Jumamosi, 6 Machi 2021

Muombee Elia ama Yusufu wako, Ni Msaada wa kutoka kwenye Majanga kama ya Corona. #Corona #Covd19

 nA mWALIMU oSCAR sAMBA

Ujumbe huu ni sehemu ya #kitabu chetu cha MAMBO MUHIMU YA KUFANYA AU KUZINGATIA KUNAPOKUWA NA ADHABU YA KIUNGU INYOIJUMUISHA ENEO ULILOPO AU JAMII

18. Muombee Elia ama Yusufu wako; Kuna mtu MUNGU amemuweka ili kukuvusha ama kulivusha taifa na hata dunia kwa ujumla! shida kubwa ya wapendwa ni kwamba katika mambo kama haya kuomba kwa maarifa kumekuwa ni tatizo kubwa sana kwao! Wamisri walivushwa kutokana na akili, na hekima, pamoja na Roho wa Bwana ndani ya Yusufu kama Farao anavyokiri kwenye ile Mwanzo 41, kuwa hapana mtu mwenye akili, hekima na Roho wa Bwana ndani yake kama Yusufu! Ina maana gani! Kama Misri na dunia ya kipindi kile ilivushwa katika janga la njaa kutokana na sifa hizo zilizopelekea uwekaji wa akiba, basi na wewe muombee mtu ambaye mbingu zimemuandaa au kumtazamia kama sehemu ya majibu ya janga husika, kama ni la njaa, sawa, kama la kijografia pia sawa. Mfano kama ni la ugonjwa, ambao tena hauna dawa au kinga, waweza muombea Mungu ampe maarifa zaidi, na uwezo zaidi ama kuwaombea wanasayansi wapate maarifa zaidi ya kuwawezesha kugundua chanjo sahihi, na yenye uwezo stahiki, na isiyo na madhara katika mwili wa mwanadamu. Pili wagunduwe dawa, au tiba, huku ukiombea na viwanda vunavyotengeneza au vitakavyotengeneza dawa hizo, na vifa ambazo pia hutumika kipindi kama hiki, pamoja na kuwaombea madakitari na wauguzi ulinzi maalumu, maana nini kitatokea kama ukienda hosipitalini na kukuta madakitari na wauguzi wote hawapo ama wamaelemewa na wagonjwa kuiasi cha kushindwa kukusaidi na sababu ni baadhi yao kufariki!
Waombee pia wafadhili wataojitoa kwa fedha zao ili kuwezesha upatikana wa dawa hizo na vifaa pamoja na kuchangia gharama ili watu wengine wazipate, na huku sio kupungukiwa na imani bali ni kiroho kabisa. Kuweka akiba kwa Yusufu ni jambo la mwilini, na dawa pia ndivyo ilivyo, sayansi ni kiroho kabisa. Sasa tumekuwa na injili ambayo huiita injili makorokocho, kuwa hata chanjo ni pepo, hususani za ambao unaendeleao sasa, kuwani njama za watu wa mataifa fulani wanaotaka kutuua! Unafikiria mwenye fikra kama hizi ataombea sayansi isaidie kupembana na tatizo kweli! Maelekezo ya Paulo mtume kwa Timotheo kutumia mvinyo ilikuwa ni sayansi, maana kuna tiba hapo! (Sasa sina maana na kwako ufanye hivyo la!) Ila ninataka uione nafasi ya sayansi katika mambo kama haya! Tunajua kwa Yesu kumpaka mtu tope na kumtaka akanawe na Isaya kutumia makate wa tini ilikuwa ni ufuno sawa, ila sayansi nayo ni kiroho, waombee wafunuliwe dawa!

Jumamosi, 27 Februari 2021

Kitabu chetu cha: MAMBO MUHIMU YA KUFANYA AU KUZINGATIA KUNAPOKUWA NA ADHABU YA KIUNGU INYOIJUMUISHA ENEO ULILOPO AU JAMII.

Na Mwalimu Oscar Samba 

Neno Kiungu huwakilisha kutoka kwa Mungu au Shetani, ujumbe huu ni sehemu ya hiki kitabu chenye mada na pwenti kadhaa, ila hapa nimezicha,bua mbili tu; #Corona #Covd19 #Tsunam #Majanga  #Kimbunga #magonjwayamlipuko  #tanzania

1. Lifanye Eneo Unloishi kuwa Ghosheni yako. 2. Ijue na Uitumie Damu ya Yesu ya Pasaka; 3. Mulize Mungu kama Daudi; 4. Litengenezee Kusudi la Mungu Kisafina kama Musa, ama Nuhu; 5. Jifunze Jambo kwa Mke wa Lutu;

6. Sadaka kama Ulinzi; 7. Sadaka kama Sehemu ya Rehema, Mfano ile ya Daudi kipindi cha adhabu ya Tauni, 8. Taka Kujua pigo Hilo au Adhabu hiyo Inataka nini ili Ujisalimishe kwa Bwana, Mfano Rahabu, na Epuka kosa la Farao.

 9. Yajue na Uyaombe Maombi ya Musa ya Kulitengeneza Boma, 10. Mtafute na Umuondoe Akani, 11. Jitenge na Kusanyiko, au Kiunganishi cha Kusanyiko ama Waadhibiwa, ondoa jina lako kwenye watu wanaotakiwa kupewa hiyo Adhabu kwa Damu ya Yesu.

 

12. Tafuta Maelekezo Maalumu ya Mungu juu yako, kama Isaka dhidi ya Janga la Njaa na Wazazi wa Yesu. 13. Unapoisikia Hofu Usiipuzie, Taaka Kujua ni Aina gani ya Hofu ala Uikabili..

 

14. Tafuta Kukumbuka kama Mungu Aliwahi Kukujuza hapo Awali na Hukumsikia Vyema au Hukumbuki. (Amosi 3:7 Hakika Bwana MUNGU hatafanya neno lolote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.) Sijui sana ni kwa nini kanisa la leo lina uzito kwenye hili,  nijualo ni kwamba uwezo wa kusoma alama za nyakati, au majira umekuwa ni adimu sana kwa kizazi cha leo! Nafahamu kuwa hali ya kupuzia ndoto, kutokutambua jinsi Mungu anavyoongea, na mafundisho manyonge kuhusu uhusiano wetu na Roho Mtakatifu ni miongoni mwa sababu ambatanishi.

 

Kama kuna mahali Shetani amefanikiwa leo ni kuondoa, ama kuzimisha kama sio kufifisha karama ya unabii, na huduma ya nabii, pamoja na neno la maarifa!

 

Na anatumia njia kuu kama mbili hivi, moja ni kuhakikisha kanisa linapoteza imani na manabii au wanaotumiwa na karama hizi, kwa kujiwekekea manabii wa uongo, ili kuwakatisha watu tamaa na kuwafanya wa waone hata wale wa Mungu nao ni kama hao wengine!

