka; 3. Mulize Mungu kama Daudi; 4. Litengenezee
Kusudi la Mungu Kisafina kama Musa, ama Nuhu; 5. Jifunze Jambo kwa Mke wa Lutu;
6. Sadaka kama Ulinzi; 7. Sadaka kama Sehemu ya
Rehema, Mfano ile ya Daudi kipindi cha adhabu ya Tauni, 8. Taka Kujua pigo Hilo
au Adhabu hiyo Inataka nini ili Ujisalimishe kwa Bwana, Mfano Rahabu, na Epuka
kosa la Farao.
9. Yajue na
Uyaombe Maombi ya Musa ya Kulitengeneza Boma, 10. Mtafute na Umuondoe Akani, 11.
Jitenge na Kusanyiko, au Kiunganishi cha Kusanyiko ama Waadhibiwa, ondoa jina
lako kwenye watu wanaotakiwa kupewa hiyo Adhabu kwa Damu ya Yesu.
12. Tafuta Maelekezo Maalumu ya Mungu juu yako, kama
Isaka dhidi ya Janga la Njaa na Wazazi wa Yesu. 13. Unapoisikia Hofu Usiipuzie,
Taaka Kujua ni Aina gani ya Hofu ala Uikabili..
14. Tafuta Kukumbuka kama Mungu Aliwahi Kukujuza
hapo Awali na Hukumsikia Vyema au Hukumbuki. (Amosi 3:7 Hakika Bwana MUNGU
hatafanya neno lolote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.)
Sijui sana ni kwa nini kanisa la leo lina uzito kwenye hili, nijualo ni kwamba uwezo wa kusoma alama za
nyakati, au majira umekuwa ni adimu sana kwa kizazi cha leo! Nafahamu kuwa hali
ya kupuzia ndoto, kutokutambua jinsi Mungu anavyoongea, na mafundisho manyonge
kuhusu uhusiano wetu na Roho Mtakatifu ni miongoni mwa sababu ambatanishi.
Kama kuna mahali Shetani amefanikiwa leo ni kuondoa,
ama kuzimisha kama sio kufifisha karama ya unabii, na huduma ya nabii, pamoja
na neno la maarifa!
Na anatumia njia kuu kama mbili hivi, moja ni
kuhakikisha kanisa linapoteza imani na manabii au wanaotumiwa na karama hizi,
kwa kujiwekekea manabii wa uongo, ili kuwakatisha watu tamaa na kuwafanya wa
waone hata wale wa Mungu nao ni kama hao wengine!
Pili analitumia kanisa lenyewe, kwa kufikia hatua ya
kupinga, na kukataa, na kuzimisha huduma na karama hizi, na sababu zao ni
nyingi ila hazina hoja timilifu kibiblia, maana kama kuna wimbi la mafundisho
na huduma potofu, suluhu bado sio kuzima na kukataa ile ya kweli, bali wafunze
watu namna ya kutambua kweli na uongo. Mchele ukiwa na chuya, dawa sio kukataza
nyumbani wasipike tena mchele bali ni kuwafunza kuzitoa, na kama ni mcahanga
basi watake kuwa makini kuchambua maana mawe mengine ni yale meupe, kwa hiyo
yanafanana kwa karibu na mchele, lakini pia kama ni vigumu, wafunze kupembua au
kuuchambua wakati wanauosha na maji, njia ambayo ni salama zaidi.
Maharage yakiwa na mchanga au mawe, hayamwagwi, bali
huchambuliwa! Na wewe ukiona dosari katika hudumka na karama hizi, hakikisha
unazikabili!
Maandiki yako wazi kabisa katika biblia kuwa
tunatakiwa kujifunza na kuhakikisha kuwa tunasoma alama za nyakati, au tunajua
mabadiliko kwa kuzitambua dalili zake, mkulima asipojua kusoma uso wa nchi,
hakika atakuwa akipitwa na maamuzi dhabiti katika majira husika, wakati wengine wanandaa mashamba yeye atashindwa kufanya hivyo, ama atajikuta
akiwacheka wengine, maana kwa wengine ili walime ni hadi waone mvua imenyesha bila
kujua kwa kufanya hivyo ni gharama zaidi maana aridhi husumbua kwani kulima
kwenye tope ni kugumu zaidi! Pia ipo hatari ya kushindwa kufanya vyema maana
kuna uwezekano wa kunyeshewa! Kuna kuchelewa pia kupanda, maana wakati wa
kuotesha wewe ndo kwanza unakwatua udongo.
Jumapili, 17 Januari 2021
kitabu cha UKULIE WOKOVU

Jumapili, 1 Novemba 2020
MATESO, MAPITO SIO ISHARA YA KUPUNGUA, KUFIFIA AU KUTOKUWEPO KWA PENDO LA KRITO PAMOJA NAWE.
Na Mwalimu Oscar Samba.
Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu chetu cha MUNGU ANAKUPENDA, chenye mukutadha wa kukujulisha hata katika taabu yako pendo lake lingali lipo hapo!
Wiki hii, (wakati
mada hii inaandikwa) nilimuliza Mwalimu anayetufundisha kitabu cha Matendo ya
Mitume swali gumu sana, ambalo lilisadifu ujumbe huu ambao ninauleta mbele yako
siku ya leo!
Nilimuliza ama
nalitaka kujua kuwa kweli ni Mungu huyu huyu liyejifunua kwa Stefano wakati anapiga
mawe! Stefano anasema anamuona mwana wa Adamu au wa Mungu katika mkono wa
kuume, tena tunaambiwa alikuwa amejaa Roho, kwa hiyo utatu mtakatifu ulikwepo
ukimtazama au uwepo wake ulikwepo pamoja naye!