Pili analitumia kanisa lenyewe, kwa kufikia hatua ya kupinga, na kukataa, na kuzimisha huduma na karama hizi, na sababu zao ni nyingi ila hazina hoja timilifu kibiblia, maana kama kuna wimbi la mafundisho na huduma potofu, suluhu bado sio kuzima na kukataa ile ya kweli, bali wafunze watu namna ya kutambua kweli na uongo. Mchele ukiwa na chuya, dawa sio kukataza nyumbani wasipike tena mchele bali ni kuwafunza kuzitoa, na kama ni mcahanga basi watake kuwa makini kuchambua maana mawe mengine ni yale meupe, kwa hiyo yanafanana kwa karibu na mchele, lakini pia kama ni vigumu, wafunze kupembua au kuuchambua wakati wanauosha na maji, njia ambayo ni salama zaidi.

 

Maharage yakiwa na mchanga au mawe, hayamwagwi, bali huchambuliwa! Na wewe ukiona dosari katika hudumka na karama hizi, hakikisha unazikabili!

 

Maandiki yako wazi kabisa katika biblia kuwa tunatakiwa kujifunza na kuhakikisha kuwa tunasoma alama za nyakati, au tunajua mabadiliko kwa kuzitambua dalili zake, mkulima asipojua kusoma uso wa nchi, hakika atakuwa akipitwa na maamuzi dhabiti katika majira husika, wakati wengine wanandaa mashamba yeye atashindwa kufanya hivyo, ama atajikuta akiwacheka wengine, maana kwa wengine ili walime ni hadi waone mvua imenyesha bila kujua kwa kufanya hivyo ni gharama zaidi maana aridhi husumbua kwani kulima kwenye tope ni kugumu zaidi! Pia ipo hatari ya kushindwa kufanya vyema maana kuna uwezekano wa kunyeshewa! Kuna kuchelewa pia kupanda, maana wakati wa kuotesha wewe ndo kwanza unakwatua udongo.

 Hosea hufananisha jambo la kuukwatua udongo sawa na kuomba, maana husema tumtafute Mungu, akitangulia na kututaka kuukwatua udongo wa mashamba yetu! Kiroho kuna vipindi kama hivi! Kuna kipindi cha kumtafuta Mungu kabla ya adahabu haijaja! Ukichelewa gharama yake ni kubwa sana! Unaweza kujikuta umeshapoteza ndugu wengi, ama hasara kubwa imeshatokea!

 Mama yangu wakati ugonjwa huu unaingia au umeanza kushamiri, ndipo aliponitaarifu kuhusu ndoto aliyowahi kuiota! Japo hakuwa ameielewa kipindi hicho! Ila nataka ufahamu kuwa Mungu alikuwa ameshaongea naye!

 Elimu na ufahamu wa kuzijua nyakati ni muhimu sana, na ni kiroho kabisa, jihakikishie kwa watu hawa, ambapo hata leo makanisani wapo, na kama hawajafungwa

Jumapili, 17 Januari 2021

kitabu cha UKULIE WOKOVU

#Habari-Njem ni kwamba, tumefanikiwa kutoa kitabu cha UKULIE WOKOVU, Kimetoka kwa njia ya PDF, tayari kwa ajili ya kusomwa kwenye simu na kompta, bei ni shilingi 5,000 za kitanzania; ukikihitaji wasilaina nasi kwa simu +255759859287, barua pepe: ukombozigospel@gmail.com pia zidi kutembelea: www.ukombozigospel.blogspot.com

 

Jumapili, 1 Novemba 2020

MATESO, MAPITO SIO ISHARA YA KUPUNGUA, KUFIFIA AU KUTOKUWEPO KWA PENDO LA KRITO PAMOJA NAWE.

Na Mwalimu Oscar Samba.

Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu chetu cha MUNGU ANAKUPENDA, chenye mukutadha wa kukujulisha hata katika taabu yako pendo lake lingali lipo hapo!

Wiki hii, (wakati mada hii inaandikwa) nilimuliza Mwalimu anayetufundisha kitabu cha Matendo ya Mitume swali gumu sana, ambalo lilisadifu ujumbe huu ambao ninauleta mbele yako siku ya leo!

Nilimuliza ama nalitaka kujua kuwa kweli ni Mungu huyu huyu liyejifunua kwa Stefano wakati anapiga mawe! Stefano anasema anamuona mwana wa Adamu au wa Mungu katika mkono wa kuume, tena tunaambiwa alikuwa amejaa Roho, kwa hiyo utatu mtakatifu ulikwepo ukimtazama au uwepo wake ulikwepo pamoja naye!

 

Jumapili, 11 Oktoba 2020

MAJIRA YA KULISIMAMISHA JUA. Ni semu ya Hiki kitabu

 Na Mwl Oscar Samba, 

Lengo: Kukujengea Kiu ya KuhakikihaMiujiza na Ishara na Matendo ya Mungu ya Ajabu Yanatendeka kwenye Huduma yajo kama Ilivyokuwa Kipindi ca Baba, na Mababu Zetu Kiimani.

Utangulizi

Mungu wa ma Mtendo ya Mitume ndie Mungu wetu! Wala hajawahi kubadilika, na jambo hili halitarajiwi wala kutazamiwa kuwa ipo siku itakuwa vivi, maana imenenwa hivi; Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele. Waebrania 13:8.

Ile ishara za Mungu hazijawa halisi kwako haina maana kwamba Mungu amebadilika, kaishiwa nguvu, ama amebadili utendaji na hata kufikiri kwamba ilikuwa ni kwa kipindi kile tu na kwa sasa haiwezekani, au inaonekana kwama Mungu hajaamua kufanya au kutenda kama hapo kale pia ni makosa tena mazito!

Jumapili, 27 Septemba 2020

MUNGU ANAKUPENDA KWA SABABU AMEANDAA MPANGO WA KUKUTOA KWENYE HILO JARIBU AU PITO.

Basi, Bwana ajua kuwaokoa watauwa na majaribu, na kuwaweka wasio haki katika hali ya adhabu hata siku ya hukumu. 2 Petro 2:9.

Wakati wana wa Israeli wanalia, wanalalamika, wanaumia ama wanaonyesha hisia zao kutokana na ugumu wa mateso yale ya nchi ya utumwa wa Misri, Mungu kwa upande mwingine alikuwa akitekeleza mipango ya kuwaokoa kwenye ile nchi!

Hakuna mtu aliyekuwa akiona, kutambua, au kufahamu kuwa upande wa pili Mungu alikuwa akimpatia Musa maelekezo ya namna ya kuwatoa kwenye ile ncchi!

Na hata kabla ya hapo, Mungu alikuwa akimuandaa Musa kwa ajili ya swala hilo, sio kwamba tu alilifanya hilo wakati Musa akiwa Midiani, bali hata kabla ya Musa kukimbilia huko Mungu alishamuandaa, ndio maana yale mahubiri yake kwenye kitabu kile cha Matendo ya Mitume yanaelelezea vyema kuwa Mungu alimuandaa huyu, ila hakumuelewa mapema, na wana wa Isreali hawakulielewa lile ndio maana walimkataa kwa wakati ule!

 

Jumamosi, 19 Septemba 2020

Kitabu cha USIFIE JANGWANI Mwalimu Oscar Samba Pdf

#Tangazo, Tunamshukuru Mungu kwa kufanikiwa kutoa kitabu hiki kwa njia ya Pdf, kwa hiyo kinaweza kusomwa kwenye Simu yako au Komputa, ukikihitaji utakipata kwa shilingi 50,000/ths. Tumia namba zifuatazo kufanya mawasiliano na malipo kwa M-Pesa, +255 (0) 756293767, jina ni Oscar Samba. Mwalimu Oscar Samba Tunajianda pia kukipeleka Amazon

 

Ijumaa, 28 Agosti 2020

Utangulizi wa Kitabu chetu cha UTUMISHI NA MTUMISHI

Mwalimu Oscar Samba

Luka 10:20 Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.
Ni kweli kabisa maandiko yanasema kuwa mtawatambua kwa matunda yao! Na mti mbaya au mwovu hauwezi kuzaa matunda mema, kwani tini huzaa tini wala zabibu haiwezi kuzaa michongoma, au kwa lugha nyingine huwezi kuchuma embe kwenye mti wa mchongoma au mchicha katika mbigili!
Lakini ukweli na uhalisia ni kwamba andiko hilo lina mukutadha wake na undani wake! Wengi wamekuwa wakiyatumia ili kuficha uhalisia wao bila kujua kuwa hawamdanganyi Mungu bali ni wanadamu wenzao, na hawa ni wale wasiojali sana hatima zao, yaani kwao maisha baada ya kufa sio kipaumbele chao kikuuu!
Kitabu hiki mpendwa kimebeba nia na kusudi la kuwasaidia watumishi, ili wasije kubweteka na utumishi walio nao, au wakifikiria kuwa utumishi ni tiketi au kibali cha kuwapeleka mbinguni, ni vyema kufahamu kuwa pasipo huo utakatifu haiwezekani kumuona Mungu!
Utumishi na Mtumishi maana yake ni kwamba hakuna uhusiano kati ya utumishi ulionao na wewe kumuona Mungu! Kuingia mbinguni kigezo kikubwa ni utakatifu au wokovu na sio jinsi gani unatumiwa na Mungu! Na kitabu hiki pia kitawasaidia wale watu ambao wanateseka na kuumia na kujiuliza maswali yasiyo na majibu kuwa inakuaje mtu anatumiwa na Mungu kwa ishara na miujuza, au kwa neno ambalo linawasaidia wengine na wengi kuokoka ama kufunguliwa lakini maisha yake mwenyewe binafsi ni machafu!
Sikatai kuwa kuna mapungufu, ambayo mtu huzidi kukamilishwa, au kuna kuanguka au kukosea kama Daudi alipolala na mke wa mtu, na kumua mumewe, au jinsi Musa na Haruni walivyokorofishana na Mungu, ama mapungufu kadha wa kadha ambayo pia tunayona kwa Petro!
Hapa ninanena habari za watu walioharibika mioyo kabisa, au ambao wapo katika kuharibika lakini kwa kuwa Mungu anajithiirisha kwao au kwa kuwa bado wamejaa Roho basi wanabweteka na hali hiyo, na kudhania kuwa Mungu hachukizwi na kosa au mwenendo wao!
Kuna muda utakatifu unaenda pamoja na utumishi! Ila kuna muda utumishi au mapenzi (kusudi maalumu) ya Mungu hutimizwa hata na chombo ambacho sio kisafi! Tutajionea kwa Balaamu, mtu mchawi aliyetumiwa kiunabii na kukamilisha makusudi ya Mungu, ila alikuwa mchawi na utumishi haukubadili maisha yake, lakini pia tutajionea kwa watu kama yule mganga wa kienyeji alivyo mpandisha Samweli nabii kutoka Ahera au kifuani mwa Ibrahimu, (Paradiso) lakini alikuwa ni mpunga pepe!
Nakutaka sana kuhakikisha kama kweli unataka kwenda mbingunbi basi unjitahidi kuulinda utakatifu! Na hii ilikuwa ni shabaha kubwa sana ya Paulo mtume, kuwa alilinda asije akawa wa kuwahubiria wengine na kisha yeye kuachwa! Nawe uwe makini, pepo kutoka sio kigezo cha wewe kuiona mbingu!
Ndio maaana furaha ya wanafunzi wa Yesu kuhusu ishara na ambao yaliyotokea haikuwa kipimo au kigezo chawao kuiona mbingu, bali furaha yao iliyopaswa kupimwa ni kwa kuwa majina yao yameandikwa mbinguni! Kuupata ulimwengu wote, kujaaa karama na kutenda miujiza hakuna faida kwako kama utapata hasara ya nafsi yako! Mathayo 16: Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake? 27 Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
Kilio chako kikubwa, na haja yako kubwa isiwe ni huduma yenye miujiza, ishara na umaarufu wa kiutumishi, bali utakatifu kwanza! Tafuta kumpendezesha Mungu kwanza!
Nayanena haya maana tumekuwa na watumishi ambao wapo tayari hata kutumia ushirikina ili tu wahakikishe wanapata nafasi fulani kwenye dini au dhehebu lake! Wapo ambao hutumia rushwa, na hata kampeni chafu ili tu kupata vyeo, wapo ambao hutumia hila wakifanya miujiza bandia ili tu wapate umaarufu na kadhalika!
Utakatifu kwanza, kisha vingine baadae! Tumekuwa na watumishi ambao hukandamiza vipawa au huduma za wengine kwa hofu ya kupinduliwa kiutumishi, na hata kuwatengenezea tuhuma au hila mabaya ili tu kuwachafua wengine kwa nia ya kulinda mkate!
Wapo ambao huhakikisha wanawaaribia wengine kwa lengo la kuchua nafasi walizo nazo! Wengine hutimia vibaya mahusioano yao na waangalizi, maaskofu au watu wenye dhamana husika ili kuwataka wamuondoshe ama wampe uhamisho mtumishi fulani kwa lengo la wao kukaa kwenye hiyo nafasi! Hii ni dhambi kama nyingine! Fahamu sana kuwa haki ni tabia ya Mungu, kutenda haki ni sehemu ya utakatifi!
Wapo viongozi ambao huonea wengine, wakikosewa au wakiona hawajatendewa sawa hata kama muhusika yupo sahihi basi kinachofuata ni wao kumuadhibu kwa kumuamisha au kumuondoa kwenbye vyeo fulani fulani! Huyu naye hatambua kwamba anapaswa kuhakikisha jina lake li mbinguni kwa kuwa mtu wa haki!
Mshirika! Kitabu hiki ni muhimu kwako pia! Maana unapaswa kuhakikisha kuwa unazingatia mambo ya adili au maadili ya kiroho kwanza na sio vinginevyo! Maana Yesu alisema kuwa napenda adili kwanza! Na katika Agano la Kale akasema anataka rehema kwanza! Kwa maana kwamba kuna vitu vya msingi ambavyo Mungu anavitazama, ili kukuhesabia haki!
Epuka sana mambo fulani fulani yakaonekana mema ila wewe ukakataliwa! Mungu alimkubali Habili, na sadaka yake, kwa hiyo angeweza kuikubali sadaka ya Habili, ila asimkubali Habili! Kwa Korinerio aliikubali sadaka yake/zake na kumkataa Korinerio! Kisha akahakikisha anamtuma Petro ili sasa sio sadaka tu zikubalike bali na kiroho cha Korinerio kikamilishwe! Sasa kwa Kornerio ilikuwa ni kesi tofauti! Kwako wewe uliyeijua kweli yote, ukiteleza/haribika hakika utakuwa kama Kaini, ambaye sadaka yake ilikuwa mbovu, ikakataliwa, na maisha yake yalikuwa mabaya pia nayo yakakataliwa! Sasa wewe usiishilie tu kuwa na sadaka njema, kuwa mfanya usafi mzuri kanisani, kumjali mchungaji wako na kusahau roho yako ! Ambapo hayo yatakubalika! Bali hakikisha na kiroho chako kipo vyema! Kwa hiyo kwa moyo mkunjufu ninakukaribisha humu kitabuni!
Kitabu kikitoka kitafute!
Hongera kwa kusoma ujumbe huu, nakutia moyo kuzidi kumtazama Mungu, na pia uwenda hujaokoka, yaani Yesu sio Bwana na mwokozi wa maisha yako! Nakutia moyo pia kuokoka sasa! Yamkini ni uchumi, fedha, hazipatikani, unazingirwa na nuksi na mikosi, kila unalofanya haliendi, unakabwa na mapepo, ! Wewe njoo kwa Yesu na hayo yote yatapita kabisa ! Sasa natumi u tayari!
Sema; MUNGU BABA, NINAKUPENDA, ASANTE KWA KUNIPENDA KWANZA, LEO NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NA NIPO TAYARI KUOKOOKA, TAFADHALI INGIA NDANI YANGU, SAMEHE DHAMBI ZANGU, NA FUTA JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKU, NA ULIANDIKE SASA KATIKA KITABU CHA UZIMA WA MILELE, Ameni.
Kwa kufanya hiyo umekwisha kuokoka sasa, na tafadhali tafuta kanisa la watu waliokoka lililopo karibu nawe ukasali, hapo, waambie kuwa umeokoa hivi karibuni, ili wakulee vyema kiroho.
Mawasiliano yetu, kwa M-Pesa au Simu: +255 759 859 287, barua pepe: ukombozigospel@gmail.com

PENDO LA KRISTO JUU YAKO NI LA MAFANIKIO


 Mpendwa nikutie tu moyo kuwa Yesu anakupenda, anakuwazia mawazo yaliyo mema, ni Mawazo ya Amani, Furaha, ana mipango mizuri juu yako, ni Mipango ya Kuinuliwa, Kufanikiwa, kama ilivyo nia yake katika 1 Yohana 3:2, kuwa anataka ufanikiwe kimwili au kifya na katika kila eneo la maisha yako ikiwemo uchumi, ndoa, huduma na kadhalika kama vile roho au nafsi yako ifanikiwavyo:

Hali ya mapito unayokutana nayo leo ni muhimu sana kufahamu kuwa ni ya muda tu! jangwa lipo ili kukufundisha na kukutengenezea mazingira mazuri zaidi kwa ajili ya Kanani yako! wana wa Israeli walipita hapo ili waweze kuishi vyema kwenye nchi ya Maziwa na Asali!
Nawe nchi yako ya maziwa na asali yaja ndiposa u ukipitishwa hapo!
La muhimu ni kuhakikisha imani yako haiyumbi, wana wa Israeli waliofia jangwani ilikuwa ni matokeo ya kutokuchanganya ile ahadi na imani kama maandiko yafunzavyo:
Lakini ukija katika Waebrania 3 na 4 utauona uapo wa Mungu pale kuwa aliwapia hawataingia rahani mwake kwa sababu ya kupungukiwa imani, na katika ile Hesabu 14 Mungu anamwambia Musa kuwa watu hawa watanidharau hadi au hata lini! Ikiwakilisha kuwa jambo la wewe kuogopa adui zako au vitisho katika safari yako ya kiroho kwa Mungu ni kumdharau ni sawa na kutokuliheshimisha jina lake!
Nikutie moyo kuwa kama wakina Yoshua na Kalebu na Musa na Haruni walivyosimama upande wa Mungu na kulitetea jina lake pale wakiwasihi wenzao wasimwasi Mungu wala wasiogope, na wewe hakikisha haumuasi Mungu nami ninakwambia kuwa usiogope maana uvuli uliokuwa juu yao umondolewa!
Jikaze kiume, jikaze viuno kama maandiko yatufunzavyo, kisha songa mbele! Mema yako yapo. majibu yako yapo. Ushindi wako upo, la muhimu ni wewe kujipa moyo!
Fahamu sana kuwa Yesu anakupenda, na anakuwazia yaliyo mema, mapito ni ishara ya upendo huo, wala sio mateso, maana askari mzuri ni yule aliyeandaliwa vyema, na Mungu anataka uwe askari mzuri!
kama hujaokoka na umeusoma ujumbe huu na kufahamu jinsi pendo la Kristo lilovyokubwa kwako, na unataka kumpa Yesu maisha yako, basi nikupongeze na hongera kwa hatua hiyo, nakutaka kufuatisha nami maneno haya ya sala hii ya toba kw aimnai, na badaa ya hapo utakuwa umeokoka:
sema, MUNGU BABA, NINAKUPENDA, NINAKUTAKA UINGIA NDANI YANGU, ILI UFANYIKE KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINAAMINI KUWA YESU NI MUNGU, ALIKUFA NA KUFUFUKA, TAFADHALI FUTA JINA LANGU KWENYe KITABU CHA HUKUMU, NA ULIANDIKE SASA KWENYE KITABU CHA UZIMA WA MILELE, Amen.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo, kwa maombezi, ushauri na mahuburi au maswali wasiliana nasi kwa Simu namba: +255759859287, Emaili: ukombozigospel@gmail.com au tembelea www.ukombozigospel.blogspot.com

YESU ANAKUPENDA!

 Na Mwalimu Oscar Samba

Sijui kama unajua kuwa Yesu anakupenda! Ni hatari kujaribu kusema kuwa mbona ninateseka, mbona maisha ni magumu, sasa inawezekanaje Yesu anipende wakati huu ni mwaka wa .. sijapona?

Ukweli ni kwamba Yesu anakupenda, na kuteseka kwako ni wewe tu bado hujatambua unachotakiwa kufanya ili kukubaliana na pendo hili! Unajua ndugu yangu acha nikwambie ukweli huu, nikuweke wazi katika viwango hivi vya uwazi! Mungu ili afanye kazi kwenye maisha yako ni lazima wewe umpe nafasi!

 

Mungu ni tofauti sana na Shetani, Shetani huweza kulazimisha, anaweza kutumia hila na mbinu batili ili kufanya jambo kwenye maisha yako, ila ili Mungu akusaidie wewe unapaswa kumruhusu!

 

Mfano, kuna mama mmoja alitokwa na damu kwa muda wa miaka 12; kwenye biblia tunajuzwa hili jambo, muda wote huo alikuwa akiwaendea waganga wa kienyeji na matatibu wa dunia hii! Ila siku alipoamua na kudhamiria moyoni mwake kwa kulishika pindo la vazi la Yesu hapo hapo alipokea uponyaji, wake!

Sasa jionee! Ni kwamba kupona kwake, kulitokea pale ambapo aliamua, alidhamiria kumuendea Yesu; Luka 8:43  Na mwanamke mmoja, ambaye ametokwa na damu muda wa miaka kumi na miwili, [aliyekuwa amegharimiwa mali zake zote kwa kuwapa waganga] asipate kuponywa na mtu ye yote, 44  alikwenda nyuma yake, akaugusa upindo wa vazi lake; na mara hiyo kutoka damu kwake kulikoma.

 

Hapo pendo la Kristo linadhibitika ndani yake! Uponyaji unatokea, lakini sio kwamba Yesu alianza kumpenda alipomponya la! Upendo ulikwepo ila huyu mama alipoamua kukubaliana na pendo hilo ndipo alipopona!

 

Yesu alitupenda na alimpenda huyu mama hata kabla hajavaa mwili yaani hajaja humu ulimwenguni, na pendo hili linadhibitishwa na Uungu wote; Yohana 3:16  Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

 

Dhambi ilipoingia ulimwenguni pendo la namna hii ililijidhiirisha mara! Halikuanzia katika kuzaliwa kwa Yesu, bali hata Agano la mlima Sinai ni ishara ya hili pendo, Mungu alipochinja mnyama na kuwavika wakina Adamu nguo ilikuwa ni sehemu ya utendaji wa hili pendo! Mahali pengine kwenye biblia hujulikana kama neema, unapoona neema, uwe na hakika huwakilisha pendo la Kristo, tumeokolewa kwa neema tu, ama tumeitwa kwa neema tu, uwe na uhakika ni pendo lake!

 

Pendo hili haliwezi kujifunua kwako wakati ukiwa na shida unaenda kwa waganga wa kienyeji, ukiwa na mahitaji humulezi Yesu unawaeleza watu tu na kuishia hapo! Hutaki kwenda kanisani, maana huyu mama alimfuata Yesu kwenye kusanyiko, na penye kusanyiko maana yake ni penye uwepo wa Mungu, sasa kwenye ibada ndipo alipo Kristo!

 

Usiende kanisa ni kanisa, usiende kusanyiko ni kusanyiko, maana siku hizi watumishi wengi wa uongo wameibuka, tafuta kanisa la watu walio hai kiroho, mahali ambapo kiukweli hata akili na ufahamu wako wa kawaida unatambua hapo Mungu yupo, epuka mbwe mbwe za Shetani, na misisimko isiyo na Mungu ndani yake.

 

Yawe ni maombi yako na ni maombi yangu pia kuwa Mungu afunguwe macho yako ya ndani ili uweze kujua sehemu sahihi itakayokuwezesha kukutana na Yesu wa kweli, maana siku hizi kuna ma-yesu wengi wa uongo, hawamuhubiri Yesu mwenye kukemea dhambi, kwao dhambi ni sehemu ya ibada, hapo kimbia!

 

Ukiona huduma isiyokemea dhambi, hiyo imepotoka, ukiona huduma ambayo wazinzi na walevi wamo humo humo na ni watumishi, hapo kimbia wala usiage! Ukiona mtumishi anawataka washirika wake kimapenzi ujue huyo ni “ajenti” ama wakala wa kuzimu, na ukimkubalia atakuunganisha na kuzimu moja kwa moja, kwani mashariti yao moja wapo ya kuwaunganisha ni kulala na watu! Hususani wenye nyota ambazo zitawasaidia kuvuta watu makanisani! Epuka na kimbia hili!

 

Unajua kuna watu wanaenda kanisani ili kuirithisha nafsi yao kuwa nao wapo kanisani! Hii ni hatari sana, ni sawa na kunywa maji machafu ili tu uwe umekunywa maji! Ni sawa na kula mkapi au vyakula vibovu ili tu kukidhi hitajio la kula! Ukifikia hapo upo mahali pagumu sana!

 

Maana baada ya muda afya yako itakongoroka tu! Wengine huabudu kwa kufuata mkumbo! Yaani ni mtumishi yupi anawika sana mjini siku za leo, akipoa au akiona ushabiki umempungua basi hufikiri kuhama hapo! Akiibuka mwingine mjini, humfuata!

 

Watoto hata! Shetani huwa naye anahubiri, tena ni muhubiri mzuri tu! Ukipinga muendee Yesu kwenye Mathayo na Luka 4, utamuona Yesu akihubiriwa na Shetani pale, na maandiko anamsomea, kuwa akiwa ndie Mwana w aAdamu ageuze jiwe kuwa mkate, na alimuonyesha hata utajiri alionao akimpa na kanuni kuwa akimsujudia atampatia!

 

Sasa usitishike na injili za mafanikio, maana hawakuanza wao alianza Shetani, na kupata fedha au mafanikio kutoka kwao sio jambo la kigeni, maana hata Yesu angemsujudia hakika angepewa, maana ni muhimu kujua nao huwa wanamsujudia nani!

Kusoma maandiko na kuyafafanua siyo kipimo, kwani hata Shetani alimsomea Yesu, maana ni kweli yapo kwenye biblia! La muhimu na jambo zuri kuliko yote ni wewe kuhakikisha kuwa ndani yako unapata amani ya Kristo, maana wapo ambao Mungu anawakosesha amani na mtu husika ila kwa ushabiki huzidi kugandamana naye! Huku ni kupotea!

 

Injili ambazo jina la Yesu limewekwa kando, msisitizo wa maombezi sio katika jina la Yesu na Damu yake kwenye uhalisia, ama nguvu za Roho Mtakatifu, bali ni katika viambatanishi, au visaidizi, kama mafuta ambayo yamesingiziwa kuwa ya upako, na wengi hawataki kujua kama ni upako upi unaotajwa hapo, maji ya upako au maji ya baraka, wengine wanagawa hadi bangili za upako, pete za upako, nasikia siku hizi kuna keki za upako,  hii ni hatari sana!

 

Najua wana wa upotevuni ni wepesi sana kukinzana na ukweli huu, na wana hoja nyingi sana wakitumia maanadiko, ila mioyoni mwao wanaujua ukweli, maana sifa zipo kwenye mafuta na maji yakaniponya, Yesu amekuwa kama ni msaidizi!

 

Nisikilize, ukitaka kuliona pendo la Kristo likikusaidia maishani mwako ni muhimu sana kuhakisha kuwa unaambatana na Yesu kama alivyo, waepuke wanaokupa maji machafu, katika Yohana 7:38-39 Yesu anaita akiwataka wale wenye kiu waje au waende kwake ili awape maji!

 

Maji yake ni safi, alimwambia yule mama kwenye kisima cha Yakobo katika Yohana 4 kuwa kiyanywa hayo maji ya Yesu hataona kiu tena! Sasa wamekupa Yesu na bado kiu ya ulevi ipo, wamekupa Yesu na bado una kiu ya kuiba waume za watu! Ukimuona mume wa mtu mate yanakutoka kama fisi na mfupa! Wamekupa Yesu angali bado una kiu ya dogo-dogo, ukimuona kijana “handsame” ama binti mrembo, hata kama ni umri wa mwanao jicho linakutoka kama vile fundi simu aliyedondosha nati, maana nati zake ni ndogo kwa hiyo asipotoa macho hawezi kuziona kirahisi, huu akiwa na hofu usikute imepotea!

Unasema eti umeokoka, au unamependa na una Yesu, sawa sikataii! Lakini mbona hajaondoa kiu ya dhambi nadani yako! Bado ni mwizi, unazini kwa siri, nyumba ndogo kuacha umeshindwa! Hakika huna Yesu aliyehai una yesu marehemu! Wala usinikunjie ndita, ila ukweli ndio huo!

 

Anasema hivi; Yohana 4:13  Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena.

Yesu akiingia nadani yako, na kiu ya mambo ya dunia ispoondoka, uwe makini, rejea msalabani upya!

Neno la Mungu ni maji, sasa injili kama inahubiriwa haibadilishi maisha yako, kuna mambo mawili hapo makuu, wewe mwenyewe u na moyo mbovu, ama injili unayopewa ni maji machafu, ni maji yasiyo na uwezo wa kukausha kiu ya dhambi, na tamaa zake, swala la upinzani wa Shetani hili ni la maombi tu! Ila hatuwezi au maombi hayawezi kukusaidia sana kama wewe mwenyewe hujakaa eneo salama, maana pepo mchafu amtokapo mtu na akipata mwanya mwingine hurejea, maandiko husema mmekuwa safi kwa lile neno, neno hukuweka kuwa safi, na mapepo hayakai maeneo ambayo yamesafishwa kwa Damu ya Yesu!

Huwa nasema kuna yesu aliyekufa, na kuna Yesu aliye hai, unaposema nataka kumuona Yesu, nina haja na Yesu, uwe makini maana wakina Pilato wapo hapo kukupa yesu aliyekufa kama Yusufu wa arimathayo, huyu alipewa Yesu/yesu ila mfu, aliyempatia alihakikisha kuwa amekwisha kufa! Na aina hii ya Yesu hawezi kuleta mabadiliko kwenye maisha yako!

 

Unasema una Yesu lakini hatuoni badiliko la ndani; ndani yako, una sema una Yesu lakini hatuoni matokeo ya wewe kuhuishwa hata kidogo! Yesu aliye hai, hukushindia dhambi, huhuisha utu mpya na kuua ule utu wa kale, hawezi kuchangamana na dhambi! Ukiona unajiita una Yesu lakini hakuna badiliko la dhambi au la kiroho ndani yako uwe na hakika kuwa kuna shida ipo mahali, utakuwa wamekupa yesu aliyekufa siyo Yesu aliye hai kama Yule aliyefufuka siku ya tatu, maana kuna dini zina yesu sawa, ila ni yesu marehemu!  

Wanahubiri habari za Yesu, Lakini wao wenyewe ni wazinzi, ni walevi, hawawezi kusimama madhabahuni bila kunywa pombe kidogo, hawawezi kukaa bila kutongoza washirika! Ni mzee wa kanisa ila sigara anavutia chooni!

 

Ona hapa; Marko 15:44  Lakini Pilato akastaajabu, kwamba amekwisha kufa. Akamwita yule akida, akamwuliza kwamba amekufa kitambo. 45  Hata alipokwisha kupata hakika kwa yule akida, alimpa Yusufu yule maiti.

Kuna dini, zimehakikisha kuwa yesu waliye naye amekwisha kufa, ndio maana wamekupa wewe! Maji yao siyo yale halisi yenye uwezo wa kuondoa kiu ya dhambi, ndio maana wamekupa wewe!

 

Huwa ninaweka sana angalizo hili, kuwa unapokuwa na kiu ya kutaka kumjua Yesu, unapokuwa na kiu ya kutaka kukoka, unapaswa kuwa makini tena mno, maana ukisema nina kiu, moja kwa moja uwe na hakika kuwa wapo watu ambao hawaachi kukuletea maji, ambayo kwa kweli siyo sahihi, ndio maanaYesu kwenye ile Yohana akapaza sauti aksema kila mwene kiu na aje kwangu, aje anywe, hakusema na aje achote maji ila alisema na aje kwangu, kwa hiyo jifunze kumtafuta Yesu kwanza, na sio maji kwanza , kama wengi wafanyanvyo! (Maana ukiwa na Yesu, atakwambia haya maji uliyopewa siyo yangu.)

Najifunza sana kwa Yesu mwenyewe, alipokuwa pale msalabani na alipopatwa na kiu, alisema naona kiu, na badala ya kumletea maji walimletea siki! Uwe na hakika na wewe ukisema nina kiu, wapo na watu ambao nao watakuletea siki ama maji machafu!

 

Ukisema nataka kuokoka, ninamtaka Yesu watakwambia usiondoke kwenye dini yetu maana na huku pia watu wanaokoka, kuna vikundi huku nako vya uaomsho, uwe na hakika ni uamsho bandia, maana kuna na moto bandia, ambao hufananishwa na ule wa Roho Mtakatifu!

 

Namtaka Yesu, wanakuletea Yesu ambaye amekufa, hawezi kuondoa dhambi! Ndio maana adui ameweka utitiri wa madhehebu na makanisa mapya na watumishi wengi, ni ili kuwapoteza watu, maana ma-yesu wafu wamejaa sana humu duniani! Umakini unahitajika sana!

Asante kwa kunisikiliza (nafsini mwako), ama kunifuatilia kwa njia ya usomaji huu wa hii makala, nina amini kuwa kuna kitu umekipata hapa, Yesu anakupenda, ila kama hujakutana na pendo lake uwe na hakika kuna dosari ipo mahali, chukua hatua mapema mnoo!

Pia anasema kwamba mtu akimpenda atazishia amri zake, kwa hiyo kama kweli umedhamiria, mpende kwa kuzishika amri zake, epuka michanganyo, epuka kuuzoelea wokovu, asante na Mungu akubariki mno; Yohana 14:23  Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake. 24 Mtu asiyenipenda, yeye hayashiki maneno yangu; nalo neno mnalolisikia silo langu, ila ni lake Baba aliyenipeleka.

Hongera kwa kusoma ujumbe huu, nakutia moyo kuzidi kumtazama Mungu, na pia uwenda hujaokoka, yaani Yesu sio Bwana na mwokozi wa maisha yako! Nakutia moyo tena kuokoka sasa! Yamkini ni uchumi, fedha, hazipatikani, unazingirwa na nuksi na mikosi, kila unalofanya haliendi, unakabwa na mapepo, ! Wewe njoo kwa Yesu na hayo yote yatapita kabisa ! Sasa natumi u tayari!

Sema; MUNGU BABA, NINAKUPENDA, ASANTE KWA KUNIPENDA KWANZA, LEO NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NA NIPO TAYARI KUOKOOKA, TAFADHALI INGIA NDANI YANGU, SAMEHE DHAMBI ZANGU, NA FUTA JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKU, NA ULIANDIKE SASA KATIKA KITABU CHA UZIMA WA MILELE, Ameni.

 

Kwa kufanya hiyo umekwisha kuokoka sasa, na tafadhali tafuta kanisa la watu waliokoka lililopo karibu nawe ukasali, hapo, waambie kuwa umeokoa hivi karibuni, ili wakulee vyema kiroho.

Mawasiliano yetu, kwa M-Pesa au Simu: +255 759 859 287, barua pepe: ukombozigospel@gmail.com

pia temnbelea: www.ukombozigospel.blogspot.com .

Alhamisi, 25 Juni 2020

UWE HODARI, SHUJAA NA MOYO MKUU.



Na Mwalimu Osacar Samba
Kuna kipindi nilipitia mahali pa gumu sana, na kutamani kufa, ama kujiua, ilifika mahali nikiwa napita mjini nilitamani kujirusha mbele ya gari ili nife! Moyo wangu ulipoteza matumaini kwa kiwango kikubwa sana! Ila kila nikitaka kufanya hivyo mbele yangu kwenye ulimwengu wa roho na kwenye mawazo yangu au nafsini mwangu nilikuwa nikiletewa picha ya watu ambao wamekwama mahali na kisha sauti kuniambia kuwa hao watu wananitegemea au wananingojea mimi! Nikikwama na wao watakwama!

Wakati namsimulia mshirika au kijana wangu mmoja aliniambia kuwa, “sasa mchungaji hauoni kuwa hao watu ndio mimi! Kama ungejiua leo ningepata wapi huu msaada!” nilifikiri kwa kina na kulitia jambo lile moyoni mwangu!


Sasa leo asubuhi (siku ya mwanzo ya uandishi) nikiwa hapa darasani, wakati naongoza maombi nilisukumwa kusoma andiko la kitabu cha Yoshua, 1:6-8; ambapo Roho alinifunza kitu kigumu kiidogo, kwamba ni Yoshua ndiye aliyepewa jukumu la kuhakikisha wana wa Israeli wanavuka salama!

Jumamosi, 20 Juni 2020

Usizike Ndoto Zako.



Na Mwalimu Oscar Samba
Utangulizi
Ninamshukuru Mungu kwa kibali na upendeleo alionipa kuhusu kitabu hiki, ni kweli nimeandika vitabu vingi ila hiki kinaupekee wa aina yake! Vipo vingi kweli vyenye kutia moyo watu, ila hiki nacho kina kitu chake cha upekee.

Kitabu hiki kinaitwa USIZIKE NDOTO ZAKO, haikuwa jambo la akili zangu kukipata, nilikuwa najisomea darasani muda wa usiku, na ghafula nikasikia Roho Mtakatifu anaugua, nilijitahidi kuhakikisha kuwa ninamaliza kwa haraka ratiba yangu ya kuhakikisha nasoma biblia kabla ya kwenda kulala maana niligundua moyoni kuwa muda wangu wa kukaaa darasani umeniishia!

Lakini haikuwa rahisis kukubaliana na wazo hili la Roho Mtakatifu maaana nilitakiwa au nilihitajika kusoma zaidi kwa mujibu wa ratiba yangu, natumai ndio maana aliamua kutumia njia ya kuugua ili kunishindikiza!

Alhamisi, 4 Juni 2020

NGUVU YA MAOMBI YA KUOMBA BILA KUKOMA


Na Mwalimu Oscar Samba:
“Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.” Luka 18:1.
Nina kusalimu ndugu yangu kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo! Ni yangu matumaini ya kuwa u mzima tena buheri wa afya tele, na kama sivyo basi Bwana wetu Yesu Kristo aipatie nafsi yako amani, na faraja tele. Na kama ni uponyaji au haja fulani, ipokee kwa imani sasa!
Siku ya leo hapa mtandaoni nimekuandalia ujumbe huu muhimu sana, wenye mukutadha ama sura ya kukutaka kuona umuhimu wa maombi ya nayoombwa bila kukoma, au kukata tamaa!

Ijumaa, 27 Machi 2020

Mwalimu Mwakasege Atoa Wito wa Kushiriki Maombi Dhidi ya Ugonjwa wa Korona

Anaandika katika mtandao wa kijamii ;
Bwana Yesu asifiwe.
Hili ni ombi kwa kila aliyewahi kuhudhuria kongamano letu,la maombi la kitaifa, tunalofanyia Dodoma kila mwaka. Lakini,hata kama hujawahi kuhudhuria kongamano hilo-ombi hili linakuhusu pia.Tunajua umekuwa ukiombea tatizo la ugonjwa wa 'Corona'. Pamoja

Alhamisi, 5 Machi 2020

MREJELEE YESU.


Na Mwalimu Oscar Samba
Waimbaji wakaimba; “Kale nilitembea Nikilemewa dhambi
Nilikosa msaada, kuniponya mateso.
Usifiwe Msalaba! Lisifiwe kaburi!
Linalozidi yote, Asifiwe Mwokozi!

Shalom Mwana wa Mungu, kwa moyo mkunjufu ninakukaribisha katika Makala hii murwa, yenye nia ya kukufanya umrejelee Yesu, ujumbe huu nimeupata usiku wa kuamkia leo nilipokuwa nimelala, ulinijia kama maomo nami nalisikia sauti hii, “mrejelee Yesu,” kisha na andiko hili kunijia; “Tangu wakati wa baba zenu mmegeukia mbali na amri zangu nanyi hamkuzishika. Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi,” asema BWANA Mwenye Nguvu.   ‘‘Lakini mnauliza, ‘Tutarudi  kwa namna gani?” Mlaki 3:7.

Sijui ni jambo gani lililokutatiza kiasi cha kuiamcha Imani, kiasi cha kuamua kurudi nyuma kiroho, kiasi cha kukataa kabisa au kukata tamaa moja kwa moja na safari hii ya wokovu ?

Yamkini unasema mimi sijarudi nyuma kabisa mtumishi, Yesu bado na mpenda, ila nimeishiwa nguvu za kiroho, nimejikuta sina tena kiu wala hamu ya maombi, nimejikuta nimekuwa mzito kusoma neno, na kuudhuria ibada ! Na hali hii ilianza tu pale mama yangu, mume aa muke alipofariki, ama mtoto, na mwingine labla ni baada ya kuugua, au biashara yake kufa ama kufukuzwa kazi, kusema vibaya na wapendwa, kuacha au kukosa msadaa, mwingine yamkini anasema ni mwaka wa sita sasa Mungu hajanijibu, amekaa kimya, hanisiki: kwa hiyo mtumishi hizo ndizo au ndiyo sababu kuu.

Alhamisi, 27 Februari 2020

JIFUNZE KUMTUMAINI BWANA.

Na Mwal Oscar Samba

“Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe” Mithali 3: 5.
Akili zako zinza mipaka, ufahamu wako kuna mahali unafikia ukingoni, utashi wako na upeo wako “ni-limited” nikiwa na maana kuwa kuna mahali unaishia, ila ukuu wa Mungu huvuka na ushinda ufahamu wote, ni yote katika yote.
“Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.” Isaya 40:28.
Embu nenda name sanjari katika andiko hili; “Msijisumbue kwa jambo lo lote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu/akili zote, itawalinda/hifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.” Wafilipi 4.6-7.

Ina maana kwamba, unapokuwa taabuni, au katika adha, kitu kimoja wapo Mungu anachokifanya ni kuachilia Amani yake, ambayo huzidi akili zako, na ufahamu wako, ikiwa na mantiki kwamba ukiiruhusu ndani yako, akili yako au ufahamu wako utapata utulivu, na njia moja wapo ya kuiruhusu ni moja tu ambayo ni kuweka Imani na tumaini lako kwa Mungu, ni kweli tumeumbwa ili kutumia akili ila sio kuitegemea, wa kutegemewa au kutumainiwa ni Mungu pekee !

Kwa nini ? kwa sababu akili na uelewa wetu huwa na mipaka ! madakitari hutegemea akili zao, ufahamu na maarifa yao, wakishindwa watakwambai hapa hatuwezi, wanasheria au mawakili watakueleza kuwa hapa haiwezekani, mazingira ya uchumi au kiuchumi, ama mapito kwenye ndoa, au ugumu fulani unaweza kufikia mahali na kukueleza au kukwambia kuwa hili haliwezekani tena ! ni kweli na ni jibu zuri kabisa maana akili zetu zina mipaka!

Jumanne, 12 Novemba 2019

USIFANYE HARAKA KUFUNGUA HUDUMA, KUHAMA KANISANI AMA KUACHA KAZI NA KUFUNGUA BIASHARA.

Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu chetu ninachoendelea naho cha: NAFASI YA VIUNGO VYA MWILI WA MWANADAMU KATIKA ULIMWENGU WA ROHO.

Na Malimu Oscar Samba:
12. Uwe na Subira, Saburi ni kitu muhimu sana, kuna wakati unakuwa katika vita vya kumiliki na kutawala lakini unakuta eneo unalotaka kumiliki au kuweka maskani yako bado hakuna nafasi, usiwe na haraka, wala usifanye haraka, endelea kuwa na uvumilivu, jambo la kuwekwa kwa adui chini ya miguu yako ni swala la mchakato, sio la siku moja, na swala la kukuwekea mazingira ya kuishi katika miliki yako kiroho iwe ni kihuduma, kiuchumi ama kiutumishi na kindoa na kadhalika linahitaji muda !

Jumatano, 30 Oktoba 2019

NGUVU YA KUWA NA UTULIVU MOYONI UNAPOKUWA KATIKA MAZINGIRA MAGUMU.

Ujumbe huu ni sehemu ya kitabu chetu cha Mungu yu Pamoja Nawe, pwenti ya nne, karibu: Na Mwalimu Oscar Samba.
4. Uwe na Utulivu Nafsini Mwako, kukosa utulivu maana yake ni kuwa na mahangaiko moyoni, ni kuwa na wasiwasi au mashaka, ni hali ya kujisumbukia au kuhaha.

Hali hii ni mlango wa dhambi, maana ni adui wa imani, humuondolea mtu uwezo wa kumtegemea Bwana, maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari liwezalo kupelekwa huku na kule na upepo !

Kukosa utulivu ni kukosa raha, ni kupungukiwa kwa kiasi kikubwa na amani, ambayo hiyo amani ni njia ya Mungu kuongea, maana maandiko husema kuwa na amani ya Kristo iamuwe mioyoni mwenu, kwa hiyo hayo mazingira humzuilia Mungu kuamua ndani yako, lakini pia amani ni njia ya Mungu kukuongoza, sasa ikipotea maana yake hutaiona njia, ndio maana dalili kubwa ya mtu aliyekosa utulivu na matokeo yake ni kuwa kama mtu aliyeko njia panda asiyejua njia ya kuiendea !

Jumatatu, 14 Oktoba 2019

HISTORIA YA WOKOVU, AMA SIMULIZI ya Uamsho wa MASAMA MUDIO. Sehemu ya 6, Zamani Enzi za Askofu Imanueli Lazaro

Utapatapia Unabii wa Askofu kuhusu kufa kwa zao la Kawaha, na Pigo kwa Uchumi wa wanaume na kuhamia kwa Wanawake.
.
Kulia ni Mwandishi wa Makala hii Mwalimu Oscar Samba akiwa na Msimulizi wetu Mch. Theofilo
Inasimuliwa na Mzee na Mchungaji Mstaafu wa TAG huko Masama, THEOFILO BARTOMAYO KIMARO, huyu ni pacha au ndugu na Mchungaji Wilsoni Kimaro.
Tuanze simulizi yetu; Niliokoka mwaka wa 1962 January na Mungu kuniita mwaka huo huo, niliunganika na kanisa huko Mbuguni, ambako kanisa nililikuwa halijaanza huko, (la wokovu) nilipokoka tukaanza kushuhudia nyumba kwa nyumba kama vijana.

Nakumbuka kuna mama mmoja kipindi hicho alishikwa na kansa, huyu mama sikuwahi kumuona kanisani maana alikuwa mgonjwa na alikuwa amekonda sana,

Jumatano, 2 Oktoba 2019

UJUZO WA HISTORIA YA UAMSHO WA MASAMA KAMA INAVYOSIMULIWA NA Afuraeli Munisi, Sehemu ya 5.

Anasema kuwa sio kwamba kanisa la TAG lilianzia hapa, lilikuwa limeshaanza huko Mbea hapa lilifika huo mwaka 1959, walianza kuokoka huko ni Askofu Lazaro na Jakobo Ringo ni mpare kutoka Same, walikutana na Askofu huko Arusha na mmeshenari Paulo Brutoni. ( Kama tulivyojionea hapo awali !)

Sikumbuki tarehe wala mwezi ila ni mwaka huo baada ya wao kuanza kushuhudia huko Arusha kidogo,hapo awali alikuwa ni mshirika wa KKT, na mama yake na baba yake pia, baba alikuwa ni mzee wa kanisa mtunza hazina wa hiyo dini, anaendelea kusimulia Mzee Munisi ! ( Ambae kwa sasa ni mzee wa miaka 83 na mke wake ni 72, aitwae Anarabi Afuraeli Munisi, ambao kwa kweli wamezeeka na mzee hapa huongea kwa utulivu maana pia sio buheri sana wa afya.)
Tunaendelea !


Walipokuja ndo walikuja